Maigizo ya Kikristo

zecomedy

Wasanii ambao hawajaokoka wamekuwa wakiigiza maigizo ya Kikristo na wengine wanaigiza hadi mambo ya ndani kabisa kama vile kuongoza watu sala ya toba, kunena kwa lugha na kukemea mapepo!

komed

Je, wasanii ambao hawajaokoka kuigiza mambo ya Ukristo kuna athari chanya au hasi kwa Ukristo?

ze-comedy

Kundi maarufu la Orijinol Komedi walialikwa na kuigiza kwenye tamasha la uzinduzi wa albam ya nyimbo za injili na kwaya ya Haleluya ya kanisa la EAGT Morogoro katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro hivi karibuni.

Flora Mbasha kwenye tamasha la Mseto wa WAHAPAHAPA

mbasha

Muimbaji wa Injili Tanzania mwenye album za JIPE MOYO, UNIFICHE,  FURAHA YAKO kwa sasa anasikika na wimbo wa WANAWAKE wenye mahadhi ya mchiriku. Atatumbuiza kwenye tamasha la uzinduzi wa album ya MSETO WA WAHAPAHAPA litakalofanyika 7 June 2009 viwanja vya Coco Beach, mbali na yeye kushiriki Tamasha hilo, waimbaji wa muziki mchanganyiko kama Mzee Yusuph (Muimbaji wa Taarabu) Banana Zoro, Enika (Muziki wa kizazi kipya) Calora Kinasha na Wahapahapa Band wataimba.

Pia WAHAPAHAPA ni tamthilia ya mchezo unaosikiwa kila jumatatu kwenye Radio Free Africa (RFA) na Radio One, lengo lao ni kuangalia athari za VVU/UKIMWI kwa vijana. Mbasha ni muimbaji pekee wa Muziki wa Injili atakayetumbuiza.

Uzinduzi wa Christina Shusho na mavazi yake!

upendokwegir

Christina Shusho akiwa na Mbunge wa kuteuliwa Mh. Alishamaa Kwegir

Tarehe 30 November 2008  Christina Shusho alizindua album yake ya UNIKUMBUKE walikuwepo waimbaji mbalimbali walioalikwa kuimba. Katika tukio la tofauti siku ile alionesha mavazi aliyoyabuni mwenyewe, anasema mavazi hayo ni kwa ajili ya wakristo.

 

PICHA ZA TUKIO HILI KWA HISANI YA ANDREW NGAI

Kaka aanza maandalizi ya kumtumikia Mungu!

kaka1

Mchezaji maarufu wa Brazil Kaka ametangaza Jumapili nia yake ya kurudi kuchezea team yake ya nyumbani Sao Paulo. Mchezaji huyo anategemea kustaafu soka baada ya hapo kabla hajarudi kwenye kanisa la Christ Evangelical Church na kuwa mchungaji.

“Mchezaji anapokaribia kumaliza kazi yake, inabidi afikirie nini afanya katika maisha yake ya baadae” alisema Kaka

“Life changes dramatically. When you are 20 years old, you think about one thing. When you are 30, you change your mind. For this reason, it is important for me to begin to think about what I want to do with the rest of my life. I am going to begin my preparations to one day become a priest,” said the star of the Brazilian national soccer team.

Kaka ni mfuasi wa kanisa la wokovu la Christ Evangelical church.

-chinaview-

Faustine Baha ashinda mbio za marathon!

Faustine Baha ameshinda mbio za marathon tarehe 19-10-2008 Ujerumani. “Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuwa mshindi wa kwanza kwa kukimbia 2:13:03 km 42 kati ya watu 160,000. kwakweli nilimtanguliza Mungu kabla ya mbio namshukuru ameniwezesha kuwa mshindi”

Kwa wasiomfahamu Faustine aliwahi kupata pesa nyingi kwa njia za giza hapo kabla hajamjua Yesu, alizunguka kwa waganga kutafuta utajiri na anawafahamu waganga wengi hapa Tanzania. Lakini sasa yeye ni mtumishi wa Mungu, ni mwanariadha na ni mwenyeji wa Arusha.

Angela awa balozi wa Redds!

Mtoto wa Askofu Deo Lubala amechaguliwa kuwa Balozi wa bia aina ya redd’s katika viwanja vya Leaders Club, Agosti 2, 2008. Angela mwenye maono ya kumtangaza Yesu kwa kupitia mashindano ya urembo amekua gumzo kwa baadhi ya wapendwa kutokana na waandaaji wa mashindano hayo na imani yake ya wokovu.

Faustine Baha, Mlokole anayeiwakilisha Tanzania

Ni jambo la kumshukuru Mungu kuona vijana waliookoka kufanya vyema katika fani mbalimbali hii huonesha wazi Mungu wanayemtumaini ndiye anayewawezesha. Faustine Baha mwanariadha mtanzania mwenyeji wa Arusha ameshindana nchini ujerumani hivi karibuni katika riadha ya kimataifa amekua mshindi wa pili kati ya wanariadha 12,500. Utukufu na Sifa ni kwa Bwana wa Majeshi.

KAKA – Mcheza soka anayependa kuwa Mchungaji


Wapenzi wa mpira wa miguu bila shaka KAKA sio jina geni kwao. KAKA ni kijana ambaye ameokoka na siku zote katika mechi anazocheza na kushinda anamtukuza Mungu na anapenda kusema mara nyingi “I don’t win alone, I want to thank God for all the victories and achievements I had this year as a player.”

Mtumishi wa Mungu KAKA ambaye ni balozi wa Yesu katika soka la kimataifa alisema pia katika vyombo vya habari “I bring here two awards – one is my son, who is coming soon. The other is this FIFA trophy. I want to give it to God and place it in this church, in Lord’s house, so that everyone can see it,”

Kaka hupenda kuongelea imani yake ya Yesu Kristo hadharani na kuzungumzia upendo wa Mungu, anapofunga goli huinua mikono yake juu na kumshukuru Mungu, katika moja ya mechi ya World Cup aliposhinda alionesha T-shirt iliyoandikwa “I belong to Christ” baadae alilimpa rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva.

Ni kijana mwenye miaka 26 anayempenda Yesu na anasema anapenda kuwa mchungaji akiacha kucheza mpira.

……hatimaye atwaa taji la miss Temeke

Mtoto wa Askofu Mkuu wa kanisa la kipentekoste la Word Alive Mchungaji Deo Lubala, Bi. Angela Deo Lubala amefanikiwa kuwa mshindi wa miss Temeke kwa kuwashinda wenzake 11, hapo awali alikuwa mshindi wa miss Changómbe kwa kuwashinda wengine 9, Angel mwenye maono ya kuufikia ulimwengu kwa kulitangaza jina la Yesu anatarajiwa kushiriki mashindano ya miss Tanzania hivi karibuni.