Fahamu asili na maana ya jina lako!

Ni vizuri kuelewa jina lako na maana yake, kuna mambo mengi hukutokea kwa uzuri au ubaya lakini yawezekana na jina lako linachangia au asili ya jina lako …Kuna wengi wetu wamepewa majina yao kutoka kwa mababu zao ambao walikua na roho fulani labda ya umasikini, uzinzi, magonjwa n.k. Wengine wamepewa majina kutoka kwa waganga wa kienyeji au mizimu, ndio maana kuna vifungo fulani unavyo kwenye maisha yako. Jina lako linang’ang’ania ubaki pale pale, hakuna kusonga mbele, wewe ni wa hivyo hivyo au unajimilikisha magonjwa  fulani kwasababu bibi au babu zako walikua nayo. Mfano unasema mimi ugonjwa wangu ni kisukari, TB au sie kwetu ndio ugonjwa wetu! nk

Jina lako lilivyo ndivyo ulivyo!

NABALI – 1Samweli 25:25 “Nakusihi, Bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma”.

Baadhi ya watumishi wa Mungu ambao majina yapo yalibadilishwa

YAKOBO – Mwanzo 32:26-28..”Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.  Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo. Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda”.

IBRAHIM – Mwanzo 17:4-6.. “Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi, wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi. Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako.”

Bila shaka unawafahamu wengi waliobadilisha majina yao na kubadilika kabisa kutoka mfumo wa maisha walikua wanaishi nawe unaweza kubadilisha jina lako au kuzuia nguvu zile zinazoambatana na jina lako zisiambatane na maisha yako Mithali 22:1..” Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu”. 

Nguvu ya majina mabaya tuliyopewa na wazazi wetu zisifanye kazi kwenye maisha yetu!

Zaburi 58:3..”Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo”.

Isaya 48:8..”Naam, hukusikia; naam, hukujua; naam, tokea zamani sikio lako halikuzibuka; maana nalijua ya kuwa wewe watenda kwa hila nyingi, nawe umeitwa mkosaji tangu kuzaliwa kwako”

Tukatae misingi mibaya ya majina yetu, tusimamishe kazi mbaya na kujenga majina yenye baraka na kibali katika maisha yetu. Barikiweni sana!

MD-

About these ads

95 thoughts on “Fahamu asili na maana ya jina lako!

  1. Bwana Yesu asifiwe!!

    Kweli kabisa majina yana mabo mengi sana. Mengi yanabeba historia za watu, hali zao na kadhalika. Ukigundua jina umepewa kwa sababu ipi, kama sababu ni mbaya, ikiwezekana badili.
    Bwana Yesu apewe sifa.

  2. Habari. mimi ni Mama mwenye watoto wawili. Naomba kujua nini maana ya jina JOAN na JOEL

    Nakutakia kazi njema
    kutoka kwa mama Joan

  3. Habari ya kazi ndugu yangu. Naomba kujua nini maana ya majina yafuatayo;
    1.Stephano
    2.esnath
    3.Stephen na
    4.Monica

    Nakutakia kazi njema.

  4. Hillary,

    Nimepata maelezo ya maana ya jina lako, HILLARY. Soma maelezo yafuatayo.

    “In English, the name Hillary means- Variant of Hilary: Joyful, glad. Cheerful. Derived from the Latin name Hilarius.. Other origins for the name Hillary include – English, Greek.The name Hillary is most often used as a girl name or female name.”

    Kwa anayehitaji kujua maana ya jina lake Unaweza kutembelea mtandao wa “meaning-of-names.com” kama ilivyoshauriwa pia na ndugu Saning’o Lenoi tarehe 20, Jan 2011.

    Asante.

  5. Shalom,mtumishi jina langu fredy linamanisha nini,kama alina maana nzuri ntawezaje kuribadili ili nipate jina jema.

  6. MAANA YA MAJINA YAFUATAYO, kama wasomaji walivyoomba:

    Henry = Teutonic (asili ya kijermani) meaning home ruler.

    George = the Greek georgos farmer or earthworker..

    Freddy = a peaceful ruler ..

    Jane = gracious, merciful, Jehovah has been gracious, Gift from God.

    Manfred = man of peace, Peaceful, Heros peace

    Lisa = consecrated to god

    Sabrina = princess, From the border, Legendary princess. .

    Janet = gods gracious gift, God has been gracious, A Gift from God.

    Geoffrey = gift of peace, Peaceful, Divine peace.

    Moses (Musa) = drawn out of the water, Saved from the water.

    Fahad = lynx panther { Mnyama jamii ya paka anayefanana na chui au simba}

    Latif = elegant, Delicate, gentle.

    Endelea kutembelea blog hii na umtaarifu mtu asiyefahamu!

  7. Hoja ya kubadilisha majina inahitaji kufanyiwa kazi,ni moja ya mafundisho yenye utata leo.

  8. naomba kufahamu maana ya majina yafuatayo:-
    JULIANA,BEATRICE, AMANI, PENDAELI, PETER, JOSEPH.
    asante sana Mungu akubariki

  9. Maana ya Majina yafuatayo:

    Juliana – soft-haired, yaani mwenye nywele laini.
    Beatrice – Bringer of joy, blesses: Mleta amani, baraka.
    Amani, Vumilia – Haya ni majina la kiswahili na lina maana kama linavyosema.
    Pendaeli – ‘Eli’ humaanisha Mungu na hivyo Pendaeli inaweza kuwa na maana ya mtu anayempenda Mungu. Pamoja na hili kuna majina kama Sifuel, Kundaeli. Wakati mwingine ni vizuri kuwauliza wazazi kwa nini waliita jina hilo.
    Peter – Jiwe, mwamba.
    Joseph – God will increase , May Jehovah add/give increase: Mungu ataongeza, Mungu aongeze.

  10. hi, naomba kujua maana, asili na watu wenye majina yafuatayo wanakuwa na tabia zipi: Catherine, Method, Pancras na Stanley

  11. (a) nini maana ya Isaack
    (b) kuna uwezekano wa asilimia ngapi mtu kuwa na tabia kulingana na jina lake?
    (c) kwa hiyo watoto wasiitwe majina ya kurithi mfano kumwita jina la babu au bibi yake?

  12. NAOMBA MAANA YA JINA (GEOFREY) NA (ANDREW) NA SANGA LENYE ASILI YA KIKINGA KWA KUWA MIMI NAITWA GEOFREY ANDREW SANGA NA JE JINA LA BABA AU BABU KAMA UBINI LINAWEZA KUKUADHIRI PIA

  13. Ni vizuri kujua maana ya jina, ndo unaweza kumpatia mtoto. Naomba kujuwa nini maana ya majina ya JESSICA, RABECCA NA PATIENCE.

  14. NAOMBA kujua maana ya jina Daniel, Evance, Sarah, Barnabas, Paulina na Amertha

  15. Bwana Yesu Asifiwe!!

    naomba kujua maana ya majina yafuatayo AIKAVIOLLA, STEVEN, GODSON, SHARON, SHEILA, STEWART, GAUDENSIA, NA GABRIELA. Nitashukuru sana kujua maana yake. kazi njema.

  16. BWANA ASIFIWE! NIMEPENDA GLOB YENU,NAOMBA KUJUA MAANA YA JINA LA” ASUMPTA” NA “TIMOTHY”

  17. blog hii ni nzuri actually. tunaomba isiishie kwenye maana ya majjina tu bali iende mbele na kuangalia all about the bible versus the practical life. hii ni kwa sababu we christian are tending to leave our endeavor out of our christian life . i love your blog, big.

  18. Emmanuel…!
    thanks God now I have pregnant I want to safe me and my baby please God guard me for everything and man of God help me for pray. And pray for my grandmother she is so sick since september 2010 up to now.
    GOD BLESS U…!

  19. kweli kuna majina mengne ni either majina yasiyoeleweka bt pipo ar kalin thea watoto mfano latoya and they dnt knw wat iz the meanin of t. And wen u fnd ts meanin unaweza kuta labda ni shimo la choo or any atha stpd thng kisicho na maana nzuri. So wapen watoto majina yanaeleweka na yenye maana ya ukweli na uwasilia. Mfano wa jina Emmanuel ni utukufu wa Mungu pa1 na wanadamu. Au weng ujua au kuklem kwakujua kuwa ni Mungu p1 nasi. Tchao!

  20. Maana ya majina umeitoa wapi mtumishi wa Mungu kwamba jina timo lina maana fulani kwa maandiko isije ukristo wetu tunautumia vibaya wasiokoka wakaogopa! Ni heli ukajitahidi ukaiambia jamii kitu ambacho hakina maswali mtumishi utaulizwa siku ile ulikuwa unafanya nini duniani ulikuwa unaiambia nini jamii; geuka huu ni utabili kabisa hamna tofauti na mganga wa kienyeji.

  21. Timothy
    majina yana maana, usimkatishe tamaa mpendwa, nakudhani waganga wa kienyeji tu ndio wanahitaji kujua maana ya majina.
    Nadhani unasoma biblia na kuielewa, umesikia wakiandika, Mungu wa ibrahim, Mungu wa Isaka na Mungu wa Jakobo, na wakiyataja majina yote kwa wakati mmoja. Kutaja huku majina kuna maana yake, kama mhubiri mmoja (Bayless Conley wa Answers Bc) alivyotoa tafsiri yake kuwa, Mungu ni wa watu wote kitabia, Ibrahimu alikuwa ni mtu wa Imani sana. Isaka alikuwa mtu wa kawaida kabisa, alikuwa na imani lakini sio kubwa kama baba yake. Yakobo, unamjua mtu wa mashaka, alimwambia mungu sikuachi usiponibariki, maana hakuamini kama atambariki asipomg’ang’ania, kuna wakristo wana imani lakini pia wana mashaka, hawaamini mpaka waone miujiza, (Yakobo) lakini kuna wanaoamini kabla ya miujiza kutokea (Ibrahim) kuna wapendwa wanaacha bila kung’ang’ania na mambo yao yanaenda vizuri (Isaka). hivyo unaposema Biblia ukiona yanatajwa majina haya matatu kwa wakati, ina maana anakusisitizia kuwa mungu ni wa wote.
    watu wanapotoa majina kwa watoto wao aidha walifurahishwa na yale yaliyomtokea yule mwenye jina, au wamelipenda tu jina hilo, au wanapenda mtoto wawe aje awe na imani kama ya yule mtu,
    blessings
    Greta

  22. Nadhani hoja hapa si maana ya jina ila asili ya jina ulilopewa wewe,yaani wazazi wako walifikiri nini walipokuwa wakikupa jina ,naona wengi wanauliza maana ya majina yao kama Jesca n.k hilo si la msingi sana jambo la msingi ni kujua ulipewa jina hilo kwa misingi gani?

  23. maaana ya jina george sija kubaliana nalo kwasababu nime pata maana nyingi kutoka sehemu mbal mbali

  24. Naomba kujua maana ya majina haya. Daniel and Regina and felista and clinton

  25. Nikweli majina mengine yamekuwa ni chanzo cha matatizo na hayo yametokana na uzembe na ukosekanifu wa uelewa wa wazazi we2,jina kama huzuni,shida,tabu,semen,nk.Eti wanabatizwa watoto kutokana na jinsi mama alivyo pata tabu enzi ya ujauzito huo.

  26. SI SAHIHI KUSEMA MAJINA YANA NGUVU YA NAMNA HIYO; HII HAINA TOFAUTI NA MAREHEMU SHEIKH YAHYA YA KUTABIRI NYOKA NA NDIO KIZAZI CHA NYOKA UKITAZAMA MIFANO ALIYOTOLEA YOTE NI AGANO LA KALE KWENYE BIBLIA NADHANI HATA KITABU KINACHOUZWA PALE MBOGO SHOP: KARUME KINGEPIGWA MARUFUKU HUU NI WIZI MTUPU; HAKUNA IMANI YA KIKRISTO KATIKA KANISA JIPYA INAYOZUNGUMZIA JINA; KAMA NDIO HIVYO TUSINGEKIWA NA MCHUNGAJI ABDALLAH; MCHUNGAJI SELEIMAN AU MCHUNGUJI ; MWAJUMA

    WAKRISTO MSIOGOPE NA KUDANGANYWA KWA UONGO UONGO WA MANABII WA UONGO :

    HAWA WAMEANDIKWA WATAKUWEPO NA WATAPENDA FEDHA KULIKO MUNGU SASA KUJUA JINA LAKO NA KUOKOKA KUNALETA MADAHARA GANI
    NAMALIZIA

    INJILI MBELE SHETANI NA FEDHA ZA WIZI NYUMA ANAYEBISHA ASHINDWE KATIKA JINA LA YESU WA NAZAREHTI ALPHA NA OMEGA ALIYE HAI.

    UONGO UONGO UONGO UONGO UONGO UONGO UONGO UONGO UONGO : MSIKUBALI KUTAPELIWA

  27. Amani na iwe kwenu ninyi nyote msomao ukurasa huu. ninaweza kusema kuwa ni muhimu kufahamu maana na asili ya jina lako, kwani kuna baadhi ya watu wenye majina fulani hawawezi kuepuka matatizo fulani. mfano:- watu wenye majina ya “MARIA”

  28. Website hii ni nzuri sana, kwani itamfanya kila mtu aweze kujua maana ya jina lake.mfano Emanuel means God with us.

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out / Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out / Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out / Change )

Connecting to %s