
Wapendwa napenda tena kuwaita toka ndani ya moyo wangu, mje msimame na taifa la Israeli wakati huu, nina mengi sana ya kusema juu ya taifa la Israeli, watu wake, na jiji la Jerusalem, Si kwamba nimepewa mzigo tu wa kusimama kwa ajili ya taifa la Israeli, lakini nina connection na bond isiyovunjika na taifa la Israeli, kwangu Israeli ni taifa rafiki, pia ni taifa ndugu kwangu, nimeunganishwa na hili taifa, liko ndani ya moyo wangu, upendo nilionao kwa ajili ya hili taifa ni upendo usioelezeka, nimelikumbatia hili taifa, hata kama adui anataka kurusha mishale juu ya Israeli na wayahudi, inipate mimi kwanza, lakini isiifikie taifa la Israeli wala watu wake ambao Mungu amenipa na nina wapenda sana.
I do real have a special connection with Israel, Israeli inapoingia kwenye shida, na mimi huwa ninapata mahangaiko sana ndani yangu, ni kama vile ndugu zangu wako kwenye shida, huwa kuna wakati namuuliza Mungu ni kitu gani hiki?
kwa watu wanaofahamu wanajua Israeli ipo karibu sana kuingia katika vita, iko kwenye hali ya kivita.
Mpango wa Palestina wa kudai taifa huru la palestina katika mipaka kabla ya vita ile ya mwaka 1967 Israel iliposhinda na kuliunganisha tena jiji la Jerusalem ni mpango hatari sana kwa uhai wa taifa la Israeli,
katika Muda wa siku chache zijazo, macho ya ulimwengu wote yataelekea mashariki ya kati, kuna mambo ambayo kwa kweli ukiyaangalia kwa macho ya Rohoni, yanasukuma kutimilika kwa nabii muhimu sana katika Biblia, wale student of Bible prophecy na wale wanaofuatilia habari ya Taifa la Israeli kwa karibu wanajua kitu ninachosema.
Vile vile natoa wito kwa serikali au taifa la Tanzania, Rais, na wizara ya mambo ya nje, na washauri wake wa mambo ya nje, taifa la Tanzania lisiingie katika muunganiko wa mataifa ambayo yatapiga kura kulitambua taifa la Palestine katika mipaka kabla ya vita ile ya mwaka 1967. Taifa la Tanzania lisipigie kura wala kushiriki kui endorse makubaliono yoyote ambayo yanalitambua taifa la palestine na kuugawa mji wa Jerusalem na nchi ya Israeli.
Taifa la Tanzania kama mwanachama huru wa Umoja wa Mataifa, huwa linapiga kura pamoja na mataifa mengine ambayo yako katika baraza kuu la umoja wa matiafa na pia ni wanachama wa umoja wa mataifa.
Maandiko ninayosoma yananiambia hasira kali ya Mungu ipo kwa ajili ya mataifa ambayo yamekusanyika au yanakusanyika kwa ajili ya kuukandamiza na kuionea sayuni, kuionea Jerusalem, na taifa la Israeli.
Kwa watu wanaotaka kuungana nami kwa maombi, hebu kwa walau masaa machache au dakika chache tu, soma Isaya 62:1-7 pata muda wa kumwambia Mungu kitu juu ya Israeli. Mimi sitaki kuona Israeli inaingia katika matatizo, kwahiyo nina jukumu la Kuomba sana kwa ajili yake, na kulitia moyo taifa la Israeli, lisifadhaike, wala kupoteza tumaini, eh Israeli, sema unazo nguvu, kwa maana Mungu wako yupo karibu sana nawe apate kukutetea na kukupigania, yeye aliye mlinzi wako hatalala wala kusinzia.
Inuka eh Bwana uitetee Israeli mataifa yaliyo ulimwenguni na watu wa kabila zote, dini zote, na watu wote wapate kuona ya kwamba wewe hujaiacha sayuni bali upo karibu sana na sayuni, eh, Mungu wangu majira na Nyakati za wewe kuonekana sayuni zimetimia, inuka eh Bwana mataifa waone ya kwamba wewe Ndiye Mungu wa Israeli. Na Israeli ni mtumishi wako.
–Lwitiko Katule