Mungu ni mwenye Rehema

Mch Piason Ndala wa Huduma ya Maombezi ya Matatizo Sugu na Ushauri wa Kibiblia (BCIC), Tawi la Temeke lililopo Mbagala Maji Meupe amewaambia waumini wa Huduma hiyo kuwa, “unaweza kuwa na sura nzuri kama malaika, kama huna rehema na kweli mbele za Mungu na wanadamu, wewe ni sawa na sifuri”

Mchungaji huyo ameyasema hayo jana wakati wa Ibada ya kumshukuru Mungu kwa matendo yake makuu aliyoyafanya katika Kitongoji cha Igonambogo, Kijijini Mayaha Kata ya Minyughe Tarafa ya Ihanja Singida Vijijini iliyohitimishwa na Mch Kiongozi, Mch Michael Peter Imani kwa waumini hao kumshukuru Mungu kwa maombi na kumtolea sadaka ya shukurani.

Mch Ndala akijikita katika somo lake, amewahubiri waumini hao na kuwaambia na hapa ninanukuu, “Unaweza kuwa na sauti nzuri kama chiriku, kama huna Rehema na Kweli, wewe ni sawa na sifuri”. Mwisho wa kunukuu. Akifundisha somo la Roho Mtakatifu, aliloliita, Rehema na Kweli, alisema, kweli Mungu ni wa Rehema. Kwa vile Mungu huwasamehe watu wenye makosa au waliotenda dhambi wakitubu na kuziacha, lakini kama ukitubu na kurudia tena dhambi, utaona Mungu alivyo mwenye hasira nyingi!

Huku akithibitisha mahubiri yake kutoka katika Biblia, alisoma kitabu cha kutoka 34:6-7 na kufafanua kuwa Mungu aliwatokea wana wa Israel katika Mlima Sinai, katikati yao katika wingu zito, akisema kwa mithili ya mchungaji anayemwongoza mwenye dhambi kutubu, Musa akafuatisha na kutangaza, Mungu ni mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, Akaendelea kusoma, mwingi wa rehema na kweli, mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa na hatia kamwe, mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.

Mchungaji huyo alihitimisha somo lake kwa kuwauliza wasikilizaji wake kama je, wanajua ni kwa nini shetani alikosa kibali kwa Mungu? Akajibu na kusema, shetani alikuwa ni muuaji tangu mwanzo, wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake, asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe. Kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo (Yohana 8:44)

Tukiwa ndani ya Yesu, sisi ni viumbe vipya!

Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! yamekuwa mapya” 2 Wakorintho 5:17

Kila aliye ndani ya Kristo. Amekuwa kiumbe kipya kwa imani, Sisi tuliookoka ni viumbe vipya, Sio wale wa zamani kabla hatujampokea Bwana Yesu, Utu wetu wa zamani umekufa, tumevikwa utu mpya! Je, unaendeleaje ndugu? Utu ule wa zamani au kwa utu mpya uliovikwa?

Bishop Lazaro Sese – KASHAI, BUKOBA

Nape Nnauye aalikwa Kanisa la Ufufuo na Uzima

Na Bashir Nkoromo

Katibu wa NEC ya CCM Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akipongezwa na Mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, baada ya kutoa mahubiri yake katika kipindi cha ‘Hekima za Viongozi’ alipohudhuria ibada ya Kanisa hilo  leo kwenye Viwanja vya kilichokuwa kiwanda cha kusindika nyama cha  Tanganyika Packers, Kawe mjini Dar es Salaam. Nape alihudhuria ibada hiyo kutokana na mwaliko wa kanisa hilo.

Mwaka 2012 ni Mwaka wa Kazi

“Mungu hatakupatia zawadi kwa kuwa umeokoka, bali kwa kuwa ulifanya kazi yake, kwa kuwa kuokoka ni kwa faida yako mwenyewe. Tufanye kazi ya kuujenga ufalme wa Mungu. Hata tunapofanya kazi zetu za kimwili, tukipata kipato zaidi, kipato hicho kitatusaidia katika kuifanya kazi ya Mungu kwa kiwango cha juu zaidi”

Tukisoma Luka 19:11-26 tunaona jinsi ambavyo watu walipewa fedha. Katika waliopewa fedha hizo wapo waliozalisha lakini kuna mwingine hakuzalisha chochote bali alificha na kuirudisha vile vile kama alivyopewa. Waliozalisha walipewa zawadi lakini yule ambaye hakuzalisha alinyang’anywa hata kile alichokuwa amepewa.

Fundisho kuu la maneno hayo ni kutuelekeza KUFANYA KAZI ili tuzalishe. Tuwe watu wenye kuzalisha.

Rev. Wilson Kimaro –  Calvary Temple – Arusha alipokuwa akihubiri katika Ibada ya Jumapili ya tarehe 1/1/2012 na kuukaribisha mwaka 2012.

Yesu anapatikana kwenye Neno lake!

Msiende kumtafuta Yesu mlimani na msituni, mahali sahihi pa kumpata Bwana Yesu ni kwenye Neno lake (Biblia) soma kuanzia Mwanzo hadi Ufunuo wa Yohana, kila kitu kuhusu wewe kimeandikwa humo, tafuta, tafakari na utafune! Yesu ni Yeye Yule, jana leo na hata Milele, ukimtafuta kwenye Neno lake anapatikana, kuna walioenda kumtafuta milimani wamerudi na imani nyingine.

Adam Haji

Tutolewe Leso – Yohana 11:43-44

Baada ya Lazaro kufufuliwa ilifanyika kazi ya ziada kuondoa sanda na leso yake. Sanda na Leso vilimfanya asiweze kutembea na kuona mbele. Tulikua wafu sababu ya dhambi, tukafufuliwa pamoja na Bwana Yesu, tukawa hai, kabla hatujaokoka tulikua kaburini. Warumi 6:4. Baada ya kufufuliwa (kuokoka) kazi ya Bwana Yesu inaendelea, tuziondoe sanda na leso zilizotufunga tufunguliwe.Tito 2:11-13

Mchg. Edward Mrope

Kubarikiwa ni mpaka uwe na Matunda

Unaweza kufunga na kuomba mara nyingi lakini usipate majibu au kufanikiwa, kwa sababu huna matunda. Neno la Mungu linasema katika Yohana 15:16, “Si ninyi mlionichagua mimi, bali mimi niliyewachagua ninyi, nami nikawaweka mkazae matunda, na matunda yenu yakapate kukaa; ili kwamba lolote mwombalo Baba kwa jina langu awapeni. Haya naawaamuru ninyi, mpate kupendana”

Baada ya kuchaguliwa na Mungu, anakuweka mahali, na sehemu aliyokuweka anataka umzalie matunda, na hayo matunda yapate kukaa, ili utakapoenda kuomba lolote, yeye aangalie matunda.

Matunda ni kufanya kitu kwa ajili ya Bwana, mipango mingi ya watu inakwama maana hauzai matunda tena yanayodumu.

Martin Mlata – Jesus Embasy, Songea

Tuzidi Kuwa Watakatifu!

Utakatifu ni hali ya kuwa safi kiroho na kimwili.Unapompokea Bwana Yesu unatengwa na dunia. Kutengwa huko kunakupa sifa ya wewe kuwa Mtakatifu, hivyo basi hupaswi kwenda sawasawa na dunia hii inavyoenda ama kama wengine ambao bado hawajatengwa. Inabidi maisha yako yabadilike na uwe mpya tofauti na awali ambapo hujamjua Kristo.

Huwezi Kuwa Mtakatifu kama haujaokoka maana Utakatifu huo hautokani na wewe bali Kristo aliyekuokoa na kukutenga na ndiye atakaye  kuwezesha kuishi katika Utakatifu.

Beatrice Eugine

Usitafute Upako, Tafuta Agano (NENO)

Watu wengi wanaenda na UPAKO, wenye akili wanaenda na AGANO, Mungu wetu sio Mungu wa UPAKO ni Mungu wa MAAGANO. Upako Huja hutoweka, Lakini Agano halitoweki linadumu milele. 

Wengi wanaotafuta Upako wanahangaika, wengine wanaenda Italia, wengine Israeli, Nigeria n.k yote hayo ni kupata UPAKO, Upako hupotea ndio maana pia inatokea kwa wahubiri wengi kuna kipindi kikifika wanahubiri Mafanikio, kipindi kingine wanahubiri Umoja, wengine Mwaka wa Toba Na vipindi hivi huja Hupotea! Kwa sasa wengi huubiri kuhusu habari za Siku Ya mwisho! 

Wawepo Wahubiri Wengi Nchini Sio Tatizo, Tatizo ni Ufahamu walinao Kuhusu Neno La Mungu (Agano) Sio Upako Maana wengine huutumuia Upako huu kwa kupata Mapato ya aibu!. 

Wewe Unayefanya biashara hauhitaji Upako, Unahitaji NENO LA MUNGU, Unayeumwa, Wenye Ndoa, Hamuhitaji Upako, Bali NENO. Sio Mtu unakuta ameokoka anahangaika kama mnganga wa kienyeji, akisikia upako wa kupata watoto anaenda, akisikia upako wa kupata pesa anaenda, akisikia mahali Fulani wanapaka mafuta anaenda. Haitakusaidia Kama Hauna Neno La Mungu Ndani Yako, Maana Biblia inasema “Neno la Kristo Likae Ndani Yenu” Utaielewa Kweli (NENO) Nayo Kweli Itakuweka Huru.

Ukiwa Huru Biashara Yako inafunguka, ndoa yako inakuwa na amani, kazi yako inakuwa huru kweli kweli, Maana Umelifahamu na Kulielewa.

Bishop. Dastun Maboya

Kuna nguvu kwenye mkono wako!

Kuna nguvu inayohama kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa kutumia mkono, naweza kuhamisha ugonjwa, woga, afya kupitia mkono. Magonjwa mengi tunayopata ni kupia mikono yetu wenyewe, sio kwa watu wengine, ukiwa ndani ya Kristo, uwezo wa kuponya, kubariki,kupokea mali, iko katiko mikono yako. Ninapomgusa mtu nguvu ya Mungu inatoka kama umeme kwenda kwake, nikimwambia pokea uzima uliomo ndani yangu yule mtu anapokea uzima!

Ndio maana ukiweka mkono juu ya mgonjwa anapokea uponyaji, ukiweka mkono au kumshika mwenye kansa, uzima unakuja ndani yake, mkono wangu ukimgusa mtu aliye na huzuni anapata furaha, Mungu amesema kitu kuhusu mkono wangu:  nikiweka mikono juu ya mgonjwa atapokea afya, sasa huo mkono sio wangu tena ni wa Bwana,tena sio mimi ninayeishi bali Kristo ndani yangu na uhai nilionao ninao katika Yesu Kristo! ndio maana nikiweka mkono juu ya mgonjwa anapokea! kwa vile umeokoka ule mkono sio wako tena ni wa Bwana, ukimgusa mgonjwa huyo anapona.

Angalia mikono yako, sema nayo, kwamba iko nguvu kwenye mikono yako, umo utajiri, kuna uzima kupitia mikono yako. Imo nguvu katika mikono yako, uwe mtu wa kufahamu kwenda sawasawa na Neno la Mungu, na nguvu ya Neno itatenda kwako!

Pastor Z.M Ryoba– Canaan Morogoro

Shetani haogopi TITLE yako!

Ni dhambi kuishi bila kujua KUSUDI lako! Kitu kinachomtisha shetani ni lile KUSUDI ulilonalo, haangalii jina lako au cheo chako. Anaangalia Je unafahamu kusudi lako hapa duniani? Wewe ni nani? Mungu amekuweka kwa makusudi gani? Ufanye nini? Ukitambua wewe ni nani hautabaki kama ulivyo, utakuwa tofauti na wasiojua KUSUDI lao!

Isack Malonga–TEHILLA NIGHT, 19 March 2010.

Mungu atakubarikije wakati unaendelea kuishi maisha ya dhambi?

Unaposema unapenda kubarikiwa, inabidi uwe mwenyenyekevu, uwe mwenye kutii, kuwaheshimu wengine pia uwe mwenye kuongozwa na Mungu. Watu wengi hawazioni baraka za Mungu katika maisha yao hata wakifunga na kuomba maana sio wanyenyekevu wanaenenda sawa na matendo yao ya zamani kabla hawajamjua Mungu, Mungu atakubarikije wakati bado unaendelea na kusengenya, kuzini, ulevi n.k.

Msidanganyike Mungu hakai katika dhambi! Tubuni na muache matendo yenu mabaya ndio mtaziona baraka za Mungu kwenu! 1 Petro 3:8

Pastor Obadia, BURUNDI

Ibada ya sanamu!

1. Kuabudu sanamu sio mpaka uchonge mti au mapambo, kuabudu sanamu ni kupenda kitu chochote kuliko Mungu, sanamu inaweza kuwa kazi yako, mke/mume wako, biashara yako n.k.

2. Unapoenda mbele za Mungu usitaje manabii waliopita wakuombee au mtakatifu yeyote, wao walikua binadamu kama wewe, uombapo Omba kwa jina la YEsu, unapotegemea kitu au mtu ili akuombee ni Ibada ya sanamu.

3. Tunao uwezo wa kuomba kwa ujasiri kwa kupitia jina la Yesu  pasipo kuwataja manabii au mitume waliopita, kama Maria mama wa Mungu, Mtakatifu Yoseph, Mtakatifu Magdalena, Cecilia, Petro, Theresea n.k

Jimmy, Mlima wa Mabadiliko— TABATA

Tatizo ni wewe, sio kanisa unapoabudu!

Watu wengi wanadhani ukubwa wa jengo la kanisa au wingi wa watu wengi kanisani inamaanisha Mungu yupo mahali pale, Mungu yupo hata katika kundi dogo, Biblia inasema katika Mathayo 18:20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.

Isifike hatua watu wakaabudu wanadamu, Mungu hawezi kuacha kuonekana katika kanisa la mahali pamoja hata kama watu ni wachache mno, kama wamekusanyika kwa ajili yake, Atakuwepo!

Yawezekana kuna tabia ambazo huwezi kuzidhibiti, Mungu anataka akufungue, lakini anataka ujikane, ukubali kubadilika na kuachana na tabia zako, Hata uzunguke makanisa mangapi ikiwa hujakubali hautapa unachokitafuta, Tatizo ni wewe!

Pastor Emmanuel, DODOMA

Unapobarikiwa Usimsahau Mungu!

Mungu anapokubariki usijiinue na kuwa na kiburi kwa mali ambazo Mungu amekupa, watumishi wengi wa Mungu wanaanza vyema wakimtafuta Mungu ili awainue katika huduma zao, biashara na mambo yao ya mafanikio. Wakifanikiwa hudhani ni kwa nguvu zao wenyewe.

Unapofanikiwa usione kwamba wengine hawafai mbele zako, Mwambie Mungu akusaidie, anapokubairki usimuache!

Mama James Odera– Nyakato, Musoma

Tunapaswa kuwapelekea watu habari njema

Watu wengi hudhani wanaenda kanisani kama vile ni lazima waende kanisani jumapili. Pengine nawe pia hudhani hivyo . Lakini nje ya kanisa kuna watu wanaohitaji msaada wako. Kuna watu ambao Mungu  amewaandaa ili wewe uwahudumie, sio mchungaji wa kanisa lako au mishionari tu ndiye mwenye jukumu la kuhubiria watu, hata wewe pia ni jukumu lako!

Kuna watu wengine walio nje ya kanisa hawajasikia habari njema za Bwana Yesu, pengine ni ndugu zako unaoishi nao, rafiki zako wa karibu hata jirani zako. Tuwapelekee watu habari njema za Bwana Yesu, tushuhudie matendo Makuu ambayo  amefanya katika maisha yetu.

–Ev. John, Gilgal Mwanza–

Fursa haiji mara mbili, nafasi huja mara nyingi!

pastor Kaleb

“Mungu anakupa fursa  ya kutoka kwenye nafasi moja kwenda katika nafasi nyingine, anakuweka katika nafasi ili uiendee fursa ambayo amekupa, kila pingamizi unalopitia katika maisha yako,  ndani ya mapingamizi hayo kuna mbegu za kuiendea fursa yako.

Tatizo sio tatizo, tatizo ni nini kilicho ndani ya tatizo lako. Mungu hutoa fursa mara moja tu lakini nafasi huja zaidi ya mara mbili ili kuinua kiwango chako”.

Pastor Justine Kaleb

Kupanda na Kuvuna katika maana ya Rohoni Wagalatia 6:7-10, Mithali 19:29

Aina za mbegu na namna ya kupanda katika roho

a)      Mawazo

Jinsi mtu awazavyo (unapowaza unapanda) ndivyo alivyo (avunavyo) Mtu anapowaza, anapanda na kama asipoyabadili anayoyawaza (asipong’oa mbegu/mche huo) atavuna

Kama vile Mungu alivyopanda bustani ya Edeni, ametupandia akili njema (sound mind) ili tuwaze vema na kutoa mavuno sahihi, Mungu aweza kutupa (mavuno) zaidi ya (mbegu tupandazo) tuwazavyo na tuombayo. Waefeso 3:20 “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu”

b)      Kumcha Mungu ni pando ambalo mavuno yake ni tunda la roho Galatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria“. Pamoja  na yaliyoelezwa katika agano la Mungu na wanadamu. Yona 12:26 “Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu“.

Tupande mambo muhimu matatu WAKATI WOTE (interchangeably)

a)      Kufanya bidii katika kujilisha Neno la Mungu

b)      Kufanya bidii katika aina zote za maombi

c)       Kufanya bidii katika kumsifu na kumwabudu Mungu katika roho na kweli

Kufanya bidii katika hayo yote matatu ni kufanyaje?

Haya yafanywe wakati wote, kwanza wakati tukiendelea na shughuli zetu za kila siku, pia kuwepo na nyakati za kujitenga na shughuli nyingine ili kufanya hayo matatu au moja au mawili kati ya hayo pekee. Ili kufanya wakati wote.

-E.Kiwia-

Ujasiri wako u wapi ndugu yangu? (Yeremia 18:1-4)

kissa

Ujasiri wako u wapi ndugu yangu? Ujasiri wako wa mwanzo tangu umemjua Bwana Yesu je uko vilevile? Je ndoa Mungu iko kama Mungu alivyokusudia? Nawe Kijana ulianza moto mbona hueleweki siku hizi? Tunda la Roho liko ndani yako ndugu yangu?

Kuna adui anaharibu kila mpango wa Mungu katika maisha yetu na kuweka atakavyo yeye, sasa gundua urudi kwa mfinyanzi aliyekufinyanga, Mungu wako akufinyange upya aondoe kiburi chako, aondoe kila pando ambalo hakuliweka yeye. Usiwe vuguvugu ndugu yangu, adui yupo na anakuwinda wakati wote ili uangamie. Kubali Bwana Yesu akufinyange upya

Kissa Mboma