Category Archives: NUKUU
“Shetani ameshakufa, tangu tarehe 4/11/2008″ – Nabii Elia
Ni ajabu na kweli kusikia maneno hayo toka kinywani mwa mzee wangu wa kanisa wa siku nyingi aliyenilea nilipookoka miaka ya 80′s. Leo niliamua kuamka asubuhi na mapema nikaenda kwenye morning glory ya kanisa mojawapo kati ya makanisa jirani. Maombi yalikua mazuri na kwa bahati ndipo nikakutana na mzee wangu huyo wa kanisa. Naye amekua muumini wa kanisa hilo.
Akaanza kunishuhudia ndipo nikaanza nami kujifunza mambo mapya ya upande mwingine wa imani ya kikristo. Kwanza mzee alikua na jina lake la ukoo tulilomtambua kwalo, ameliacha na kupewa jina lingine. Kitabu chake cha neno la Mungu kina gamba la juu jipya na hakiitwi “Biblia” akitaka kuomba anatumia majira, siku na nyakati ili kufanikiwa. Lililoniacha mdomo wazi ni pale aliponiambia kuwa “Shetani ameshakufa, tangu tarehe 4/11/2008 na ameuawa na nabii wetu mkuu. Hata wapunga pepo wanajua hilo, ukiwauliza wanasema ameuawa na nabii Elia…” Nikajiuliza kama wapunga pepo wanajua hilo, wewe Mtakatifu unajua shetani ni marehemu? Kazi kwako!
–EK–
Wachungaji Msitangazie washirika dhambi ya mtu mwingine!
“Mchungaji unapotangaza dhambi/makosa ya mtu kwa washirika/waumini kinachotokea ni kwamba yule mtu hata kama ameshatubu kwa Mungu wale washirika watabakia wakimhukumu “fulani alitenda dhambi hii”. Kwa kufanya hivyo watu hao wanabakia na dhambi hiyo hadi siku yao ya kufa. Maana mtu akitubu Mungu humsamehe lakini watu ni vigumu sana kusahau.
Na wewe mtu uliyeokoka, mtu akitenda dhambi achana naye, usiweke dhambi yake moyoni mwako bali songa mbele katika kumwangalia Yesu”
Mwinjilisti Obadia alipokuwa akihubiri katika mkutano wa Injili mjini Arusha tarehe 22, June, 2011.

