“Kwasababu ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako yakuwa Mungu alimfufua katika wafu, UTAOKOKA. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa mtu hukiri hata KUPATA WOKOVU”. (Rum 10:9-10.)
Baada ya kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako, ni muhimu sana kupata mafundisho ya awali, yatakayokusaidia kujua kwa hakika, maana ya KUOKOKA au WOKOVU; “ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.” (Efe 4:14)
Ndio maana Yesu alisema, tukishawahubiri na kuwasaidia kuokoka, tuwafundishe yote!“Yesu akaja kwao akasema nao, akawaambia, nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na mkiwafundisha kuyashika yale yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote hadi ukamilifu wa dahari”. (Math 28:18-20).
“Basi kama mlivyompokea Kristo Yesu, Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye; wenye shina na wenye kujengwa katika yeye; mmefanywa imara katika imani, kama mlivyofundishwa; mkizidi kutoa shukrani”. (Kol 2:6-7)
“Wakawa wakidumu katika fundisho la Mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali” (Mdo 2:42)
“Muwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu, lakini kwa upole na kwa hofu” (1Pet 3:15)
Watu wengi wamechanganya sana maana halisi ya neno “kuokoka”. Unaweza kupewa tafsiri nyingi na watu, juu ya neno “kuokoka”. Wengine hudhani kuokoka ni dini au dhehebu Fulani la “walokole”. Wengi hudhani wokovu ni maisha Fulani ya kujinyima raha na kujitenga na jamii. Wengi hudhani wokovu ni maisha duni nay a umasikini au kutokuwa na mali za kifahari. Ndani ya fikra za watu, kuna tafsiri nyingi tofauti juu ya “kuokoka” na hizo tafsiri nyingi si sahihi. Lakini hii hapa chini nadhani ndio tafsiri rahisi zaidi kueleweka.
NINI MAANA YA KUOKOKA?
KUOKOKA ni lugha ya kawaida kabisa, yenye maana ya;
Kunusurika, kusalimika, kupona, kukombolewa, kufunguliwa au kutoka katika janga au hatari fulani.
Mfano:-
- Kunusurika; Paulo aliposafiri mashuani pamoja na watu wengine mia mbili na sabini na sita, alisema;“safari hii itakuwa na madhara na hasara nyingi, si ya shehena na merikebu tu, ila na ya maisha yetu pia … baada ya muda mchache, ukavuma upepo wa nguvu wa namna ya tufani … na kwa maana tulikuwa tukipigwa sana na ile tufani, siku ya pili yake, wakaanza kuitupa shehena baharini. Siku ya tatu wakatupa vyombo vya merikebu kwa mikono yao wenyewe. Jua wala nyota havikuonekana kwa siku nyingi, na tufani kuu ikatushika, basi tukakata tamaa ya kuokoka … na baharia walipotaka kukimbia na kuiacha merikebu … Paulo akawaambia akida na askari, hawa wasipokaa ndani ya merikebu, hamtaweza kuokoka … Shauri la askari lilikuwa kuwauwa wafungwa, mtu asiogelee na kukimbia. Bali akida akitaka kumponya Paulo, akawazuia wasifanye kama walivyokusudia, akawaamuru wale wawezao kuogelea, wajitupe kwanza baharini, wafike nchi kavu … na hivyo watu wote wakapata kuifikilia nchi kavu salama. Tulipokwisha kuokoka, ndipo tulipojua ya kuwa kisiwa kile chaitwa Melita”. (Mdo 27: 1-44. 28:1)
H Hivyo tunaona “KUOKOKA” katika mistari hii, imetumika kama “KUNUSURIKA”.
- Kupona; Wayahudi walimdhihaki Yesu , “Jiponye nafsi yako, ushuke msalabani.
( Mk 15:30)
Sisi je, tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kasha ukadhibitishwa kwetu na wale waliosikia. (Ebr 2:3)
“KUOKOKA” katika mistari hii imetumika kama “KUPONA”.
“Na niseme nini tena? Maana wakati usingetosha kuleta habari za Gideoni, na Baraka, na Samsoni, na Yefta, na Daudi, na Samweli, na za Manabii; Ambao kwa imani, walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga.
- KUOKOKA katika mistari hii, imetumika kama KUPONA, KUSALIMIKA AU KUNUSURIKA!
- Kusalimika; Wakati Mungu anaangamiza dunia kwa maji ya gharika, Biblia inasema;
“Wala hakuuachilia ulimwengu wa kale, bali alimhifadhi Nuhu mjumbe wa haki na watu
wengine saba, hapo alipoleta gharika juu ya ulimwengu wa wasio mcha Mungu. Tena
akaihikumu miji ya sodoma na Ghomora, akiipindua na kuifanya majivu, akaifanya
akaifanya iwe ishara, kwa watu watakaokuwa hawamchi Mungu baada ya hayo.
Akamwokoa Lutu, yule mwenye haki, aliyehuzunishwa sana na mwenendo wa ufisadi
wa hao wahalifu. (2Pet 2:5-7)
“Hapa KUOKOKA” imetumika kama “KUSALIMIKA” kutoka katika janga la gharika na moto.
- Kufunguliwa au Kukombolewa; Herode alipomtia Petro gerezani ili amuuwe, Biblia inasema;
“Panapo majira yale yale, herode mfalme akanyoosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa. Akamuuwa Yakobo ndugu yake Yohana kwa upanga. Na akiona yakuwa imewapendeza Wayahudi, akaendelea, akamshika na Petro … akamweka gerezani, akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka, kumtoa na kumweka mbele ya watu. Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa lilikuwa likimwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake. Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule, Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, alikuwa amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakailinda gereza. Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi! Minyororo yake ikamwanguka mikononi. Malaika akamwambia, jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, jivike nguo yako, ukanifuate. Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua yakuwa ni kweli, yaliyofanywa na malaika. Bali alidhani kwamba anaona maono. Na walipopita lindo la kwanza na la pili, wakaja hata mlango wa chuma wa kuingilia mjini, ukawafungukia wenyewe. Wakatoka nje, wakapita katika njia moja; mara malaika akamwacha. Hata Petro alipopata fahamu akasema, “sasa nimejua yakini yakuwa, Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi”. Na alipokuwa akifikiri hayo, akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana Marko … na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba. Naye alipobisha, kijakazi jina laki Rhoda akaja kusikiliza. Alipoitambua sauti ya Petro, hakufungua mlango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani, akawaambia kwamba, Petro anasimama mbele ya lango. (Mdo 12:1-14-19)
“KUOKOKA” katika mistari hii, imetumika kama “KUFUNGULIWA” au “KUKOMBOLEWA” katika kifungo.
UHAKIKA WA WOKOVU
Kwahiyo KUOKOKA ni KUNUSURIKA, KUSALIMIKA, KUKOMBOLEWA, KUFUNGULIWA au KUPONA kutoka katika JANGA au HATARI fulani.
Yesu alikuja kuleta wokovu (kuokoa) na Biblia inataja mistari mingi sana juu ya koukoka au wokovu.
Kwa mfano:-
- Yoh 3:16-18; Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanae wa pekee ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyehamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la mwanawe wa pekee.
- Luk 9:59; Kwa maana mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa,
- Yoh 12:47; Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi si mhukumu, maana sikuja niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu.
- 1Tim 1:15; Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa ya kwamba, Kristo Yesu alikuja ulimwenguni awaokoe wenye dhambi; ambao wa kwanza wao ni mimi.
- 1Tim 2:14; Mungu … hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yalio kweli.
- Efe 2:5,8; Hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo, yaani, mmeokolewa kwa Neema, Kwa maana mmeokolewa kwa Neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;
- 1Kor 1:18; Kwa sababu neno la Msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi, bali kwetu tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
- Mdo 4:10-12; Jueni nyote na watu wote wa Israel ya kuwa, kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulubisha, na Mungu akamfufua katika wafu … kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. Yeye ndiye jiwe lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limekuwa jiwe kuu la pembeni. Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina lingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.
Mdo 2:22-24, 36-40, 43-44, 47; Enyi waume wa Israel, sikilizeni maneno haya: Yesu wanazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua; Mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulubisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua; ambaye Mungu alimfufua, akifunga uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao…
Basi nyumba yote ya Israel nawajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulubisha kuwa Bwana na Kristo. Walipoyasikia hayo wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? Petro akamwambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa watu wote watakao itwa na Bwana Mungu wetu wamjie. Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi …
Kila mtu akaingiwa na hofu; ajabu nyingi na ishara zikafanywa na mitume. Na wote walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika … Wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.
(Mdo 2:22-24, 36-40, 43-44, 47)
Rum 10:9-10; Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, nakuamini mioyoni mwako yakuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
Mdo 16:30-31; Kisha akawaleta nje akasema. Bwana zangu, Yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, mwamini Bwana Yesu nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.
2Kor 6:2; Kwa maana asema, wakati uliokubalika nalikusukia, siku ya wokovu nalikusaidia; Tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; Tazama, siku ya wokovu ndio sasa.
Ebr 2:1-3; Kwa hiyo, imetupasa kuangalia zaidi hayo yaliyosikiwa, tusije tukayakosa, kwa maana, ikiwa lile neno lililonenwa na malaika, lilikuwa imara, na kila kosa na uasi, ulipata ujira wa haki. Sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukadhibitika kwetu na wale wanaosikia.
TUMEOKOLEWA KUTOKA KWENYE NINI?
1. TUMEOKOLEWA KUTOKA KATIKA NGUVU YA DHAMBI / UASI
Maana sijui nifanyalo; kwasababu lile nilipendalo silitemdi; Bali lile nilichukialo ndilo nilitendalo … naikiri kuwa ile sheria ni njema. Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. Kwa maana najua kuwa, ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema, kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati … lakini katika viungo vyangu, naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi iliyo katika viungo vyangu. Ole wangu, masikini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti? NAMSHUKURU MUNGU, KWA YESU KRISTO BWANA WETU. (Rum 7:15-15)
“Nanyi mlikuwa wafu kwasababu ya makosa na dhambi zenu. Ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuaata Mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi; ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tama za miili yetu, tulipo yatimiza matendo ya mwili na nia, kukawa kwa tabia yetu watoto wahasira kama na hao wengine. Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; hata wakati ule tulipokuwa wafu kwasababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, mmeokolewa kwa neema akatufufua pamoja naye akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu.”(Efe 2:1-1-2-6)
“Sasa basi hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti”. (Rum 8:1-2) … “tukijua neno hili, ya kuwa, utu wetu wa kale ulisulubishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike. Tusitumikie dhambi tena … Basi dhambi isitawale ndani ya miili yenu … kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi. Lakini Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mli-itii kwa mioyo yenu, ile namna ya elimu (Injili ya wokovu), ambayo mliwekwa chini yake. Na mlipokwisha kuwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki … kwa maana mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki. Ni faida gani mliyopata siku zile kwa mambo hayo mnayo yatahayarikia sasa? Kwa maana mwisho wa mambo hayo ni mauti. Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima. … Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa. (Ezek 28:20-23) … kwa maana mshahara wa dhambi nimauti wa milele, bali karama (zawadi) ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (Rum 6:23)
Pia soma; Tito 2:11-12; Tito3:3-4; 2Kor 4:3-4; Efe 4:18-19; 1Tim 1:13-15
TUMEOLOKEWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA GIZA.
“Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana wa pendo lake”. (Kol 1:13)
“Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, mliwafanya hai pamoja naye, akisha kutusamehe makosa yote; akisha kuifuata ile hati iliyoandikwa kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi za mamlaka, na kuzifanya kwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo”. (Kol 2:13-15)
Tazama, nimwewapa amri ya kukanyaga nge na nyoka na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. (Luk 10:19)
Pia soma; Math 27:45,50-54; Ebr 2:14-15; Luk 11:21-22; Yoh 19:28-30
3. TUMEOKOLEWA KUTOKA KATIKA LAANA YA TORATI.
“Fahamuni basi, yakuwa wale walio na imani, hao ndio wana wa Ibrahim. Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahim habari njema zamani, kusema, katika wewe mataifa watabarikiwa. Basi hao walio na imani hubarikiwa pamoja na Ibrahim aliyekuwa mwenye imani. Kwa maana wale wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana maana imeandikwa amelaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Torati, ayafanye. Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu mwenye haki ataishi kwa imani. Na torati haikuja kwa imani, bali ,ayatendaye hayo, ataishi katika hayo. Kristo alitukomboa katika laana ya Torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa , amelaaniwa kila mtu aangikwae juu ya msalaba; ili kwamba baraka ya Ibrahim iwafikirie mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya roho kwa njia ya imani”. (Gal 3:7-14, 23-29).
“Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. (Rum 10:4)
Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”. (Ebr 8:13)
Basi twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria …
Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au Sabato; ( Rum 3:28; Kol 2:16)
Pia Mdo 15:1-10-29; Gal 2:16; Rum 8:3; Rum 7:12,14-16; Rum 8:1-4; Yer 31:31-34
4. TUMEOKOLEWA KUTOKA KATIKA DUNIA (UOVU WA DUNIA).
“Neema na iwe kwenu, naamani, zitokazo kwa Mungu Baba, na Bwana wetu Yesu Kristo; ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili ya dhambi zetu, ili atuokoe na dunia hii mbovu, iliyopo sasa. Gal 1:3-4
“Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmoja wapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie. Na sasa naja kwako; ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao. Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umechukia; kwa kuwa wao si waulimwengu, kama mimi nisivyo na ulimwengu. Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; basi uwalinde na yule muovu. Wao sio wa ulimwengu, kama mimi nisivyo waulimwengu. Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndio kweli kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami hivyohivyo naliwatuma hao ulimwenguni. Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe katika kweli”. Yoh 17:11-19 (14-16)
Pia Yoh 8:21-24 (23); 1Kor 5:9-11; Rum 12:1-2
5. TUMEOKOLEWA KUTOKA KATIKA JEHANUM YA MOTO.
“Kwahiyo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji ikaangamia, lakini mbingu za sasa na nchi, zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na kuangamia kwao wanadamu wasio mcha Mungu. Lakini wapenzi, msilisahau neno hili … Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyodhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu yeyote apotee, bali wote wafikie toba. Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi; katika siku hiyo, mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.. Basi kwakuwa vitu hivi vyota vitafumuliwa, hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani? Katika mwenendo mtakatifu na utauwa! Mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo, mbingu zitafumuliwa na zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka. Lakini kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake”. 2 Pet 3:6-13
“Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, nayeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake;
Na mauti na kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadri ya matendo yake mauti za kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndio mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. Naiwapo mtu yeyote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima alitupwa katika lile ziwa la moto.” Ufu 20:11-15 “Amini, amini nawaambia, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna na uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mauti kuingia uzimani”. (Yoh 5:24) Pia Lu 10:20; Fil 4:3; 1Yoh 3:14; Rum 5:6-9;
6. TUMEOKOLEWA KUTOKA KATIKA MAGONJWA.
Nanyi mtamtumikia Bwana Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako na maji yako. Nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. (Kut 23:25) … Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote, wala hatatia juu yako maradhi yeyote, mabaya uyajuayo …” (Kumb 7:15)
Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo, akawatoa pepo kwa jina lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi (wagonjwa). Ili litimie lile neno lililonenwa na Nabii Isaya akisema; “Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu na kuyachukuwa magonjwa yetu.” (Math 8:16-17) “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote, na udhaifu wa kila aina”. (Math 9:35) “ … Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu; wawatoe na kupoza, magonjwa yote na udhaifu wa kila aina (Math 10:1)
Yeye mwenyewe alizichukuwa dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; Na kwa kupigwa kwake mliponywa (1Pet 2:24) “Hakika ameyachukuwa masikitiko yetu, amejitwika huzuni zetu …. Bali alijeruliwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu. Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake; Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. (Isa 53:4 -5)
Damu ya Msalaba iliyoondoa dhambi, ndiyo iliyoondoa magonywa pia. Yatupasa kuyaona magonjwa kama tunavyoiona dhambi. Hatupaswi kuyaona kuwa ni sehemu ya maisha yetu. Magonjwa ni matokeo ya anguko la mwanadamu katika dhambi. Tukiisha okolewa toka dhambini, yatupasa kuokolewa kutoka katika magonjwa pia. Afya njema ni matunda ya msalaba kama ilivyo wokovu.
Tunatakiwa kuchukia magonjwa kama tunavyochukia dhambi, kwasababu yote haya, ni kazi za shetani. Yatupasa kuzikataa na kuzivunja katika maisha yetu. Kifo cha Yesu, kitakuwa hakina maana kamili, kama tutaokolewa katika dhambi, halafu tubaki katika magonjwa pia, wakati Yesu aliyefia dhambi, ndiye aliyefia magonjwa pia. Msalaba ulifanya vyote, uliondoa dhambi na magonjwa pia. “Mwenyewe aliutwa udhaifu wetu na kuyachukuwa magonjwa yetu.” (Math 8:16-17)
7. TUMEOKOLEWA KUTOKA KATIKA UMASKINI
Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake. Na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka. Na kila kitu ulichonacho kitakapoongezeka; Basi hapo moyo wako usiinuke ukamsahau Bwana Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa … hapo usiseme moyoni mwako, nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu, ndio ulionipatia utajiri huo; Bali utamkumbuka Bwana Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri, ili alifanye imara agano lake … (Kumb 8:12-18) Lakini hawatakuwepo masikini kwenu, kwakuwa Bwana atakubariki kweli, katika nchi akupayo Bwana Mungu wako, uimiliki, iwe urithi wako. (Kumb 15:4)
Naye Abrahamu alikuwa tajiri sana kwa mifugo, kwa fedha na kwa dhahabu (Mwa 13:2)
Maana mmejua Neema ya Bwana wetu, Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa masikini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajri. Ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake. (2Kor 8:9) … mkitajirishwa katika vitu vyote, mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. (2Kor 9:11) … Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu. (Fil 4:19) … Maana yeye yule ni Bwana wa yote, mwenye utajiri kwa wote wamuitao; kwa kuwa, kila atakayeliitia jina la Bwana ataokoka. (Rum 10:12)
Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi, mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la. Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi. Na mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema Bwana wa majeshi. (Malaki 3:10 – 12)
Thawabu ya unyenyekevu, ambao ni kumcha Bwana, ni utajiri na heshima, nayo ni uzima.
(Mith 22:4)
Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya dunia; na baraka hizo zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani, utabarikiwa na uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo. Maongeo ya Ngombe wako, na wadogo wa kondoo zako: utabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga. Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako watakutokea kwa njia moja; lakini watakimbia mbele kwa njia saba. Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubariki katika nchi akupayo Bwana wako Mungu wako.
Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakapoishika maagizo ya Bwana Mungu wako na kutembea katika njia zako na mataifa yote ya dunia watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako. Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako, na uzao wa nchi yako, kama Bwana alivyowaapia baba zako kwamba atakupa.
Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri, nayo ni Mbingu , kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubariki kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi wala hutokopa wewe. Bwana atakufanya uwe kichwa wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapo yasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo,kuyaangalia na kuyafanya; msipokengeuka katika maneno niwaamuruo leo kwa lolote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia. (Kumb 28:1-14)
Damu ya msalaba iliyoondoa dhambi, ndiyo iliyoondoa umasikini pia, Yatupasa kuuona umasikini kama tunavyoiona dhambi. Umaskini ni matokeo ya anguko la mwanadamu katika dhambi. Tukiisha okolewa katika dhambi, yatupasa kuokolewa katika umasikini pia. Utajiri ni matunda ya msalaba kama ilivyo wokovu. Yatupasa kuchukia umasikini kama tunavyochukia dhambi. Kifo cha Yesu, kitakuwa hakina maana kamili, kama tutaokolewa katika dhambi, halafu tubaki maskini katika mwili pia, wakati Yesu aliyefia dhambi, ndiye aliyefia umasikini pia. Msalaba ulifanya vyote, yaaani uliondoa dhambi na umasikini pia. Biblia inasema; “Maana mmejua Neema ya Bwana wetu, Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa masikini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri. Ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake. (2Kor 8:9) … mkitajirishwa katika vitu vyote, mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. (2Kor 9:11)
JE UMEOKOKA? UMEOKOLEWA KATIKA HUKUMU IJAYO?
Yesu alikuja kutafuta na kuokoa sisi tuliopotea. Ndio maana alileta wokovu. Kuokoka si dini Fulani au dhehebu Fulani. Kuokoka uzima wa milele ndani ya mtu. “Amini , amini, nawambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka, yuna (ana) uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”. Ina maana AMEOKOKA kutoka mautini (jehanum). Jehanum ndio mauti ya pili. (Ufu 20:14-15)
Watu wengi wnadhani kutokunywa pombe, kutovuta sigara, kutofanya zinaa, kutoiba, n.k ndio kuokoka na hukumu ya Mungu. Wengi wanadhani, kwenda kanisani, kuimba kwaya, kuhubiri, kuwa mzee wa kanisa au kiongozi wa kikundi, n.k ndio kuokoka na hukumu ya Mungu. Si kweli. Kuna wokovu halisi na matendo au maisha ya wokovu. Watu wengi wanaishi maisha ya wokovu, lakini kwa uhalisi, hawajaokoka bado, hawajampa Yesu mioyo yao na maisha yao.
Kushika sheria za dini na kuishi maisha ya wokovu, siko kunakompendeza Mungu, kama huyo mtu hajampokea Yesu na kumwamini kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. Yesu alisema hivi kwa Mungu Baba, “ Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma” (Yoh 17:3). Hatuokoki na hukumu ya Mungu kwa kushika sheria, bali kwa kuipokea neema ya wokovu kwa kumwamini Yesu Kristo. “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, ambayo hiyo haitokani na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu (zawadi). Wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu (Efe 2;8-9)
Kushika sheria za dini na kuishi maisha ya wokovu, siko kunakompendeza Mungu, kama huyo mtu hajampokea Yes una kumwamini kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. “hali tukijua ya kuwa, mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; Sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria. Maana kwa matendo ya sheria, hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki” (Gal 2:16; Gal 3:7-14) Kuna wokovu halisi na matendo au maisha ya wokovu. Watu wengi wanaishi maisha ya wokovu, lakini kwa uhalisi, hawajaokoka bado, hawajampa Yesu mioyo yao na maisha yao.
Kuna habari ya mtu wa namna hiyo katika Biblia; aliye shika sheria, aliyedumu katika sala, aliyefunga na kuomba, aliyetoa sadaka nyingi kwa watu maskini, n.k lakini alikuwa hajafanya hatua muhimu kuliko zote ya kumwamini na kumpokea Yesu Kristo, ilia pate uzima wa milele na kuokolewa. Aliitwa Kornelio. Isome katika Matendo ya Mitume 10:1-8, 23-48.
Mungu akamhurumia kuwa, japo amekuwa mwaminifu kushika sheria na kuishi maisha ya kumcha Mungu, lakini kwasababu hajamjua Yesu bado, asingeokoka na hukumu ya milele, kwa maana hana uzima wa milele. Mungu akamtuma malaika kumwambia Kornelio, amfuate Petro, naye atamweleza cha kufanya. Ndipo Petro akaja na akamweleza habari za Yesu, Kornelio na familia yake, wote wakamwamini na kumpokea Yesu. Wakapata wokovu halisi (uzima wa milele). Baada ya hapo, maisha ya wokovu ndipo yanakuwa na maana. Kushika sheria za dini na kuishi maisha ya wokovu, siko kunakompendeza Mungu, kama huyo mtu hajampokea Yesu na kumwamini kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. Inawezekana nawe umekuwa mcha Mungu kama Kornelio, lakini hujampokea Yesu moyoni na kumkiri. Mpokee sasa!
NAMNA YA KUPATA WOKOVU (KUOKOKA)
HATUA YA KWANZA; TAMBUA KUWA WEWE NI MWENYE DHAMBI NA UTUBU
DHAMBI ZAKO, KWA KUMAANISHA KUZIACHA.
“Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele” (Rum 3:23). “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja kwa jina la Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.” (Mdo 2:38)
HATUA YA PILI; MWANINI NA KUMPOKEA YESU MOYONI MWAKO. TOA
MAISHA YAKO KWAKE, AWE BWANA NA MWOKOZI WAKO.
Yule mlinzi wa gereza akamwambia Paulo na Sila “Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako” (Mdo 16:30-31).
“Kwasababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, UTAOKOKA. Kwa maana moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri, hata KUPATA WOKOVU. (Rum 10:9-10)
HATUA YA TATU: ISHI MAISHA YA WOKOVU, MAISHA SAFI YA KUMPENDEZA MUNGU NA KUZISHIKA AMRI ZAKE (NENO LAKE)
“nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi… Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua yeye (Mungu) ikiwa tunashika amri zake. Lakini Yeye asema neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli, katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake….” (1Yoh 2:1-6). Kwahiyo sasa, anza maisha mapya ndani ya Yesu.
“…mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita, tazama! Yamekuwa mapya”. (2Kor 5:17) Jitenge na uovu wote na Usiishi katika maisha ya dhambi tena.
Pia soma Josh 1:8 na Rum 6:1-23.
MAMBO 12 YALIYOKUTOKEA MAISHANI MWAKO BAADA YA KUMPOKEA YESU AWE BWANA NA
MWOKOZI WAKO.
Mpendwa, nataka ujue kwamba, Mungu amefanya mambo mengi makubwa katika maisha yako, tangu saa/siku ile ulipompokea Yesu, kuwa Bwana na Mwokozi na Mwokozi wako. Ni muhimu uelewe kwamba, wewe si yule wa zamani tena. Sahau yaliyopita, kwasababu umefanyika kiumbe kipya. (2 kor 5:17)
Yafuatayo ni baadhi ya mambo yaliyotokea kwako tangu ulipofanya uamuzi huu mzuri na wa busara, wa kumpokea Yesu Kristo, kuwa Bwana wako na Mwokozi wa maisha yako.
KWANZA: UMEFANYIKA MWANA WA MUNGU
Umefanyika mwana wa Mungu, kwasababu umempokea Yesu Kristo na kuliamini Jina lake; Kwasababu Biblia inaema “Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake (Yoh 1:12) … Roho (Mtakatifu) mwenyewe, hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu…” (Rum 8:16)
Tangu sasa, wewe ni mmoja wa wana-familia ya Mungu. Nasi tunakukaribisaha kwa upendo wa Kristo. Karibu sana, Baba (Mungu) na sisi tumefurahi kukuona umerudi nyumbani. This is where you belong. We missed you so much. Karibu!
PILI: DHAMBI ZAKO ZOTE ZIMEOSHWA NA KUSAFISHWA KWA DAMU YA YESU NA UMESAMEHEWA KABISA.
Biblia inasema, dhambi zako zote zimeoshwa na kusafishwa kwa damu ya Yesu na umesamehewa zote kabisa, kwasababu umekuja kwa Yesu na umekiri dhambi zako; Kwa maana imeandikwa “katika yeye huyo (Yesu), kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, msamaha wa dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake (Efe 1:17)… Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa nyeupe kama sufu (Isa 1:18)… maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.” (Yer 31:34b) pia soma: Kor 1:14, Ufu 1:5.
TATU: UMEFANYIKA KIUMBE KIPYA
“Hata imekuwa mtu akiwa ndani ya Kristo; amekuwa kiumbe kipya; (mambo ya kale yamepita Tazama! Yamekuwa mapya (2Kor 5:17)… Najua neno moja kuwa, mimi nilikuwa kipofu, na sasa ninaona” (Yoh 9:25)
Kwahiyo sahau maisha yaliyopita, sasa anza maisha mapya ndani ya Yesu.
NNE: ROHO MTAKATIFU ANAISHI NDANI YAKO NA ATAKUWA
PAMOJA NAWE MILELE
“Mkinipenda, mtazishika amri zangu. Nami nitamwomba Baba (Mungu), naye atawapa msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; Ndiye Roho wa kweli, ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwakuwa haumwoni wala haumtambui, Bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu”.
(Yoh 14:15-17) “… Hamjui yakuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu? Na yakuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? Kama mtu alikiharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.” (1Kor 3:16-17)
TANO: UMEHAMISHWA KUTOKA KATIKA NGUVU ZA HETANI au MAMLAKA YA SHETANI au UFALME WA SHETANI, NA KUINGIZWA KATIKA UFALME (MAMLAKA) WA YESU KRISTO.
“Naye (Mungu Baba) alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana wa Pendo lake (Yesu Kristo)” (Kol 1:13)
“Nanyi mfahamu kwamba, mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu, mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa …” (1Pet 1:18)
SITA: UMEHAMISHWA KUTOKA MAUTINI KUINGIA UZIMANI
“Amini amini nawaambia, yeye aliskikiaye neno langu, na kumwamini yeye aliyenipeleka, yuna (ana) uzima wa milele, wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani (Yoh 5:24) “Sisi tunajua yakuwa tumepita kutoka mautini kuingia uzimani…” (1Yoh 3:14). Sasa basi, hakuna hukumu ya adhabu, juu yao walio katika kristo Yesu; kwasababu sheria ya Roho wa uzima, ule ulio katika kristo Yesu, imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. (Rum 8:1-2)
SABA: UMEOKOLEWA AU UMEOKOKA KUTOKA KATIKA GHADHABU NA ADHABU YA MUNGU.
“Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu. Wala hakuachilia ulimwengu wa kale, bali alimhifadhi (alimwokoa) Nuhu mjumbe wa haki, na watu wengine saba, hapo alipoleta gharika, juu ya ulimwengu wa wasiomcha Mungu. Tena akaihukumu miji ya Sodoma na gomora, akiipindua na kuifanya majivu. Akaifanya iwe ishara kwa wtu watakaokuwa hawamchi Mungu baada ya hayo” (2 Pet 2:4-6)
“Dunia ile ya wakati ule, iligharikishwa kwa maji ikaangamia, lakini mbingu za sasa na nchi, zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilohilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na (siku) ya kuangamia kwao, wanadamu wasiomcha Mungu … Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyodhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu yeyote apotee, bali wote wafikie toba …waokolewe na kupata kujua yaliyo kweli.
((2Pet 3:6-7; 1Tim 2:4)
“Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi katika siku hiyo, mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu na vioumbe vya asili vitaunguzwa na kufumuliwa na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea…. mbingu zitfunuliwa, zikiangua na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka. Lakini kama ilivyo ahadi yake, tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. (2Pet 3: 9 -13)
Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki, katika damu yake (Yesu), tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. (Rum 5:9)
(Kwahiyo)ukimkiri Yesu kwa kinywa chako na kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako yakuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka kwa maana, kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, Na kwa kinywa mtu hukiri, hata kupata wokovu, (Rom 10:9 -10)
Kwa maana mmeokolewa (sio, mtaokolewa) bali; MMEOKOLEWA kwa neema, kwa njia ya imani, ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu, wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisfu. (Efe 2:8)
Maana neema ya Mungu, iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa (Tito 2:11) na itakuwa, kila atakayeliitia jina la Bwana, ataokolewa (Mdo 2:21) …. (Petro) Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya; akisema, jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi (Mdo 2:40)
Walipoyasikia haya, wakachomwa mioyo yao, wakmwambia Petro na mitume wengine; Tutendeje ndugu zetu? Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe, kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu nanyi mtapokea kipawa cha Roho mtakatifu (Mdo 2:37-38). Nao waliopokea neno lake, wakabatizwa. Na siku ile wakaongezeka watu (waume) wapata elfu tatu (41)………Bwana akalizidisha kanisa kila siku, kwa wale waliokuwa wakiokolewa (Mdo 2:47)
NANE: JINA LAKO LIMEANDIKWA KATIKA KITABU CHA UZIMA.
“Lakini msifurahi kwa vile peopo wanavyowatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni (Luk 10:20)…“Na ndani ya mji mtakatifu) hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo” (Ufu 21:27) …“Na iwapo mtu yeyote, hakuonekan ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto” (Ufu 20:15)…“Naam, nataka na wewe pia, mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao, maana waliishindania injili, pamoja nami, na wale waliotenda kazi pamoja nami, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uzima (Fil 4:3)
TISA: UMEPEWA (UNAZO) NGUVU NA MAMLAKA YOTE JUU YA SHETANI NA NGUVU ZOTE ZA GIZA.
Hata wakati ule tulipokuwa wafu kwasababu ya makosa yetu, alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema. Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika kristo Yesu. (Efe 2:5-6)….. juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina (au cheo) litajwalo (Efe1:21) (akasema)
”Tazama nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui (shetani), wala hakuna kitu kitakachowadhuru (Luk 10:19)… “Nami nitakupa funguo za ufalme wa mbinguni, na lolote utakololifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni (Math 16:19)… Angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung’oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza, ili kujenga na kupanda (Jer 1:10).
Kila mahali utakapopakanyaga nyayo za miguu yenu, mimewapa ninyi …. hapatakuwa mtu yeyote atakeyeweza kusimama mbele yako, siku zote za maisha yako; kama ulivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakanyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha (Josh 1:3,5) … Muwe na kiasi na kukesha; kwakuwa mshitaki wenu ibilisi, kama simba aungurumaye, huzunguka zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo mkiwa thabiti katika imani … (Basi mtiini Mungu. Mpingeni shetani, naye atawakimbia (Yak 4:7) … “Na ishara hizi, zitafuatana na hao waaminio, kwa jina langu watatoa pepo, watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha (kuua), hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya (Mk 16:17-18)
Pia soma: Dan 7:13,14,27; Yer 51:20
KUMI: UNALINDWA KWA ULINZI WA MALAIKA WA MBINGUNI
Malaika wa Bwana hufanya kituo, akiwaangalia wamchao (Mungu) na kuwaokoa
(Zab 34:7) …“Kwakuwa (Mungu) atakuagizia malaika zake, wakulinde katika njia zako zote (Zab 91:11) … Je? hao (Malaika) wote si roho watumikao, wakitumwa kuwuhudumia wale watakaourithi wokovu? (Ebr 1:7,14) Nani (Yohana) nikaanguka mbele ya miguu yake (Malaika) ili nimsujudie; akaniambia, angalia, usifanye hivi, mimi (Malaika) ni nyoli (Mtumishi) wako na w ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu…(Ufu 19:10) … Awagusaye ninyi, aigusa mboni ya jicho lake (Mungu). Kwa maana, tazama, nitatikisa mkono wangu juu yao … (Zek 2:8-10). Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu, kwa njia ya imani… (1Pet 1:5)
KUMI NA MOJA: UMEFANYIKA MTUMISHI WA MUNGU.
Watu wengi waliookoka hawajioni au hawajihesabu kuwa ni watumishi wa Mungu. Bali huwaona Wachungaji na Wainjilisti kuwa ndio watumishi wa Mungu. Pengine na wewe unajiona hivyo. Lakini neno la Mungu linasema; Sisi Kanisa (Yaani: Jamii ya waaminio au watu waliookoka), sote kwa pamoja, ni mwili wa Yesu Kristo …
Mungu alipomfufua Yesu Kristo kutoka katika wafu, alimtukuza, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; Juu sana kuliko falme zote na mamlaka zote, “Akavitia vitu vyote chini ya miguu yake. Akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote, kwa ajili ya kanisa, ambalo ndilo mwili wake…” (Efe 1:20-23) “Naye (Yesu) ndiye kichwa cha mwili, yaani cha kanisa….” (Kol 1:18) … Basi ninyi nimekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake… kwa maana katika Roho mmoja, sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu wayahudi, au kwamba tu wayunani; ikiwa tu watumwa, au ikiwa tu huru;
Nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja, kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi… Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na vioungo vyote vya mwili ule navyo ni vingi, na viungo vyote vya mwili ule navyo ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo. (Kor 12,27,13-14,12) … “Basi pana tofauti za karama; Bali Roho ni (mmoja). Tena pana tofauti za huduma, (lakini) Bwana ni mmoja. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni (mmoja) azitendaye kazi zote katika wote. Lakini Kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kusaidiana. (1kor 12:4-7)
Angalia hili neno “kila mmoja”
“…Mungu amevitia viungo kila Kimoja katika mwili, kama alivyotaka. Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. kila mmoja katika mwili, kama alivyotaka. Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. “(1Kor 12:18-20)
Angalia hilo neno tena “kila kimoja” limejirudia.
“ Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa (kama) apendavyo Roho yeye yule; mwingine (hupewa) imani katika Roho (huyo huyo); na mwingine hupewa kaama za kuponya katika Roho yule mmoja; na mwingine (hupewa) unabii; na mwingine (hupewa) kupambanua roho; na mwingine (hupewa) aina za lugha; na mwingine (hupewa) tafsiri za lugha; Lakini kazi hizi zote, huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake, kama apendavyo yeye. (!Kor 12:8-11)
Angalia hilo neno “kila mmoja” limejirudia tena
Kwa hiyo, kama vile katika mwili, kila kiungo kina kazi yake (ya kujenga mwili); Vivyo hivyo, katika mwili wa Kristo, yaani Kanisa, kila muumini, ana kazi yake ana huduma yake, na karama yake na wajibu wake, katika kujenga mwili wa Kristo. Wewe na mimi, tu watumishi wa Mungu. Jione hivyo na ujihesabu hivyo. Mungu anataka utumie karama na uwezo aliokupa, ili kuuvunja ufalme wa shetani, na kujenga ufalme wa Kristo duniani. Neno la Bwana likamjia, kusema, kabla sijakuumba katika tumbo, nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; Nimekuweka kuwa nabii wa Mataifa. Ndipo niliposema, Aah! Bwana Mungu! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto lakini Bwana akaniambia, usiseme mimi ni mtoto; … usiogope kwasababu ya hao, maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema. Bwana.
Ndipo Bwana, akanyoosha mkono wake, akanigusa kinywa changu; Bwana akaniambia; Tazamani, nimetia maneno yangu kinywani mwako; Angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung’oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; Ili kujenga na kupanda (Yer 1:4 -10) “… enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi (wangu) mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu; Na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari. (Math 28:18-20).
KUMI NA MBILI: UMEPEWA AHADI KUBWA MNO NA ZA THAMANI NA MUNGU
Tangu umeingia katika familia ya wana wa Mungu umepewa urithi wa baraka za Mungu. Umeingizwa katika mkondo wa baraka na ahadi kubwa na nyingi mno katika kriso Yesu.
“Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana (wa Mungu), Mungu alimtuma Roho wa mwanawe mioyoni mwetu, aliaye Aba, yaani Baba. Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena, bali u mwana (wa Mungu); Na kama u mwana, basi u mrithi kwa Mungu” (Gal 4:6-7)
“Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu…, ili kwamba, Baraka ya Ibrahimu, iwafikie mataifa ktika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya roho kwa njia imani … Na kama ninyi ni wa kristo, basi mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawa sawa na ahadi” (Gal 3:13-14,29).
“Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa Baraka zote za rohoni, katika ulimwengu waro ho, ndani yake Kristo. (Efe 1:3)… Tena kwa hayo, ametukirimia ahadi kubwa mno za thamani, ili kwamba, kwa hizo (ahadi na baraka) mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani, kwa sababu ya tamaa.”(2Pet 1:4) Kwa mfano:-
Ahadi ya Baraka – Kumb 28:1 – 14; Law 26:1-13
Ahadi ya mafanikio – Zab 1:1 -3; Josh 1:8-9
Ahadi ya utajiri – Kumb 15:14; 2Kor 8:9 / 2Kor 9:8,11
Ahadi ya Afya njema – Kut 15:26: Kumb 7:15
Ahadi ya Ulinzi – Zab 91:11; Zab 121:1-8
Ahadi ya Akili nzuri – Zab 119:97-100; Zab 111:10
Ahadi ya Wokovu kwa familia - Mdo 16:31; Isa 54:13 – 14
UHAKIKA WA WOKOVU.
Sasa elewa vizuri kuwa, TAYARI UMEOKOLEWA, hapa hapa duniani, na si baada ya kufa. Kwasababu Biblia inasema, “Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa (ni) hukumu”
(Ebr 9:27). Mungu ametuletea wokovu hapa hapa duniani, ili tuupokee hapa hapa duniani. Baada ya kufa, hakuna wokovu tena, bali hukumu. Mtu anayesubiri wokovu baada ya kufa, atakuwa amechelewa!
Kumbuka habari ambayo Yesu alisema “Palikuwa na mtu mmoja tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula siku zote kwa anasa. Na alikuwepo masikini mmoja, jina lake Lazaro, aliyewekwa mlangoni pa tajiri, na ana vidonda vingi. Naye masikini alitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri, hata mbwa wakalamba vidonda vyake”.
Hii ina maana kwamba, tajiri hakuwa mcha Mungu; Kwa maana hakumjali masikini, pamoja na kwamba alikuwa na uwezo. Masikini alikuwa na hali mbaya sana, ya njaa na ugonjwa, hata hakuweza tena kuwafukuza mbwa waliomkaribia. Ndio maana, Tajiri alipokufa, alikwenda motoni. “ikawa yule masikini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu”. (Hii ina maana, masikini alikuwa mcha Mungu). “Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwasababu ninateswa katika moto huu. Ibrahimu akasema, mwanangu, kumbuka ya kwamba, wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi, kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu, wasivuke kuja huku.
(Tajiri) akasema, basi, Baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu (duniani), kwakuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso. Ibrahimu akasema, (kule duniani) wanao Musa na Manabii; na wawasikilize wao. (Tajiri) akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu. (Ibrahimu) akamwambia, wasipowasikia Musa na Manabii (wahubiri mbalimbali), hawatashawishiwa, hata mtu akifufuka katika wafu”.
BAADA YA KUFA NI HUKUMU! HAKUNA WOKOVU! Mungu ametuletea wokovu hapa hapa duniani, ili tuupokee hapa hapa duniani, kabla ya kifo kutujia. Baada ya kufa, hakuna wokovu tena, bali hukumu. Mtu anayesubiri wokovu baada ya kufa, atakuwa amechelewa, kama yule Tajiri!
Ni muhimu pia uelewe kwamba, tajiri hakwenda motoni kwa sababu alikuwa tajiri; wala masikini hakusalimika au hakuokoka kwasababu alikuwamasikini. Utajiri si dhambi, wala umasikini si utakatifu. Uhusiano wako na Mungu ndicho kitu kitakachoamua utakwenda kuishi wapi milele. Wala si fedha yako, wala elimu yako, wal dini yako! Kitu pelee kitakachoamua wapi utaishi milele, ni uhusiano wako na Mungu. “Basi tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote NA HUO UTAKATIFU (ucha Mungu) ambao hapana mtu atakayemwona Mungu, asipokuwa nao” (Ebr 12:14)
Unaweza ukaupata ulimwengu wote, ukawa na kila kitu duniani; utajiri, elimu nzuri, dini nzuri, kazi nzuri, nyumba nzuri, mshahara mzuri, magari mazuri, viwanda hata migodi ya thamani. Lakini kama huna wokovu, yaani uhusiano mzuri na Mungu, hutaweza kuingia mbinguni. “Kwani itamsaidia nini mtu, akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake?” (Math 16:26) Hakuna faida!
Utajiri halisi ni ule wa ndani (wokovu) ukiunganishwa na wanje (mali na pesa). Ndio maana Yesu anasema “Nayajua matendo yako, yakuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. Basi kwasababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. Kwakuwa wasema, mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe ni mnyonge, na mwenye mashaka, na masikini, na kipofu, na uchi.” (Ufu 3:15-17).
Kumbe unaweza ukavaa na kupendeza mbele za watu, na kumbe mbele za Mungu uko uchi kabisa! Unaweza ukawa mbabe na mjanja mbele za watu, na kumbe mbele za Mungu ukawa mnyonge na si kitu kabisa! Unaweza kudhani unaona kwa macho, na kumbe umefichwa vitu vingi halisi, huvioni! Unaweza ukawa tajiri wa mali za ulimwengu, na kumbe mbele za Mungu ukawa masikini kabisa, kwasababu huna ule utajiri halisi, yaani wokovu. Yesu anamalizia kwa kusema “Nakupa ushauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto (yaani WOKOVU), UPATE KUWA TAJIRI, na mavazi upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.”
Dhahabu inayotajwa hapo ni WOKOVU, kama ilivyoandikwa katika Mathayo 13:44-46; “Tena Ufalme wa mbinguni umefanana na HAZINA iliyositirika katika shamba, ambayo mtu aliopoiona, aliificha; na kwa furaha yake, akaenda akauza vyote alivyo navyo, akalinunua lile shamba. Tena Ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta LULU NZURI; naye alipoona LULU MOJA YA THAMANI KUBWA, alikwenda akauza vyote alivyo navyo, akainunua”. Hapa, tunaambiwa habari za wokovu kuwa ni KITO cha thamani! Wokovu ni LULU! Wokovu ni DHAHABU Ya thamani nyingi! Wokovu ni HAZINA njema!
Maadam umempokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako, Mungu anakwambia “unao uzima wa milele” sasa hivi ukiwa hapa hapa duniani. “Amini amini nawaambia, yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka, YUNA (ANAO) UZIMA WA MILELE; WALA HAINGII HUKUMUNI, BALI AMEPITA KUTOKA MAUTINI KUINGIA UZIMANi” (Yoh 5:24). Mungu anakwambia “unao uzima wa milele” sasa hivi ukiwa hapa hapa duniani. Sio kwamba “utakuwa nao” bali ansema “unao” yaani sasa! Na tena anasema, kwa kuwa unao uzima moyoni mwako, hutaingia hukumuni, bali “umepita” kutoka mautini kuingia uzimani! Sio “utapita”, bali Mungu anasema, “tayari umepita” kutoka mautini, kuingia uzimani.
Pia imeandikwa hivyo katika 1Yoh 3:14. Na tena 2Wakorintho 6:2 inasema; “… Tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; TAZAMA, SIKU YA WOKOVU NDIO SASA.
Baada ya kufa, hakuna wokovu tena, bali hukumu. Mtu anayesubiri wokovu baada ya kufa,atakuwa amechelewa!
UWE NA UHAKIKA WA WOKOVU WAKO. JUA KWAMBA, KWA NEEMA YA MUNGU, UMEOKOKA! Kwa maana imeandikwa “MMEOKOLEWA KWA NEEMA, KWA NJIA YA IMANI; HIYO HAIKUTOKANA NA NAFSI ZENU, NI KIPAWA CHA MUNGU”. (Efe 2:8)
KANUNI ZA MAISHA YA KILA SIKU YA KIKRISTO.
(KANUNI ZA MAISHA YA WOKOVU)
Mpendwa, inabidi ufahamu kwamba, kuokoka haimaanishi tayari umefika mbinguni; Bali inamaana kwamba; ndio tu umeanza safari salama ya kwenda mbinguni. Mtu ambaye hajaokoka, ni kwamba hajaanza kabisa safari ya kwenda mbinguni. Na unafahamu kwamba, wakati mwingine, si wasafiri wote humaliza safari zao; Kwasababu katika safari huwa kuna vikwazo mbalimbali. Wengine huishia mwanzoni kabisa mwa safari, wengine huishia katikati ya safari na wengine huishia mlangoni kabisa na kushindwa kuimaliza safari.
Safari ya mbinguni pia, ina vikwazo vingi. Ndio maana Biblia inasema “mlango ni mwembamba na njia imesonga, iendayo uzimani” (Math 7:14). Ni shauku ya Mungu na yetu pia, kwamba uimalize salama safari yako ya kwenda mbinguni, ambayo uliianza siku uliyompa Yesu Kristo maisha yako na kuokoka. Si njia rahisi. Kuna mambo mengi ya kukukwaza na kukuzuia. Lakini Mungu amekuahidi ushindi katika mambo yote hata kukufikisha mbinguni salama.
Biblia inasema; “Hata (Mitume) walipokwisha kuihubiri injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, wakifanya imara roho za wanafunzi, na kuwaonya wakae katika ile imani, na yakwamba imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi” (Mdo 14:21-22). Yesu alisema; “Ulimwenguni mnayo dhiki, lakini jipeni moyo, mimi (Yesu) nimeushinda ulimwengu” (Yoh 16:33). Lakini “Katika mambo yote tunashinda na zaidi ya kushinda, katika yeye (Yesu) aliyetupenda” (Rum 8:37). Hebu sema kama Paulo “Nayaweza mambo yote, katika yeye (Mungu) anitiaye nguvu” (Fil 4:13)
Ebr 11:32-38 inasema “Na niseme nini tena? Maana wakati usingetosha kuleta habari za Gideoni, na Baraka, na Samsoni, na Yefta, na Daudi, na Samweli, na za Manabii; Ambao kwa imani, walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga, walitiwa nguvu baada ya kuwa wadhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni. Wanawake walipokea wafu wao, waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuwawa … wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam kwa mafungo na kwa kutiwa gerezani. Walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuwawa kwa upanga, walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; … wakiteswa, wakitendwa mabaya; … Walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima, na katika mapango na mashimo ya nchi.”
Haiwezekani hawa mashujaa wa imani, washinde vita na upinzani huo, na kuingia mbinguni kwa ushindi, kwa nguvu zao wenyewe. Ni lazima kuna siri fulani iliwasaidia kumaliza safari yao kwa ushindi. Siri hizo na kanuni hizo ndizo zilizowasaidia wengi na ndizo zinazotusaidia wengi, kuishi maisha ya wokovu kwa ushindi.
Mpendwa, fahamu kwamba, NEEMA YA WOKOVU ambayo umepewa na Yesu, ni ya thamani kuu kuliko kitu chochote duniani. Hakuna fedha wala dhahabu inayoweza kununua wokovu. Wala hakuna kitu chochote duniani kinachoweza kulingana na wokovu ambao Yesu ametupa. Si fedha, wala dhahabu, wala almasi, wala elimu, wala cheo, wala pesa au chochote kinachoweza kulingana na zawadi ya wokovu tulionao katika Yesu. Wokovu ulionao sasa, ndicho kitu cha gharama zaidi na cha thamani zaidi kuliko vitu vyote duniani.
Kila kitu cha gharama kama vile redio, televisheni, friji, gari, compyuta, n.k. hutengenezwa na kuuzwa pamoja na kitabu chenye maelezo ya jinsi ya kukitumia (manual book), kinachokuwezesha kukitumia hicho kifaa au chombo, kwa usahihi bila kukiharibu. Kama mmiliki wa kifaa au chombo hicho hatafuata maelekezo ya watengenezaji wa chombo kile, basi kifaa hicho kitaharibika na kushindwa kulitimiza kusudi lake.
Vivyo hivyo, na WOKOVU huu tuliopewa na Bwana Yesu, ni wa thamani na gharama kubwa, tena unaweza kuharibika kirahisi (very fragile). Hivyo, unatakiwa kuutunza kwa umakini na uangalifu mkubwa, kwa kufuata maelekezo, kanuni na siri za maisha ya wokovu. Siri hizo na kanuni hizo, ndizo zilizowasaidia wengi na ndizo zinazotusaidia wengi, kuishi maisha ya wokovu kwa ushindi, bila kuharibu. Bwana Yesu mtoa uzima, na aliye mwanzilishi wa wokovu wetu, ametupa kitabu cha maelekezo (manual book) cha namna ya kuutunza wokovu wetu, ili tusiuharibu, tusiuchafue wala kuupoteza. Kitabu hiki kinaitwa BIBLIA TAKATIFU!
Kila siku hakikisha unasoma maelekezo ya kutosha kwa ajili ya wokovu wako. Na kwa kuyafuata maagizo ya NENO LA MUNGU, hautaweza kamwe kuuharibu, kuuchafua au kuupoteza wokovu, yaani uhusiano mzuri na Mungu. Nawe utaweza kuimaliza safari yako ya mbinguni kwa salama na uhahika, kama wale mashujaa wa imani. Angalia maandiko yanavyosema; “Kitabu hiki cha torati (Neno la Mungu) kisiondoke kinywani mwako; bali uyatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawa sawa na maneno yake yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana”. (Joshua 1:8)
KANUNI ZA MAISHA YA USHINDI
1. DUMU KATIKA MAOMBI – ONGEA NA MUNGU KILA SIKU
KWA SALA NA MAOMBI.
“Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba, huku na shukurani …” (Kol 4:2) “… imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala msikate tamaa” (Luk 18:1) … “Kwa sala zote na maombi, mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote”
(Efe 6:18) … “Furahini siku zote; ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo, maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika kristo Yesu.” (1Thes 5:16-18)
Kwanini Biblia inasisitiza sana tudumu katika maombi? Maombi ni namna ya wewe kuwasiliana na Mungu Baba. Tangu umeokoka, umefanyika mwana wa Mungu. Maongezi huunganisha familia. Maongezi huimarisha uhusiano. Ili uzidi kukua katika kumjua Mungu na uhusiano wako na Mungu uweze kuimarika, yakupasa kudumu sana katika maombi na sala. Tamani kujifunza kuomba, tena tamani kiwango chako cha maombi kiongezeke. “Ikawa (Yesu) alipokuwa mahali fulani akiomba, alipomaliza, mmoja katika wanafunzi wake akamwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake” (Luk 11:1).
Katika maombi kuna faida nyingi;-
Kwa mfano:
(i) Katika maombi unapata kumjua Mungu na kuwa karibu nae zaidi.
ii) Katika maombi unapata uongozi wa Mungu na kujua mapenzi ya Mungu
(iii) Katika maombi unapata nguvu za kushinda dhambi na majaribu.
(iv) Katika maombi anapata nguvu za kumpinga shetani na kuvunja kazi zake.
(v) Katika maombi unapata kumweleza Mungu mahitaji yako na haja zako.
(vi) Katika maombi unapata kukua katika karama, huduma na vipawa.
(vii) Katika maombi unapata amani na kujaa furaha ya Roho Mtakatifu.
(viii) Katika kuomba unapata baraka na kibali cha Mungu (favour) maishani .
Ndio maana Neno la Mungu linasisitiza kudumu katika maombi. Tenga muda wa kuomba kila siku. Na uwe mwaminifu. Utaona furaha, amani, Baraka, Ushindi na Mafanikio katika maisha yako na kazi zako.
Uwe na muda wako binafsi, wa kufanya maombi. Biblia inasema, Yesu alituonyesha mfano; “Walikwenda kila mtu nyumbani kwake; naye Yesu akaenda mpaka mlima wa Mizeituni (kuomba) (Yoh 8:1) … Hata alfajiri na mapema sana, akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko. (Mk 1:35) Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. (Math 14:22-23) … Yeye (Yesu) siku hizo za mwili wake, alimtolea (Mungu) maombi na dua na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu. (Ebr 5:7)
2. SOMA BIBLIA – MRUHUSU MUNGU ASEME NAWE KILA SIKU KWA NENO LAKE.
“Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana”
(Kol 3:16) …” kila andiko lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema” (2Tim 3:16-17) … “kama watoto wachanga waliozaliwa sasa, yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu”. Kitabu hiki cha torati (Neno la Mungu) kisiondoke kinywani mwako; bali uyatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawa sawa na maneno yake yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana”. (Joshua 1:8) Neno la Mungu li hai lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga ukatao kuwili…” Ebr 4:12-13, Pia soma Ebr 5:12-13.
3. KUSANYIKA / JUMUIKA NA WAAMINIO WENGINE, KUMWABUDU MUNGU
NA KUJIFNZA NENO LA MUNGU.
“Bwana akalizidisha kanisa kila siku, kwa wale waliokuwa wakiokolewa … na watu walioamini, walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika … na siku zote kwa moyo mmoja, walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha, na kwa moyo mweupe, wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote … wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali. (Mdo 2:42-47) … Tena nawaambia, ya kwamba, wawili wenu watakapo patana duniani katika jambo lolote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu; nami nipo papo hapo katikati yao (Math 18:19-20). Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana (Kol 3:16)
Pia soma 2Tim 2:22; Heb 5:12-13.
4. ISHI MAISHA MASAFI NA MATAKATIFU, YANAYO MPENDEZA MUNGU
“Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Hasha! Sisi tulioifia dhambi, tutaishije tena katika dhambi? … Tukijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale, ulisulubishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilika, tusitumikie dhambi tena; … Vivyo hivyo, ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu wa dhambi, na walio hai kwa Mungu, katika Kristo Yesu … Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa zenu; wala msiendelee kuvitoa viungo vyenu kuwa silaha za dhuluma kwa dhambi; Bali jitoeni wenyewe kwa Mungu, kama walio hai baada ya kufa, na (vitoeni) viungo vyenu kwa Mungu kuwa silaha za haki. Kwa maana dhambi haita watawala ninyi, kwasababu hamuwi chini ya sheria, Bali chini ya Neema.
… Lakini Mungu na shukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa mioyo yenu ile maana ya elimu (wokovu) ambayo mliwekwa chini yake; na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki … kwakuwa kama mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo sasa, vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa.
Kwa maana mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki. Ni faida gani basi mliyoipata siku zile kwa mambo hayo mnayoyatahayarikia sasa? Kwa maana mwisho wa mambo hayo ni mauti. Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele. Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; Bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu, Bwana wetu. (Rum 6:1-2, 6, 11-14, 17-23)
Basi nasema neno hili, tena nashuhudia katika Bwana, tangu sasa msienende kama mataifa waenendavyo, katika ubatili wa nia zao; ambao akili zao zimetiwa giza, nao wamefarakanishwa na uzima wa Mungu, kwasababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwasababu ya ugumu wa mioyo yao; ambao wakiisha kufa ganzi, wanajitia katika mambo ya ufisadi (uchafu), wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani. Bali ninyi, sivyo mlivyojifunza Kristo; ikiwa mlimsikia mkafundishwa katika yeye, kama kweli ilivyo katika Yesu, mfue kwa habari ya mwenendo wa kwanza, utu wa zamani, unao haribika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya. Na mfanye wapya katika roho ya nia zenu, mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli (Efe 4:17-24)
“Iliyobaki ndugu, tunawasihi na kuwaonya kwamba, mwenende katika Bwana Yesu; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza Mungu, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana. Kwakuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu. Maan hayo ndiyo mapenzi ya Mungu, (ndiyo) kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; Kila mmoja wenu, ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima; si katika hali ya tamaa mbaya, kama mataifa wasiomjua Mungu. (1Thes 4:1-5) … “Jitengeni na ubaya wa kila namna” (1Thes 5:22), “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na (pia tafuteni kwa bidii kuwa na) huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana, asipokuwa nao.” (Ebr 12:14) …“Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, mtakuwa watakatiku, kwa kuwa mimi ni mtakatifu” (1Pet 1:15-16)
5. UWE SHAHIDI WA YESU KWA WATU WENGINE.
“Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu” (1Kor 4:1) … Kwa urahisi kabisa, mwambie mtu mwingine, mambo ambayo Mungu amekutendea, ya kwamba Mungu ameyabadilisha maisha yako. Waambie kwamba, ulikuwa na maisha maovu na kwamba Yesu amekusamehe, amekuokoa na amekupa maisha mapya, ambayo ndiyo maisha ya uzima milele. Kisha waambie kuwa, Yesu anawapenda, na anataka kuingi katika maisha yao. Waulize kama wako tayari kumpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Kama wako tayari, waombee wapokee wokovu kama wewe; Nawe utakuwa mtumishi wa Mungu kwa kuifanya kazi ya Mungu.
Wewe ni mtumishi wa Mungu (1Kor 4:1) Yesu anakwambia “Enenda zako, nyumbani kwako, na kwa watu wa kwenu, kawahubiri ni mambo gani makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokurehemu. Akaenda zake, akaanza kuhubiri katika Dekapoli, ni mambo gani makuu, Yesu aliyomtendea; watu wakastaajabu”. (Marko 5:19)
NAMNA YA KUSHUHUDIA INJILI KWA WATU WENGINE.
Waeleweshe kwamba;
WANADAMU WOTE TUMEFANYA DHAMBI.
“… (wanadamu) wote tumefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu” (Rum 3:23)
ADHABU YA MUNGU INAUJIA ULIMWENGU WOTE.
“…mbingu na nchi zimewekwa akiba kwa moto, zikilindwa hata siku ya hukumu, na kuangamia kwao wanadamu wasio mcha Mungu” (2Pet 3:7)
HAKUNA MWANADAMU ANAYEWEZA KUJIOKOA MWENYEWE.
“ni nani awezaye kuokoka? Yesu akawakazia macho akawaambia, kwa wanadamu, hilo haliwezekani; Bali kwa Mungu, yote yanawezekana” (Math 19:25-26)
IKO NJIA MUNGU AMEANDAA, YA KUOKOKA KATIKA ADHABU HIYO.
YESU NDIYE NJIA YA KUOKOKA NA HUKUMU YA MUNGU.
“ Yesu akamwambia, Mimi ndimi Njia, na Kweli, na Uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya Mimi” (Yoh 14:6) “Aniaminiye Mimi , anao uzima … haingii hukumuni, bali amepita kutoka hukumuni kuingia uzimani” (Yoh 5:24) Ukimkiri na kumwamini ……utaokoka”
(Rum 10;9-10)
MUULIZE KAMA YUKO TAYARI KUMWAMINI NA KUMPOKEA YESU.
MWONGOZE SALA YA TOBA NA KUPOKEA WOKOVU. (Mdo 8:35-39)
Kwa mfano;
Ee Bwana Yesu, ninakuja kwako. Ninakiri mimi mwenye dhambi na makosa mengi. Nazijutia dhambi zangu na kutubu kweli. Ninaomba unisamehe na kuniosha kwa damu yako ya thamani. Ninaomba uniokoe maisha yangu. Nafungua moyo wangu na ninakukaribisha. Ingia ndani yangu kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Uwe Bwana na Mwokozi wangu tangu sasa. Weka ndani yangu, uzima wa milele na uhakika wa wokovu. Asante Yesu kwa kuniokoa. Naomba unipe nguvu za Roho wako Mtakatifu, nianze maisha mapya, nisirudi nyuma tena. Katika jina la lako takatifu, Yesu Kristo, ninaomba na kushukuru, Amen.
WEWE NI MSHINDI.
Mpendwa, nataka kukwambia, tunaishi katika ulimwengu mbaya na mchafu sana. Lakini katikati yake, kuna watu walioipata furaha na amani ya kweli, ambayo ni bora na ya thamani mno kuliko vitu vyote. Watu hawa wanadharauliwa na kutukanwa, wengine wanateswa na kunyanyaswa, lakini wao hawajali. Wanachukiwa na ulimwengu wote lakini siku zote , wamejaa furaha na amani ya Mungu. Ni mabwana wa nafsi zao, wameushinda ulimwengu na hakuna kinachoweza kuwazuia. Wanaonekana wako katika upande wa washindi tu.
Watu hawa wanaitwa WAKRISTO. WAMEOKOKA, WAMEJAZWA NA ROHO MTAKATIFU na WANAKWENDA MBINGUNI. Nataka ujue kwamba, MIMI PIA MMOJA WAO! Na kwasababu NA WEWE UMETUBU DHAMBI ZAKO NA KUMPOKEA YESU KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKO, WEWE PIA NI MMOJA WETU. NASI TUNAKUKARIBISHA KATIKA FAMILIA YA MUNGU, KWA UPENDO MKUBWA.
YESU ANAKWAMBIA; “…USIOGOPE WALA USIFADHAIKE, KWA KUWA BWANA MUNGU WAKO YUKO PAMOKA NAWE KILA UENDAKO … SITAKUACHA WALA SITAKUPUNGUKIA ….NIKO PAMOJA NAWE HATA MWISHO WA DUNIA …. UWE MWAMIIFU HATA KUFA, NAMI NITAKUPA TAJI YA UZIMA.
(Joshua 1:9,5 Math 28:20 Uu 2:10)
“Kwasababu hiyo, tangu (sisi) tulipopata habari za imani yenu katika Bwana Yesu, na pendo lenu kwa watatakatifu wote, hatuachi utoa shukrani (kwa Mungu) kwa ajili yenu na tukiwakumbuka katika sala zetu, ili Mungu wa Bwana Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima naya ufunuo katka kumjua yeye; macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la wito wake jinsi lilivyo, na utajiri wa utukufu wa urithi wake kwa watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi, kwa kadri ya utendaji wa nguvu za uweza wake ….” (Efe 1:15-19),
“Desciples of Christ” tunakuombea sana. Ni kwasababu tunakupenda na tunakujali. Ni maombi yetu kwa Mungu Baba kwamba, uweze kukuwa katika neema ya wokovu na katika kumjua sana Yesu Kristo Bwana na kuimaliza safari yako salama ya kwenda mbinguni. Nasi tunaamini kabisa ya kuwa “Yeye (Mungu) aliyeanzisha kazi njema mioyoni mwenu, ataimaliza (ataikamilisha) hata siku ya Kristo Yesu.” (Fil 1:6)
Nina Mushukuru Mungu kwayote ametufanyiya ninawashukuru nanyinyi kwa mafudisho mazuri tena yamaana mimi nina simamiya ministri inaitwa BETHISAIDA MINISTRY OF RWANDA kwahiyo nina wasarimu kwa jina la Yesu.
kweri kuhusu mafudisho ya wokovu nimeshukuru nanitaedere kufuata mafudisho yote
Pastor Mukongo wa Rwanda, mimi Mwalimu Mgisa, niliyeandika MAANA YA WOKOVU. Nimetiwa moyo sana kwa kuweza kukufikia huko Rwanda. Thank God for this technology. You are in our Prayers.
Mwalimu Mgisa unatupeleka hatua nyingine ya wokovu. Hakika Mungu akubariki uzao wako na Vick
Mimi naitwa Mary Ngowi. Kwa hakika sasa hivi Mungu anaonekana kila mahali hata kwenye mipaka na nje ya nchi yetu. Ubarikiwe sana Mtumishi wa Mungu kwa kufunuliwa yote haya. Naomba tuendelee kuombeana ili Mungu aendelee kutenda kazi zaidi na watu wake pia Taifa letu lote la Tanzania.
Mungu akubariki sana kwa article yako nzuri na yenye mafundisho matamu kuliko asali.
Mary
Through your message i got point and encouragement for being more reading, if possible will you continue to supply this message through my mail?
GOD BLESS YOU.
Firstly I would like to thank God for leading me to this site
I ask blessing from above to whoever wrote/posted this.
may the Lord bless ya more and more.
asante sana kwakujitoa kwa sababu ya kazi ya Mungu bwana alietuokoa
that’s what makes me happy kuona neno la Mungu lina fundishwa/hubiriwa kwa jnia yoyote ambayo iko possible.
Keep it up man, Mungu azidi kuku bariki coz kwa huu ujumbe wa Mungu kupitia wewe najifunza mengi na nitajifunza mengi na Imani inazidi kuongezeka day by day as I read this article.
Ujumbe huu unani encourage me everyday I read it
may the Lord bless ya
kazi yenu ni njema mbarikiwe
Shalom, Ninamshukuru sana mungu kwa ajili ya mwalimu aliyeandika somo hili. kazi yenu ni njema sana na Mungu azidi kuwabariki watu wengi zaidi wazidi kufunguliwa kupitia huduma yenu.
Ninaitwa Musa Luzali, nimebarikiwa sana na mafundisho ya awali yampasayo mkristo kuyafamu ili kuwa na uhakika na wokovu wake kwa Bwana Yesu.
What I want to suggest to you is about all the people who are unreached by the gospel; How are you going to consider them in order that they could get this teaching because they lack the true Jesus’gospel. I’m myself interested in those who are unreached.
My request is; May you please send this teaching to me as a handout so that I could use it for teaching!
Mungu akubariki sana mtumishi wa Mungu kwa kuandika somo hili kwa kina cha kutosha. Mungu aongeze wigo wa huduma yako ifike hadi miisho ya dunia. Tunao watumishi wazuri sana Tanzania tuzidi kuwaombea Mungu awatunze na kuwainua zaidi kwa ajili ya ufalme wake. Nasema Tena mwalimu Mgisa Ubarikiwe na dada Mary Ubarikiwe kwa huduma hii. Tuko pamoja na wewe kuhakikisha kazi hii inazaa matunda katika ufalme wa Mungu.
Praise the most high God and Lord Jesus Christ;I am very thankful before our living father God for raising such kind of people in my home country who real teaches such kind of the truth.My request to you is to publish the books which will contain all these teachings, through books these teachings will not only help our present generation church but also to the feature one.May the Lord bless you more and keep you.I pastor Bruno South Korea.
Kwangu mimi kuokoka ni kubadilika, yaani kumkabidhi YESU maisha, Mtu hupitia hatua tatu katika tendo la wokovu. Hatua ya kwanza ni ile ya KUJIKANA, YESU anasema atakaye kunifuata sharti ajikane mwenyewe hivyo hiyo ni hatua ya kujikana. Hatua ya pili ni kujitwika msalaba, Baada ya kujikana YESU anasema jitwike msalaba, hii ndiyo ile hatua ambapo mtu anaongozwa sala ya toba, yaani kumkataa shetani. YESU anasema atakayenikiri machoni pa watu nami nitamkiri mbele za baba yangu.Hatua ya tatu ni ile ya kumfuata YESU, hii ndiyo hatia ngumu ambapo wokovu wa kweli huonekana hapa, kuna milima na mabonde katika kumfuata YESU, ndiyo maana YESU anasema watu hao mtawatambua kwa matendo. Hivyo hizo ndizo hatua tatu za wokovu, wewe uliyeokoka hebu jiangalie katika hatua hizo zitumie kama kioo.
Thanks very much for this programme am very much blessed and kindly request a handout of your teaching because sometime its expensive for me to access at the cybercafe. Godbless you as your doing this hard job, you will receive your reward at the end of it.
Await to here from you.
Margaret
Hii package ya mafundisho ya msingi kwa Wakristo wapya ni nzuri sana,itamsaidia Mkristo mchanga na hata mwalimu pia,nawahimiza watumishi wenzangu wanaojua wana masomo yakuwafaa wengine waige mfano wako wa kufanya mafundisho yao kupatikana kwenye mtandao,wengi watafaidika na mwili wa Kristo utajengwa,Mungu akubariki sana,ni ”heri kutoa kuliko kupokea,Mdo 20:35”.
Asante sana Bra.Mgisa Mungu akutumie zaidi na zaidi.
Vizuri sana Mml. Mgisa kwa somo hilo zuri sana Mungu akubariki,akuzidishie siku za kuishi hapa duniani ili uwatoe watu ktk utumwa wa dhambi kwa njia ya NENO.
AMEN.
Brother Mgisa big big Job, Warm up the sky!
Very handy teachings, i real love them, Highly appreciated.
Worthy to be read by new and older born again christians and those who are not! i can see the msg is very broad to all of us, spare few minutes and see it pays back.
Me and My Siti Msharifu
Love you Mr & Mrs Mgisa Victoria William Mtebe
GLORY,GLORY TO GOD!
BRO.Mgisa Mtebe ninaungana na wote kukutakia Roho wa Neema azidi kukuangazia,BW.Asifiwe!
nina kitabu chako cha “NGUVU YA MAOMBI”.
PIA Dada Mary pongezi sana you will real never miss 2 shine like a star.
Stay Shining.
Love You Much 4 ur gud job!!
Mungu akubariki sana mtumishi wake maana amekutumia na anaendelea kukutumia katika kuihubiri injili ya mwanae mpendwa Yesu Kristo.kwakweli nimebarikiwa sana na mafundisho yako na hakika Mungu atakubariki nakwa hili pia.Pia naomba nami unikumbuke katika maombi yako ili Mungu azidi kunitia nguvu katika kuliitia jina la YESU KRISTO ambaye ni Bwana na muokozi wa maisha yetu.AMEN.
Haleluya,
Jina la Bwana libarikiwe, ubarikiwe Mtumishi kwa huduma nzuri songa mbele, somo hili ni baraka na ni msingi muhimu wa maisha ya mtu aliyeokoka.
Bwana Yesu asifiwe wapendwa, mungu awabariki sana waandaji wa hii mada kwani ninaamini kama nilivyofunguliwa mimi baada ya kusoma neno hili la Mungu kila mmoja atakuwa amebarikiwa nalo hivyo hivyo nawaaombeeni sana Mungu awape kila la kheri ili muuweze kuendelea mbele kama Wana wa Israel kutulisha neno la Mungu. Nimmempikia dada Helen baada ya kusoma neno hili hapo ofisini kwenu na ameweza kunielekeza vema mliko ili tuweze kuwatembelea na kununua vitabu na pia kujionea jinsi mnavyoitenda kazi ya shambani mwa Bwana. Naomba wote tuombeana amani upendo na tumaini pia nawaombea wagonjwa wote nimepata uponyaji kwa upande wangu ndiyo maana nawaombea wagonjwa wote ili kila atakayemwamini bwana Yesu Roho Mtakatifu akapate kuushusha mkono wake na kumponya. AMEN.
BWANA YESU KRISTO ASIFIWE SANA. Nimejaa furaha sana kusoma mafundisho haya ya wokovu, ni muhimu katika maisha ya mwanadamu hasa katika siku hizi ili watu waelewe maana halisi ya wokovu. Furaha yangu pia ni kuona kuwa kuna watumishi wa MUNGU wenye mzigo na maisha ya wengine kwa kufundisha njia ya kuelekea UZIMANI. Ujumbe uwafikie wale wote wenye uhitaji. Neno la Mungu halipiti bure lina kusudi maalumu, nawashauri watu wa Mungu tung’ang’anie baraka za Bwana ili tubarikiwe. Ahsante sana mtumishi kazi yako si bure. Mwenyezi Mungu aendelee kukutia nguvu ili kazi hii isonge mbele. UBARIKIWE
Bwana Yesu asifiwe,
Nikupongeze kwa elimu hii ya neno la Mungu,hii itasaidia wapendwa wapya na wale wenye shauku ya kuokoka lakini walikuwa hawajui nini maana ya neno kuokoka.
Asante,
Na Mungu wa amani awabariki
hi CHRISTINE I HAVE BEEN BLESSED MUCH BY YOUR SONG NIKUMBUKE A CTUALLY LET ALMIGHTY GOD USE YOU MIGHTLY TO ENCOURAGE MANY DISCOURAGED SOULS
MUNGU AWABARIKI KWA KAZI NJEMA HII YAKE MAANA SI MCHEZO KUKAA NAKUANDIKA YOTE HAYA,LKN NAOMBA UZIDI KUFAFANUA ZAIDI MAMBO MBALIMBALI AMBAYO YANATATANISHA WATU MFANO MABATIZDO,KUNENA KWA LUGHA,SABATO NK NA KADRI ROHO WA MUNGU ATAKAVYO KUONGOZA.
Hii tovuti ni ya maana sana katika kusaidia watu wenye uwelewa mdogo kuhusu Wokovu na dhumuni la Yesu Kristo. Mimi binafsi nimebarikiwa sana baada ya kusoma waraka huu wa Maana ya Wokovu. Kila ninaposoma aya moja, navutiwa kusoma aya inayofuata na hata kukaa vizuri ili nipate chakula cha kiroho vema zaidi. Ama kweli Mungi ni pendo kwani amewapa watumishi wake neema ya kufafanua maana kamili ya Wokovu ili kila atakayesoma na kuelewa awekwe huru.
Mungu awabariki kuanzia unyayo wa miguu yenu hata unywele mrefu wa vichwa vyenu. Amen
hakika Bwana ni mwenye kusifiwa maana yeye ndiye aliye weka ufaham na uweza wake kinywani mwako ktk kuandaa maana ya wokovu hakika bwana aendelee kukutumia sawasawa na mapenzi yake.ntaendelea kukuombea BWANA aendelee kukutumia.barikiwa na BWANA
Nimependa Mafundisho haya sana. Kwetu tuliookoka ni msaada hata kwa wengine. Nimeona ni vyema kama nitawafandisha wengine mapema iwezekanavyo.
ubarikiwe sana mwalimu
mtumishi wa mungu ubarikiwe kwa mafundusho yako mazuri.Mungu akulinde.
MTUMISHI WA MUNGU. MUNGU WANGU WA MBINGUNI AKUBARIKI MIMI NIKO MOSHI KILIMANJARO NAOMBA TUENDELEE KUWASILIANA.
First of all I would like to thank you Professor Mgisa for the wonderful work you have done about the whole concept about Salvation. Actually, there were alot of misconception about the real meaning of being saved. Another thing christians sometimes we do not take a time to read the Bible to understand what have been written concerning the Salvation. Also the misconception was even strike me for many years. But I decided to do a lot of readings and listening to Pastors and asked myself a lot of questions. As a baby christian, Salvation made me as a person who I was created. This blog has made me to deepen my understanding.
Thanks very much for your time.
RoseNyamizi
Mungu akubariki sana. Nafurahi sana kuona watu wanajua maana sahihi ya wokovu. Ukweli ni kwamba watu wengi wanaishi maisha ya shida sana kwa sababu hawajajua maana sahihi ya wokovu. Laiti wangejua maana sahihi ya neema hii ya wokovu wasingeteseka milele
Nakushukuru sana kwa somo la wokovu,Mungu akutie nguvu uendelee kumutegemea na uendelee na kazi hii ya kumubariki Mungu. Mimim binafsi nimebarikiwa sana na somo hili na limenitia nguvu katika safari yangu salama.
Mungu na azidi kukutia nguvu katika kazi ya BWANA Kazi yako ni njema sana na inanibariki mno hakika nimefurahi sana kupokea somo hili Mungu akubariki sana
nimefurahi sana kuona maneno ya Mungu ndani ya webset yenu,Nimepata mengi yatakayonijenga katika maisha ya kiroho,Naomba Muendelee kuweka neno la Mungu kwenye webset ili tuweze kusoms kila mara na kupata kitu kipya.Na ninaomba muwe mnanitumia neno la Bwana kwenye email yangu.Nashukuru na Bwana azidi kuwatia nguvu na afyaAmeni
Bwana yesu asfiwe ndugu ktka yesu kisto Nampenda sana yesu lakini nipo kwenye pito ambalo sielewi mwazo wala mwisho je watumishi wa mungu nifanye nini nishinde na kamwe sitaki kurudi nyuma hata siku moja naomba maombi yenu
shalom,
Mungu wangu wa mbinguni akubariki akutumie ktk kuwafumbua wenye macho lakini hawaoni na wenye masikio lakini hayasikii. akupa hekima na maarifa kama mfalme sulemani na moyo wa ushujaa kama Paulo na azidi kukufunulia mengine kama Yohana alivyotupwa kule patmo akafunuliwa, na watu walijua wamemweza kumbe makusudi ya Mungu na iwe hivyo. ubariki kwa somo nzuri la kututia moyo kwa ajili ya safari ya mbinguni. AMEN
IS ONCE SAVED FOREVER SAVED? OR…, ONE CAN LOOSE THEIR SALVATION?
WHY YES, WHY NO?
kati ya hao unaowadhani ni ndugu wa kiroho wamo wazinzi na waesharati, waabuduo sanamu, na wenye kutenda uwovu wa kila namna, kumbuka mpanzi alipanda mbegu njema shambani lakini baada ya mpanzi kuondoka shambani alikuja shetani na kuanza kupanda magugu shambani, hivyo simama kama wewe, amani ya Krito iamue maishani mwako, YESU anasema “asiyemchukia baba au mama yake kwaajili yangu hanistahili” katika shida ma jaribu ulilonalo YESU anakwenda kuonekana usikate tamaa, bali Mungu hapendi kujikweza kwako yeye anapenda roho zilizopondeka hivyo nyenyekea machoni pa BWANA, ukamtwike yeye fadhaha zako, hivyo upo uwezekano wa mtu kuupoteza wokovu wake, hasa kama mtu huyo nni ajenti wa shetani wapo maajenti wanaojielewa na wasiojielewa wanafanya kazi kubwa sana ya kuwaangusha wana wa MUNGU, wewe utawajuwa kwa matendo nyao, kuwa makini sana.
Question: “Can a Christian lose salvation?”
Answer: Before this question is answered, the term “Christian” must be defined. A “Christian” is not a person who has said a prayer, or walked down an aisle, or been raised in a Christian family. While each of these things can be a part of the Christian experience, they are not what “makes” a Christian. A Christian is a person who has, by faith, received and fully trusted in Jesus Christ as the only Savior (John 3:16; Acts 16:31; Ephesians 2:8-9).
So, with this definition in mind, can a Christian lose salvation? Perhaps the best way to answer this crucially important question is to examine what the Bible says occurs at salvation, and to study what losing salvation would therefore entail. Here are a few examples:
A Christian is a new creation. “Therefore, if anyone is in Christ, he is a new creation; the old has gone, the new has come!” (2 Corinthians 5:17). This verse speaks of a person becoming an entirely new creature as a result of being “in Christ.” For a Christian to lose salvation, the new creation would have to be canceled and reversed.
A Christian is redeemed. “For you know that it was not with perishable things such as silver or gold that you were redeemed from the empty way of life handed down to you from your forefathers, but with the precious blood of Christ, a lamb without blemish or defect” (1 Peter 1:18-19). The word “redeemed” refers to a purchase being made, a price being paid. For a Christian to lose salvation, God Himself would have to revoke His purchase that He paid for with the precious blood of Christ.
A Christian is justified. “Therefore, since we have been justified through faith, we have peace with God through our Lord Jesus Christ” (Romans 5:1). To “justify” means to “declare righteous.” All those who receive Jesus as Savior are “declared righteous” by God. For a Christian to lose salvation, God would have to go back on His Word and “un-declare” what He had previously declared.
A Christian is promised eternal life. “For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life” (John 3:16). Eternal life is a promise of eternity (forever) in heaven with God. God promises, “Believe and you will have eternal life.” For a Christian to lose salvation, eternal life would have to be taken away. If a Christian is promised to live forever, how then can God break this promise by taking away eternal life?
A Christian is guaranteed glorification. “And those he predestined, he also called; those he called, he also justified; those he justified, he also glorified” (Romans 8:30). As we learned in Romans 5:1, justification is declared at the moment of faith. According to Romans 8:30, glorification is guaranteed for all those whom God justifies. Glorification refers to a Christian receiving a perfect resurrection body in heaven. If a Christian can lose salvation, then Romans 8:30 is in error, because God could not guarantee glorification for all those whom He predestines, calls, and justifies.
Many more illustrations of what occurs at salvation could be shared. Even these few make it abundantly clear that a Christian cannot lose salvation. Most, if not all, of what the Bible says happens to us when we receive Jesus Christ as Savior would be invalidated if salvation could be lost. Salvation cannot be reversed. A Christian cannot be un-newly created. Redemption cannot be undone. Eternal life cannot be lost and still be considered eternal. If a Christian can lose salvation, God would have to go back on His Word and change His mind—two things that Scripture tells us God never does.
The most frequent objections to the belief that a Christian cannot lose salvation are 1) What about those who are Christians and continually live an immoral lifestyle? 2) What about those who are Christians but later reject the faith and deny Christ? The problem with these two objections is the phrase “who are Christians.” The Bible declares that a true Christian will not live a continually immoral lifestyle (1 John 3:6). The Bible declares that anyone who departs the faith is demonstrating that he never truly was a Christian (1 John 2:19). Therefore, neither objection is valid. Christians do not continually live immoral lifestyles, nor do they reject the faith and deny Christ. Such actions are proof that they were never redeemed.
No, a Christian cannot lose salvation. Nothing can separate a Christian from God’s love (Romans 8:38-39). Nothing can remove a Christian from God’s hand (John 10:28-29). God is both willing and able to guarantee and maintain the salvation He has given us. Jude 24-25, “To Him who is able to keep you from falling and to present you before his glorious presence without fault and with great joy—to the only God our Savior be glory, majesty, power and authority, through Jesus Christ our Lord, before all ages, now and forevermore! Amen.”
Question: “Once saved always saved?”
Answer: Once a person is saved are they always saved? When people come to know Christ as their Savior, they are brought into a relationship with God that guarantees their salvation as eternally secure. Numerous passages of Scripture declare this fact. (a) Romans 8:30 declares, “And those He predestined, He also called; those He called, He also justified; those He justified, He also glorified.” This verse tells us that from the moment God chooses us, it is as if we are glorified in His presence in heaven. There is nothing that can prevent a believer from one day being glorified because God has already purposed it in heaven. Once a person is justified, his salvation is guaranteed – he is as secure as if he is already glorified in heaven.
(b) Paul asks two crucial questions in Romans 8:33-34 “Who will bring any charge against those whom God has chosen? It is God who justifies. Who is he that condemns? Christ Jesus, who died more than that, who was raised to life – is at the right hand of God and is also interceding for us.” Who will bring a charge against God’s elect? No one will, because Christ is our advocate. Who will condemn us? No one will, because Christ, the One who died for us, is the one who condemns. We have both the advocate and judge as our Savior.
(c) Believers are born again (regenerated) when they believe (John 3:3; Titus 3:5). For a Christian to lose his salvation, he would have to be un-regenerated. The Bible gives no evidence that the new birth can be taken away. (d) The Holy Spirit indwells all believers (John 14:17; Romans 8:9) and baptizes all believers into the Body of Christ (1 Corinthians 12:13). For a believer to become unsaved, he would have to be “un-indwelt” and detached from the Body of Christ.
(e) John 3:15 states that whoever believes in Jesus Christ will “have eternal life.” If you believe in Christ today and have eternal life, but lose it tomorrow, then it was never “eternal” at all. Hence if you lose your salvation, the promises of eternal life in the Bible would be in error. (f) For the most conclusive argument, I think Scripture says it best itself, “For I am convinced that neither death nor life, neither angels nor demons, neither the present nor the future, nor any powers, neither height nor depth, nor anything else in all creation, will be able to separate us from the love of God that is in Christ Jesus our Lord” (Romans 8:38-39). Remember the same God who saved you is the same God who will keep you. Once we are saved we are always saved. Our salvation is most definitely eternally secure!
Question: “If our salvation is eternally secure, why does the Bible warn so strongly against apostasy?”
Answer: The reason the Bible warns us so strongly against apostasy is that true conversion is measured by visible fruit. When John the Baptist was baptizing people in the Jordan River, he warned those who thought they were righteous to “produce fruit in keeping with repentance” (Matthew 3:7). Jesus warned those who were listening to Him while He was giving the Sermon on the Mount that every tree can be known by its fruit (Matthew 7:16) and that every tree that does not bear good fruit will be cut down and thrown into the fire (Matthew 7:19).
The purpose behind these warnings is to counter what some people would call “easy-believism.” In other words, following Jesus is more than saying you are a Christian. Anyone can claim Christ as Savior, but those who are truly saved will bear visible fruit. Now, one may ask the question, “What is meant by fruit?” The clearest example of Christian fruit can be found in Galatians 5:22-23 where Paul describes the fruit of the Holy Spirit: love, joy, peace, patience, kindness, goodness, faithfulness, gentleness, and self-control. There are other types of Christian fruit (such as praise, winning souls for Christ), but this list provides us with a good summary of Christian attitudes. True believers will manifest these attitudes in their lives to an increasing degree as they progress in their Christian walk (2 Peter 1:5-8).
It is these true, fruit-bearing disciples who have the guarantee of eternal security, and they will persevere to the end. There are many Scriptures that bear this out. Romans 8:29-30 outlines the “golden chain” of salvation by pointing out that those who were foreknown by God were predestined, called, justified, and glorified—there is no loss along the way. Philippians 1:6 tells us that the work God began in us, He will also finish. Ephesians 1:13-14 teaches that God has sealed us with the Holy Spirit as a guarantee of our inheritance until we possess it. John 10:29 affirms that no one is able to take God’s sheep out of His hand. There are many other Scriptures that say the same thing—true believers are eternally secure in their salvation.
The passages warning against apostasy serve two primary purposes. First, they exhort true believers to make sure of their “calling and election.” Paul tells us in 2 Corinthians 13:5 to examine ourselves to see whether we are in the faith. If true believers are fruit-bearing followers of Jesus Christ, then we should be able to see the evidence of salvation. Christians bear fruit in varying degrees based on their level of obedience and their spiritual gifts, but all Christians bear fruit; and we should see the evidence of that upon self-examination.
There will be periods in a Christian’s life where there is no visible fruit. These would be times of sin and disobedience. What happens during these times of prolonged disobedience is that God removes from us the assurance of our salvation. That is why David prayed in Psalm 51 to restore to him the “joy of salvation” (Psalm 51:12). We lose the joy of our salvation when we live in sin. That is why the Bible tells us to “examine yourselves to see whether you are in the faith; test yourselves” (2 Corinthians 13:5). When a true Christian examines himself and sees no recent fruitfulness, it should lead to serious repentance and turning to God.
The second reason for the passages on apostasy is to point out apostates so that we may recognize them. An apostate is someone who abandons his religious faith. It is clear from the Bible that apostates are people who made professions of faith in Jesus Christ, but never genuinely received Him as Savior. Matthew 13:1-9 (the Parable of the Sower) illustrates this point perfectly. In that parable, a sower sows seed, symbolizing the Word of God, onto four types of soil: hard soil, rocky soil, weed-choked soil, and freshly tilled soil. These soils represent four types of responses to the gospel. The first one is pure rejection, whereas the other three represent various levels of acceptance. The rocky soil and the weed-choked soil represent people who initially respond favorably to the gospel, but when persecution comes (rocky soil) or the cares of the world bear down (weed-choked soil), they turn away. Jesus makes it clear with these two types of responses that, although they initially “accepted” the gospel, they never bore any fruit because the seed (of the gospel) never penetrated the soil of the heart. Only the fourth soil, which was “prepared” by God, was able to receive the seed and bear fruit. Again, Jesus says in the Sermon on the Mount, “Not everyone who says to me, ‘Lord, Lord,’ will enter the kingdom of heaven” (Matthew 7:21).
It may seem unusual for the Bible to warn against apostasy and at the same time say that a true believer will never apostatize. However, this is what Scripture says. First John 2:19 specifically states that those who apostatize are demonstrating that they were not true believers. The biblical warnings against apostasy, therefore, must be a warning to those who are “in the faith” without ever truly having received it. Scriptures such as Hebrews 6:4-6 and Hebrews 10:26-29 are warnings to “pretend” believers that they need to examine themselves and realize that if they are considering apostatizing, they are not truly saved. Matthew 7:22-23 indicates that those “pretend believers” whom God rejects are rejected not because of having lost faith, but because of the fact that God never knew them.
There are many people who are willing to identify with Jesus. Who doesn’t want eternal life and blessing? However, Jesus warns us to count the cost of discipleship (Luke 9:23-26, 14:25-33). True believers have counted those costs, whereas apostates have not. Apostates are people who, when they leave the faith, give evidence they were never saved in the first place (1 John 2:19). Apostasy is not a loss of salvation, but rather a demonstration that salvation was never truly possessed.
Question: “What is apostasy and how can I recognize it?”
Answer: Apostasy, from the Greek word being apostasia, means a defiance of an established system or authority; a rebellion; an abandonment or breach of faith. In the first century world, apostasy was a technical term for political revolt or defection. And just like in the first century, apostasy threatens the Body of Christ today.
The Bible warns about people like Arius (A.D. ca. 250 – 336), a Christian priest from Alexandria, Egypt, who was trained at Antioch in the early fourth century. About A.D. 318, Arius accused Bishop Alexander of Alexandria of subscribing to Sabellianism, a false teaching which asserted that the Father, Son, and Holy Spirit were merely roles or modes assumed by God at various times. Arius was determined to emphasize the oneness of God; however, he went too far in his teaching of God’s nature. Arius denied the Trinity and introduced what appeared on the surface to be an inconsequential difference between the Father and Son.
Arius argued that Jesus was not homoousios (of the same essence) as the Father, but was rather homoiousios (of similar essence). Only one Greek letter – the iota (i) – separated the two. Arius described his position in this manner: “The Father existed before the Son. There was a time when the Son did not exist. Therefore, the Son was created by the Father. Therefore, although the Son was the highest of all creatures, he was not of the essence of God.”
Arius was very clever and did his best to get the people on his side, even going so far as to compose little songs that taught his theology, which he tried to teach to everyone who would listen. His winsome nature and revered position as a preacher and one who lived in denial of himself contributed also to his cause.
With respect to apostasy, it is critical that all Christians understand two important things: (1) How to recognize apostasy and apostate teachers; (2) Why apostate teaching is so deadly.
The Forms of Apostasy
To fully identify and combat apostasy, it is important that Christians understand its various forms and the traits that categorize its doctrines and teachers. As to the forms of apostasy, there are two main types: (1) A falling away from key and true doctrines of the Bible into heretical teachings that proclaim to be ‘the real’ Christian doctrine; (2) A complete renunciation of the Christian faith, which results in a full abandonment of Christ.
Arius represents the first form of apostasy—a denial of key Christian truths (such as the divinity of Christ) that ultimately begins a downhill slide into a full departure of the faith, which is the second form of apostasy. It is important to understand that the second form almost always begins with the first. A heretical belief becomes a heretical teaching that splinters and grows until it pollutes all aspects of a person’s faith and then the full end goal of Satan is accomplished, which is a complete falling away from Christianity.
A recent example of this process is a 2010 study done by prominent atheist Daniel Dennett and Linda LaScola called “Preachers who are not Believers.” Dennett and LaScola’s work chronicles five different preachers who over time were presented with and accepted heretical teachings about Christianity and now have completely fallen away from the faith and are either pantheists or clandestine atheists. One of the most disturbing truths highlighted in the study is that these preachers maintain their position as pastors of Christian churches with their congregations being unaware of their leader’s true spiritual state.
The dangers of apostasy were warned about in the book of Jude, which serves as a handbook for understanding the characteristics of apostates like those chronicled in Dennett and LaScola’s study. Jude’s words are every bit as relevant for us today as they were when he penned them in the first century, so it is important we carefully read and understand them.
The Characteristics of Apostasy and Apostates
Jude was the half-brother of Jesus and a leader in the early Church. In his New Testament letter, he outlines how to recognize apostasy and strongly urges those in the body of Christ to contend earnestly for the faith (vs. 3). The Greek word translated “contend earnestly” is a compound verb from where we get the word “agonize.” It is in the present infinitive form, which means that the struggle will be continuous. In other words, Jude is telling us that there will be a constant fight against false teaching and that Christians should take it so seriously that we “agonize” over the fight in which we are engaged. Moreover, Jude makes it clear that every Christian is called to this fight, not just the local body’s leaders, so it is critical that all believers sharpen their discernment skills so that they can recognize and prevent apostasy in their midst.
After urging his readers to contend earnestly for the faith, Jude then highlights the reason: “For certain persons have crept in unnoticed, those who were long beforehand marked out for this condemnation, ungodly persons who turn the grace of our God into licentiousness and deny our only Master and Lord, Jesus Christ” (vs. 4). In this one verse, Jude provides Christians with three traits of apostasy and apostate teachers.
First, Jude says that apostasy can be subtle. Jude uses the word “crept” (found in no other book of the Bible) to describe the apostate’s entry into the church. In extra-biblical Greek the term describes the cunning craftiness of a lawyer who, through clever argumentation, infiltrated the minds of courtroom officials and corrupted their thinking. The word literally means slip in sideways; come in stealthily; sneak in; hard to detect. In other words, Jude says it is rare that apostasy begins in an overt and easily detectable manner. Instead, it looks a lot like Arius’ preaching and, for example, in a seemingly dismissive and nonchalant manner says that only a single letter differentiates its doctrine and the real teaching of the Christian faith.
Describing this aspect of apostasy and its underlying danger, A. W. Tozer wrote: “So skilled is error at imitating truth, that the two are constantly being mistaken for each another. It takes a sharp eye these days to know which brother is Cain and which is Abel.” The Apostle Paul also speaks to the outwardly pleasing behavior of apostates and their teaching when he says, “For such men are false apostles, deceitful workers, disguising themselves as apostles of Christ. No wonder, for even Satan disguises himself as an angel of light” (2 Corinthians 11:13-14). In other words, do not look for apostates to appear bad on the outside or speak dramatic words of heresy at the outset of their teaching. Rather than denying truth outright, apostates will twist it to fit their own agenda, but as pastor R. C. Lensky has noted, “The worst forms of wickedness consist in perversions of the truth.”
Second, Jude describes the apostates as “ungodly” and those who use God’s grace as a license to commit unrighteous acts. Beginning with “ungodly,” throughout his letter Jude describes eighteen unflattering traits of apostates so his readers can more easily identify them. Jude says the apostates are ungodly (vs. 4), morally perverted (vs. 4), denying Christ (vs. 4), ones who defile the flesh (vs. 8), rebellious (vs. 8), people who revile angels (vs. 8), who are ignorant about God (vs. 8), those who proclaim false visions (vs. 10), self-destructive (vs. 10), grumblers (vs. 16), fault finders (vs. 16), self-satisfying (vs. 16), people who use arrogant words and false flattery (vs. 16), mockers of God (vs. 18), those who cause divisions (vs. 19), worldly minded (vs. 19), and finally (and not surprisingly), devoid of the Spirit/unsaved (vs. 19).
Third, Jude says apostates “deny our only Master and Lord, Jesus Christ.” How do apostates do this? Paul tells us in his letter to Titus: “To the pure, all things are pure; but to those who are defiled and unbelieving, nothing is pure, but both their mind and their conscience are defiled. They profess to know God, but by their deeds they deny Him, being detestable and disobedient and worthless for any good deed” (Titus 1:15-16, emphasis added). Through their unrighteous behavior, the apostates show their true selves. Unlike an apostate, one who is a true believer is someone who has been delivered from sin to righteousness in Christ. With Paul, they ask the apostates who promote licentious behavior: “What shall we say then? Are we to continue in sin so that grace may increase? May it never be! How shall we who died to sin still live in it?” (Romans 6:1-2)
But the apostates’ false teaching also shows their true nature. Peter says: “But false prophets also arose among the people, just as there will also be false teachers among you, who will secretly introduce destructive heresies, even denying the Master who bought them, bringing swift destruction upon themselves” (2 Peter 2:1). Another aspect of true believers is that they have been delivered out of spiritual darkness into light (Ephesians 5:8) and therefore will not deny core truths of Scripture like Arius did with the divinity of Jesus.
Ultimately, the sign of an apostate is they eventually fall away and depart from the truth of God’s Word and His righteousness. The apostle John signifies this is a mark of a false believer: “They went out from us, but they were not really of us; for if they had been of us, they would have remained with us; but they went out, so that it would be shown that they all are not of us” (1 John 2:19).
Ideas Have Consequences
That God takes apostasy and false teaching seriously is evidenced by the fact that every New Testament book except Philemon contains warnings about false teaching. Why is this? Simply because ideas have consequences. Right thinking and its fruit produces goodness, whereas wrong thinking and its accompanying action results in undesired penalties. As an example, the 1970’s Cambodian killing fields were the product of the nihilistic worldview of Jean Paul Sartre and his teaching. The Khmer Rouge’s leader Pol Pot lived out Sartre’s philosophy toward the people in a clear and frightening way, which was articulated in this manner: “To keep you is no benefit. To destroy you is no loss.”
It should be remembered that Satan did not come at the first couple in the Garden with an external armament or supernatural weapon, but instead he came at them with an idea. And it was that idea that condemned them and the rest of humankind, with the only remedy being the sacrificial death of God’s Son.
The great tragedy is, whether knowingly or unknowingly, the apostate teacher dooms his unsuspecting followers. One of the most frightening verses in all of Scripture comes from the lips of Jesus. Speaking to His disciples about the religious leaders of His day, He said: “Let them alone; they are blind guides of the blind. And if a blind man guides a blind man, both will fall into a pit” (Matthew 15:14, emphasis added). This verse is alarming because Jesus affirms that it is not only the false teachers that go to destruction, but their disciples also follow them. Christian philosopher Soren Kierkegaard put it this way: “For it has never yet been known to fail that one fool, when he goes astray, takes several others with him.”
Conclusion
In A.D. 325, the Council of Nicea convened primarily to take up the issue of Arius and his teaching. Much to Arius’s dismay, the end result was his excommunication and a statement made in the Nicene Creed, which affirmed Christ’s divinity: “We believe in one God, the Father Almighty, maker of all things visible and invisible; and in one Lord Jesus Christ, the Son of God, the only-begotten of his Father, of the substance of the Father, God of God, Light of Light, very God of very God, begotten not made, being of one substance with the Father.”
Arius may have died centuries ago, but his spiritual children are still with us to this day in the form of cults like the Jehovah Witnesses and others who deny Christ’s true essence and person. Sadly, until Christ returns and every last spiritual enemy has been removed, tares such as these will be present among the wheat (Matthew 13:24-30). In fact, Scripture says apostasy will only get worse as Christ’s return approaches. “At that time [the latter days] many will fall away and will betray one another and hate one another” (Matthew 24:10). Paul echoes Jesus in his inspired writings as well. The Apostle told the Thessalonians that a great falling away would precede Christ’s second coming (2 Thessalonians 2:3) and that the end times would be characterized by tribulation and hollow religious charlatans: “But realize this, that in the last days difficult times will come. For men will be . . . holding to a form of godliness, although they have denied its power; Avoid such men as these” (2 Timothy 3:1-2, 5).
This being true, it is critical, now more than ever, that every believer pray for discernment, combat apostasy, and contend earnestly for the faith that has once and for all been delivered to the saints.
Ndugu Joseph,
Katika majibu uliyoweka nimejifunza mengi ambayo nilikuwa siyafahamu. Asante sana.
Mungu wa mbinguni akuzidishe!
Asante Ndugu John,
Glory to God!
Joseph may the Almight God bless you for a good explanation on “apostacy” and its effects on the body of christ.
This is great, bro. Joseph. Many would reserve such an exposition to a paid-for paper, but you’ve put it here all for free to whoever desires – this is a great christian spirit and a great christian service. Receive blessings from our God
Mungu azid kuwapa maono zaidi namna ya kuwavuta watu kwake.
Mpendwa Mungu Asifiwe, Nashukuru kwa swali zuri kwa ufupi Wokovu ni kipawa
Shaloom mtumishi wa BWANA ndugu ASANTERABI.Nakukumbuka sana rafiki mzuri katika Bwana.
NDUGU KATKA KRISTO NASHUKURU SANA KWA MADA YAKO NZURI SANA JUU YA WOKOVU,KWAKWELI KUOKOKA NI MAISHA MAPYA KABISA KWA MTU YEYOTE AKIMPOKEA YESU.1KORINTHO 5:17,i.e,”Mtu akiwa ndani ya Yesu amekuwa kiumbe kipya”. Ubarikiwe sana mtumishi wa Mungu kwa kazi yako njema Amen!
NASHUKURU MWL AGGREY ENDELEA KUOMBEA UCHAGUZI MKUU
Nashukuru sana kupata maelezo yaliyopo katika website ya Radio Safina kwa vile yatanisaidia katika WOKOVU wangu ambao ni mchanga. Napenda kusema kuwa kwa YESU hakuna wokovu mchanga maana hata katika Yeremia 1:4-10 Mungu alimwambia Yeremia nimekuweka kuwa nabii na tangu tumboni mwa mama yako nilikutakasa. Yeremia alijibu mbona mimi ni mchanga. Lakini Mungu alimwambia usiwaogope hao na wala usiseme mimi ni mtoto kwa maana kila nitakayekutuma kwake utasema lile nitakalokuamuru. Mimi niko pamoja nawe nikuokoe.Mungu alichukua Mkono wake akaugusa kinywa chake akatia maneno yake kinywani mwake. Aliendelea kumwambia tizama leo nimekuweka kuwa juu ya mataifa na falme, ili kung’oa, kubomoa, kuharibu na kuangamiza ili kujenga na kupanda.
Mungu aliyeniokoa yuko pamoja nami mahali popote na saa yoyote, hivyo nina haki ya kusema kwamba mimi sio mchanga/mtoto kwa sababu anao uwezo wa kuweka maneno yake kinywani mwangu nikawa na uwezo wa kun’goa, kubomoa, kuharibu na kuangamiza pia kujenga na kupanda.
Namshukuru Mungu, ameyabadilisha maisha yangu, ninamuona Mungu akiendelea kunipigania, kunitetea.
Naomba muendelee kuniombea ili nisimame na niweze kuomba.
Mary Peter
Shalom,
Nashukuru sana kwa mafundisho yako mazuri yaani si kwa wale ambao wanataka kuhokoka tu la hasha hata kama una miaka kwenye uhokovu mafundisho yako yanagusa kabisa na unajitambua kupitia mafundisho haya na kujua ni njia ipi ulipo mpaka sasa.
Mungu ni mwema na ni kusudi lake limetimia.
Bwana Yesu asifiwe sana.
Ninamshukuru Mungu sana kwa ajili ya mafunuo haya ya siri za ufalme wa Mungu anazotufunulia kupitia mtumishi wake Mgisa Mtebe. Kwa kweli mafundisho ya mwalimu huyu yamenisogeza hatua zaidi katika kuutafuta uso wa Mungu. Naomba Bwana aendelee kumpa mafunuo zaid kwa ajili ya kuliponya kanisa katika nyakati hizi za mwisho. 2Nya 7:14. Mungu ambariki sana mtumishi wake na kumtunza.
Thanx so much!
mbarikiwe kwa somo zuri sana lina fundisha hata kama hujui chochote baada ya kusoma unajikuta unakuwa mwalimu
i thanks god a lot for blessing teaching from mwakasege it change my life totally.
Thank you for your teaching. I’ve now changed my life, I now living and serving as our God, Lord Jesus wants.
Amen
mtu aliye okoka , unapo muona tu anaonekana kuwa ndanimwaki munakitu.
neno wokovu ni neno ambalo halija wahi kufuchikiwa. sababu kama alivyo imba mwenzi wetu Bonyi mwayitege alisema kwamba utembeyapo tu watakutambuwa ikiwa wewe unao huwo .ndo sababu nami nina shuhudiya kwamba wokovu hauna mamabo yaku uliza uliza hapa .
aksanti na Mungu utuzidishiye kuwa nao pia kuwa ndani yahuo (wokovu).
bwana yesu asifiwe, nawashukuru sana kwa mada hii nzuri, imenielimsha vya kutosha na nimeelewa kabisa, Mungu awabariki sana muendelee kutufundisha sisi kwa njia hii.
Oh God is very great.I was in a situation where by I didnt understand wht to do in my problems.After reading a very long lesson about salvation I got many answers for my unaswered questions.I was blessed so much from the lessons provided.
I hope I will review to get more understanding.
May god bless you for your time to prepare that long srcipture.
Rose
KUOKOKA
Ni kuwa na imani isiyo na mbadala juu ya BWANA YESU.
WOKOVU
- Nini maana ya wokovu
- Kwanini wokovu
- Nani ameleta wokovu
- Wokovu unapokelewa kwa namna gani
- Nini uthibitisho wa wokovu
- Namna ya kutembea katika wokovu
- wokovu katika maisha ya ndani
- wokovu katika maisha ya nje
- wokovu unatunzwaje
- Wokovu unaharibiwaje
>Maeneo matano muhimu ya nguvu za mwamini
- Maombi
- Neno
- Roho mtakatifu
- Ushuhudiaji
- Sadaka na mafungu ya kumi
>Uhusiano wa wokovu na karama za rohoni
>Uhusiano wa wokovu na kukua kiroho
>Kilele cha wokovu (Tumaini lenye Baraka)
Utangulizi
Wokovu unahusisha hali ya usalama, uhifadhi, uponyi au kutoa kitu kutoka katika hali isiyo na usalama, mzuri na kupeleka katika hali iliyo nzuri au bora zaidi.
Katika maisha ya Mkristo wokovu ni muhimili wa maisha yake kwa sababu ya historia ya mwanadamu.
Inafahamika kuwa mwanadamu aliumbwa katika hali ya ukamilifu, na isiyokuwa na dhambi, Mwanzo1:26. Mungu alimkusudia mwanadamu aishi maisha yaliyojaa hali ya utawala ndani yake. Alimtaka mwanadamu awe shirika naye katika tabia ya Mungu.
Mwanadamu huyo alikusudiwa aishi sawasawa na neno la Mungu. Kwasababu neno la Mungu ni kile alichokisema/anachokisema Mungu juu yako. Wanadamu wa kwanza Adam na Eva wakalisikiliza neno la Shetani na kulihalifu neno la Bwana. Kosa walilolifanya Adam na Eva ndilo linaloendelea kutendwa siku za leo kwa wanadamu kushindwa kuisikiliza sauti ya Mungu wao.
Anguko la mwanadamu lilileta kifo cha kiroho na kimwili. (maana ya kifo ni kutengana)
Mwili na roho vikitengana ni kifo cha kimwili
Roho na Mungu vikitengana ni kifo cha kiroho
Mwanzo 3:15 Mungu anatoa unabii wa wokovu kwa mwanadamu aliyepotea.
Ifahamike kuwa baada ya mwanadamu kuanguka alianza kutafuta njia mbalimbali za kumrudia Mungu ambazo hazikuzaa matunda. Jambo ambalo lilizaa dini mbalimbali.
Dini – Ni mpango wa wanadamu kumtafuta Mungu
Wokovu- Ni mpango wa Mungu kuwatafuta wanadamu Yoh 3:16
(1) Somo
Wokovu ni tukio linalohusisha mwanadamu kutambua kuwa amemwacha Mungu na kutubia uasi huo kwa toba ya kweli, ambayo itazaa badiliko ndani yake, litakalosababisha asirudi tena katika maisha ya kale na kumwezesha kufikia kilele cha nia ya Mungu, yaani kuishi na Mungu milele. Yoh. 3:8a
Kutokumtii Mungu huzaa kitu kinachoitwa dhambi, na dhambi ni uasi dhidi ya Mungu. Ni kushambulia sehemu ya utakatifu na heshima ya Mungu, dhambi inapozoeleka huitwa uovu. Uovu unapomfikia Mungu huzaa ghadhabu ya Mungu, na ghadhabu ya Mungu huondolewa kwa malipizi.
Wanadamu wengi hujiuliza kwanini Mungu asingetangaza msamaha bure kwa watu wote, bila hata kazi ya msalaba? au kwanini Yesu amekuja na watu watubu?
Mungu ana sifa nyingi lakini katika hili ana sifa za kipekee tatu zinazomfanya asishawishike kumwesabia mtu mwenye hatia kuwa hana hatia Kutoka 34:6-7 Rumi 2:4-16
(1) Mungu ni mtakatifu
Kwa asili anapigana na kila kitu kinachoitwa dhambi
Dhambi ni kushambulia utakatifu wa Mungu na heshima yake
Kwahiyo mtu yeyote anapofanya dhambi anajihusisha na kutengeneza silaha ya kupambana na uungu wa Mungu.
Pia wanadamu wanapofanya dhambi wanakuwa ni waamuzi wa nafsi zao wenyewe. kwasababu hiyo ni miungu/ bwana wa nafsi zao.
Kwa maana nyingine dhambi ni kukomesha utawala wa Mungu katika maisha ya mtu. Kwa hiyo kuwaachilia wanadamu wote kuendelea kufanya dhambi ni Mungu kujitangaza kuwa yeye si Mungu kati ya wanadamu. Na Mungu ana wivu na kila kitu kinachojiinua kutaka kuchukua nafasi yake. Kwahiyo lazima uovu ukichipua kwa wakati wake uadhibiwe. Ili Mungu abaki kuwa yote katika yote (Absolute controller)
II. Mungu ni mwenye haki
Haki ya Mungu inamadai mbele za Mungu kumtaka atimize Neno lake sawasawa na alivyosema. Inakumbusha Mungu kutoa Malipo kwa kadri ya matendo. Zab 34:15-16. Kutokutimiza neno lake ni kumfanya kuwa muongo na kigeugeu. Na kamwe hatakuwa hivyo. Ikiwa amesema mshahara wa dhambi mauti. akiwatangazia Adamu na Eva kuwa siku mtakayo kula matunda ya mti wa katikati kufa mtakufa hakika. Haki ya Mungu inasimama kudai kutimizwa.
“Ogopa sana Mungu anaposimama kwenye haki yake” Hakikisha muda huo upo upande wake maana ni hatari.
III. Mungu ni mwenye rehema
Laiti Mungu asingelikuwa na rehema maisha ya mwanadamu yangaliishia bustani ya Edeni. Kwa mujibu wa aya mbili zilizotangulia mwanaamu hakustahili kuishi, lakini ajabu ni kuwa rehema za Mungu zinafanya kazi ya kumshikilia Mungu asiachilie ghadhabu yake kwa upesi, Hapa ndipo tunapoongezewa muda wa sisi kutubu Zab 100:5.
N:B. Rehema za Mungu zinakikomo. ilikuruhusu Mungu kujilipizia kisasi (Usichezee kipindi cha rehema).
Sababu hizi zinatufanya tuone kuwa kumbe asili na umbile la dhambi ya mwanadamu ilikuwa inatangaza mauti yake.
Ndipo tunapopata Yoh 3:16 upendo wa Mungu wa agape. Aliupenda ulimwengu hali ukiwa umejaa dhambi na uovu. Akaandaa mipango mwenyewe udhubuti wa wokovu.
Kosa la Adamu na Eva lilizaa kizazi kilichoanza kuwa na asili ya dhambi (mtaji wa dhambi) yaani mtu akiwekwa katika mazingira ya dhambi anaweza akafanya dhambi. Yesu anakuja ndani ya mtu kuleta dawa ya kuondoa asili ya kuasi/ kipingana na Mungu ndani ya Mwanadamu.
NB Kuna imani zinasema tunazaliwa na dhambi ya asili lakini imani yetu ya kipentekoste inasema tunazaliwa na asili ya dhambi. Yaani dhambi haijafanywa na sisi. Ila tumepokea asili ya dhambi ambayo kwahiyo inatoa mtaji wa kufanya dhambi popote panaporuhusu.
Sasa: Yesu ni mdhamini wa agano jipya
Sifa za mwokozi
(I) Alitakiwa kuwa mtu wa karibu na mwanadamu, mwenye kuwajua na kuwaelewa wanadamu (Yesu akazaliwa kama mtu, akachukua mwili)
(II) Alitakiwa awe na uwezo wa kulipa gharama. (Alitoa damu isiyo na hatia)
(III) Alitakiwa kujitoa kwa hiari (nitume mimi Bwana)
Wokovu ulianzishwa na Mungu Baba ukaletwa kwetu na Mungu mwana na unapokelewa kwa Roho.
Ni neema ambayo inapatikana pasipo mtu kuitabikia
Kwa hali ambayo mwanadamu alikuwa nayo haiwezekani kujiokoa mwenyewe kwa jinsi yoyote.
Fikiri hivi
(i) Mwanadamu mwenye Mungu
- Moyo umejaa Mungu
- Anatembea nuruni
- Sauti ya Mungu ikisemwa, ndani yake yumo Mungu (kunatengeneza mazingira ya makubaliano)
(ii) Mwanadamu Mwenye dhambi
- Moyo umekaliwa na shetani
- Anatembea gizani
- Sauti ya Mungu ikisema, ndani yake yumo shetani. Hakuna mzingira ya makubaliano kati ya Sauti ya Mungu na moyo wake.
Ndiyo Maana inahitajika aliyejuu ya yote mwenyewe aingilie nyumba hii amkamate mwenye umiliki amtoe nje, aweke makazi yake (Mungu) ndipo mwanadamu huyu aanze kusikiliza Mungu anasema nini kwa ajili ya maisha yake
Tukio hili linatupa kuamini tumeokolewa bure kwa neema hakuna kazi tuliyoifanya. Ila deni yetu yote Yesu aliilipa Msalabani Isaya 53. La muhimu kwetu ni maamuzi ya kuamua ama kuokoka au kutookoka ila huruma na rehema za Mungu ni tele.
NB: huu ni ufupisho, inahitaji maelezo mapana kujua nini kmefanyika unapookoka ili usirudi tena ulikotoka.
Wokovu unapokelewa kwa toba inayohusisha
- Kumwamini Yesu ya kuwa ndiye njia pekee ya Mungu kuwakomboa wanadamu Rumi 10:9
- Toba- ni huzuni ya kweli juu ya dhambi na juhudi za makusudi ya kutokutenda dhambi hiyo tena.
- Ni kuichukia dhambi kiasi cha kuiacha
- Ukiona mtu ametubu kisha anarudi rudia yale ya zamani, anakuwa hajazaa matunda yapatanayo na toba.
- Wokovu pia unahusisha kutambua nini kimefanyika katika maisha ya mtu (kuzijua haki zake ili asiishi tena kama mtumwa kwenye nchi yake mwenyewe.
- Wokovu unahusisha kuhamishwa kutoka kwenye ulimwengu wa giza kuingia kwenye ulimwengu wa nuru
- Kanuni za ulimwengu huu ni kila mtu kuishi chini ya utawala wa Bwana wake (Utawala wa Nuru ni neno la Mungu, utawala wa giza ni neno la Ibilisi (uovu)
- Asije mtu akafanya dhambi na kuhisi kuwa ufalme wa Mungu utamhifadhi (It will never happen) Efeso 2:1
Tunapookoka roho zetu zinarudishiwa uhusiano zilioupoteza mbele za Mungu
Lakini nafsi zetu kwakuwa ziliharibiwa na utu wa kale tunazigeuza kwa neno la Mungu. kweli inatufungua kila iitwapo leo.
Lakini miili yetu tuaitoa dhabihu na kuisulibisha ikubaliane na kweli. Maana mara zote mwili hautatupa ushirikiano sana lakini tunaisulubisha imfuate Kristo.
Nafsi ni kiungo kati ya roho na mwili ila inategemea sana nguvu iliyopo katika roho au mwili ili nafsi ifanye kazi.nafsi inaendeswa na Maamuzi yanayofanyika ama ktk mwili au roho
Baada ya kukiri wokovu anahusisha yale yote tunayoyafanya mpaka tunaingia mbinguni
- Hivyo basi tunaweza tukagawanya wokovu katika makundi ya wakati (yaani nyakati tatu) za misingi katika maisha yako.uliopita, uliopo, ujao.
Yaani – ulifanya nini (ulikiri)
- Unafanya nini (unaishi maisha matakatifu)
- Utapata nini (Nitakwenda kukaa na Bwana milele)
Inashauriwa: Ni vyema sana ukasoma vizuri kitabu cha Yohana na kisha warumi
Vitabu hivi vinamjengo mzuri wa kimafundisho ya kukua katika wokovu
Daudi katika roho anayoona hayo katika Zab 32 na kukiri
“Heri aliyesamehewa makosa yake ……..” Luka 1:73
2kor 5:17 yakale yote yemepita
Baada ya kuokoka tunaambiwa kuwa ya kale yote yemepita
- Hakuna nguvu ya dhambi juu yetu tena
- Magonjwa hayana nafasi
- Laana haziwezi kutufuatilia kabisa
NB: Kunabaadhi ya imani zinazosema umeokoka lakini hauja kombolewa. Hivyo kujihusisha na kuvunja laana.
Elewa Hivi – Kazi ya msalaba ilitosha kutufanyia matukio yote mawili
Laana ililetwa na dhambi
Magonjwa yaliletwa na dhambi.
Alichokifanya Yesu ni hiki
(i) Kulipa Deni – Ndiko kukombolewa
(ii) Kutuhamisha – Ndiko kuokoka
Kwa hiyo haya ni matukio mawili yanayofanyika mara moja
Kumwambia mtu umeokoka bali huja kombolewa ni kusema tumekutoa jela lakini bado unadaiwa madeni laazima uyalipe.
Sisi tunaamini deni ya dhambi ilimalizikia msalabani Yesu akitangaza imekwisha kazi ya kumuokoa mwanadamu
- Kinachobaki baada ya kuokoka ni mtu kuifahamu kweli, na Yesu akatuhakikishia ya kuwa mtaijua kweli na hiyo kweli itawaweka huru.
Kwahiyo basi.
Maeneo matano muhimu ya nguvu za mwamini
Ni muhimu mkristo akayajua haya kwasababu ndipo hasa chemchem za nguvu na uhai wa kiroho na hapa ndipo watu wanapopaharibu na ghafla kuonekana hawapo kiroho.
I: MAOMBI
Ni mazungumzo baina ya mwanadamu na Mungu. Ni sehemu ya ibada ambapo mwanadamu anatulia chini ya uwepo wa Mungu na kuzungumza naye.
NB kunatatizo kubwa hapa katika nyakati zetu ambapo maombi yamekuwa ni one way traffic. Ni tukio la watu kumweleza Mungu bila kujua Mungu ananena nini.
Zingatia yafuatayo (What are the demands for effective prayer)
- Maombi yanahitaji utakatifu
- Maombi yanahitaji muda
- Maombi yanahitaji kujitoa (Devotion)
- Maombi yanahitaji muendelezo (hayana cut is a continuation)
- Maombi yanahitaji utulivu (Uhusika wako)
- Maombi yanahitaji umakini
- Maombi yanahitaji ulijue neno la Mungu vizuri
- Maombi yanahitaji imani
- Maombi yanahitaji uhakika juu ya uwepo wa Mungu (kuna watu wanaomba kama watu wapiga kelele tu maana uwepo wa Mungu haupo hapo). Yaani hawajatengeneza mazingira ya kukutana na Mungu. Maana Mungu hashuki popote, hashawishiwi ila anaguswa.
Jumla ya hayo na mengine mengi yamezaa maneno mengi lakini matokeo hafifu.
(NB somo hili la maombi ni somo pana linahitaji nafasi yake).
Lakini tunaweza kuyagawa katika maeneo mengi
Prayer at first level – Maombi ya kusikizisha dua, matatizo maombezi na kila aina ya kitu kilichopo katika fahamu.
Prayer at the second level –Maombi ya mtu aliyekomaa kiroho ya kutafuta kukaa na Bwana. Kujenga fellowship, kuutafakari ukuu wa Mungu uwepo na nguvu zake
(Kumbuka Mungu ………… kwenye maombi primarily objective sio, kusikiliza shida zetu maana anazijua zaidi kuliko sisi.
II. NENO
Neno ndilo kiongozi wa maisha ya mkristo
- Utaomba sawasawa na neno
- Utafunguliwa kadri unavyolijua neno
- Utaishi neno
- Utasema neno ili ufanikiwe
Popote Mungu anapotaka kufanya kazi atalituma Neno.Alipotaka kuwakomboa wanadamu alilituma neno kutoka mbinguni likafanyika mwili, na Neno ni Yesu mwenyewe na ndiyo maana maandiko yanasema yeye aliyemwamini mwana anao uzima.Refer maelezo ya mwanzo.
III.ROHO MTAKATIFU
Mdo 1;8
Kama tulivyoona wokovu ukiandaliwa na Baba ukiletwa kwetu na Mwana ukipokelewa kwetu kwa Roho
Na ni vyema mkristo akaielewa personality(Unafsi Wa Roho Mt) ya Roho mt ili asipate shida wakati wa kuomba ujazo wa Roho Mt na namna ya kuishi naye.Wengi wamemchukulia Roho mt kama kitu cha namna Fulani ambacho baada ya kuomba kitakuja na kuingia kwa kushtukiza au nguvu Fulani. Lakini msingi ni kuwa Roho mt ni Mungu, ni zaidi ya nguvu, si kitu bali ni Mungu mwenyewe na uwepo wake akitembea na mtu.Kujua personality yaRoho mt kutakusaidia kuelewa kuwa Roho Mt anahisia, akihitajiwa, akipendwa anajua.Na pia akitendewa jeuri ana mwitikio.Hivyo Mungu hawezi kukuacha utaabike anaitaji tuu uelewa wako ili utembee vizuri na Roho mt.
Nani anampokea
-Aliyeokoka,
-Mwenye imani
-kiu
-Shauku
-Uvumilivu na utulivu
Ukimjua vizuri tamaa yako itakuwa sio aingie kwa kiwango gani bali ujitoe kwake kwa kiwango gani ili akumiliki.
IV.USHUHUDIAJI
Ushuhudiaji ni hali ya kuwaeleza wengine kile Mungu alichokifanya ktk maisha. Angalia mfano wa mwanamke msamaria alizunguka kijiji kizima akisema yale aliyeyaona.Hakuna mtu aliyetendewa jambo na Mungu ambaye aliweza kunyamaza kimya.Lakini zaidi ushuhudiaji ni agizo kuu math 28;19 Marko 16;15
Kutoshuhudia ni dhambi kama zilivyonyingine.
Umuhimu wa kushuhudia
-Ni changamoto ya kuishi maisha matakatifu
-Ni kuendelea kushiriki kazi ya upatanishi kati ya Mungu na wanadamu, huduma ambayo tumepewa 2kor 5;19
-ni kuendelea kuujenga ufalme wa Mungu duniani
V.SADAKA NA MAFUNGU YA
KUMI
Katika kukamilisha ibada, sadaka ni jambo la Muhimu na ni agizo la Mungu mwenyewe kuwa tusiingie nyumbani mwake mikono mitupu, tunaheshimu kuwa Mungu ndiye atupaye nguvu za kupata mali na tupo tayari kumtumikia Mungu kwa nguvu zetu zote, akili zetu zote lakini pia kwa mioyo yetu.Hatumpi Mungu kwasababu anahitaji, au kama tusipotoa tutakwamisha kazi yake.Huo ni mtizamo mbaya ambao ndani yake hauna Baraka.
Nitoe namna gani
-Kwa moyo wa uhiari na kupenda
-Kutoa kitu kisicho kidhaifu kulingana na uwezo wako
-Kutoa kwa nia njema na safi
-Kutoa kitu ambacho kitaugusa moyo wa Mungu
-Kutotoa kwasababu ni kawaida kutoa katika muda na sehemu hiyo lakini kwasababu ni ibada.
Fungu la kumi
Ni sehemu ya kumi ya kila tunachokipata, Ni agizo la Mungu kuwa sehemu hiyo ni takatifu kwaajili yake.Hii ni laazima kuwa makini nayo kwasababu tangu zamani hakuna mtu aliyekula kitu kitakatifu akabaki salama.Na sehemu hii inatolewa ktk kanisa lako linalokulea (local church)
Nb
Kifupi wokovu unasura ya nje na ndani
Nje – Ni namna unavyoenenda
Watu wanavyokusoma/ au unavyosomeka (kumbuka sisi ni Barua ya kusomwa na watu wote)
Ndani – Ni namna ya wokovu kiuhusiano na Mungu
Namna Mungu anavyokusoma/ unavyosomeka. (Maana yeye huichunguza mioyo na kuvipima ..)
Sasa kuna kanuni moja ya kufanikiwa kiroho kama tunataka kuendelea kiroho. Nje yetu ya kiroho lazima ifanane sana na ndani yetu ya kiroho.
Namna tunavyojihudhurisha mbele za Mungu sawasawa na tunavyoonekana nje.
Mfano. Mafarisayo waliikosea kanuni hii wakasubstitute external outlook na viwango vya kiroho vya ndani
Wakaingiza maisha mema nje lakini ndani yao hawana Mungu.
Wokovu ni kuishi maisha halisi sio kuigiza uhalisi
Wokovu ni kufanya kwelikweli sio usanii
Mungu anatuchunguza pande zote mbili yaani undani wetu na unje wetu
Ndani yetu anatakiwa kuumbika kristo ambaye atachonua na kuonekana nje
Wokovu unaharibiwaje
Kwa mtu kuanza kuonyesha tabia zisizokuwa na uzima /za kimungu
(i) Kutokuitii kweli kwa bidii
(ii) Kuanza kuvutiwa na mambo ya dunia
(iii) Kuona mambo ya kimungu ni mzigo mzito
(iv) Kuanza kufuatisha aina ya maisha ya watu wa dunia hii
(v) Kushindwa kulinda fahamu zake na kuruhusu uchafu ambapo unamnyima Mungu kutembea naye
(vi) Kutokuwa na bidii katika yale anayofahamu kuhusu Mungu
(vii) Kuanza kupata uwezo wa kutetea mambo ya kipagani na kutaka kuyahalalisha kuwa ni ya Kimungu kwa sababu yeye anayafanya.
(viii) Kuigiza wokovu – nguvu za Mungu
utakatifu etc.
Na mengineyo mengi yafananayo na hayo
Uhusiano wa wokovu/ karama za rohoni na kukua kiroho
Baada ya mtu kuokoka anaweza kupokea karama za rohoni na kuanza kutumika kwa nguvu pengine kuliko hata waliomtangulia kwa kadri ya kiu, shauku kuu na kujitoa. Lakini haimaanishi kuwa amekua kiroho. Kukua kiroho kunahusisha tabia za kristo kuanza kuonekana katika maisha ya mwamini.
Tunda la Roho Galatia 5 kujifunua katikati ya watu. Unaweza ukatumiwa kwa karama nyingi lakini nyenyekea chini ufundishwe yaani ukubali kufundishika ili uukulie wokovu vyema na kuwa chombo kinachofaa kwa kila kazi njema.
Wengi wamezolewa katika eneo hili kwa kuinuka kinyume na watu walio walea kiroho.
Kanisa la Wakoritho lilikuwa na tatizo hilo. Walisisitiza sana karama za rohoni kuliko tunda la roho. Walikuwa ni watu waliokiroho kwa utendaji wa kazi za Mungu lakini waajabu katika maisha yao ya kawaida.
Paulo hakuwakataza kuwa na karama za rohoni lakini anawaonya kuwa mambo haya yanafanyika kwa utaratibu.
KILELE CHA WOKOVU
Baada ya kukiri na kuishi maisha safi tunatarajia siku moja Bwana wetu atakuja kutuchukua ile Yeye alipo sisi nasi tuwe hapo.Biblia inasema kila aliye na matumaini haya ktk yeye hujitakasa.uf 22;20
Heri Yule aliyealikwa katika karamu ya harusi ya Mwana kondoo.
source: CASFETA-TAYOMI MLIMANI BRANCH –DOCTRINE COMMITTEE
curently watu wengi hawajui maana halisi ya wokovu! wengi wameufanya wokovu kuwa ni fashion ya maisha, wengine hata wanadiriki kusema wameokoka huku matendo yao hayadhihirishi kuwa wameokoka. inasikitisha sana coz inazuia hata wengine walioko nje washindwe kuukubali wokovu na kudiriki hata kuutukana. wengi tumeipokea neema ya Mungu bure na tunaichezea 2kor 6:1. Mungu atusaidie sana tuweze kuushika kwa uaminifu huu WOKOVU ambao uligharimikiwa kwa gharama zisizolipika za MUNGU kumtoa mwanawe wa pekee kuimwaga damu yake pale msalabani!
WITO WANGU KWA WALIOOKOKA WOTE
Sisi je! tutapataje kupona ,tusipojali wokovu mkuu namna hii?….Ebrania 2:3
Do you Know Jesus?
Do you want to commit your life to God?
Do you want to experience “TRUE” peace in your life?
You can begin a “NEW LIFE IN CHRIST JESUS” Today.
I invite you to make Jesus Christ the Lord of your life by praying this prayer
Pray this prayer
Say, “O Lord God, I come to you in the Name of Jesus Christ. I confess that I am a sinner in need of forgiveness. This very moment; I receive your free gift of forgiveness of all of my sins. Your Word says in the book of Acts 2:21″…whosoever shall call on the name of the Lord shall be saved”. I ask Jesus to come into my heart to be the Lord of my life.
I receive eternal life into my spirit and according to Romans 10:9, which says, “That if I shalt confess with my mouth that Jesus is Lord, and shall believe in my heart that God has raised Him from the dead, I shall be saved,”
I declare that I am saved; I am born-again; I am a child of God! I now have Jesus Christ living in me, and greater is He that is in me than he that is in the world! (1 John4:4).
I now walk in the awareness of my new life in Christ Jesus. Hallelujah!”
Congratulations! You are now a child of God. Send me your name and the date which you prayed this prayer and gave your life to Jesus Christ so that I may rejoice with you and pray for you as you begin your “New Life” in Christ Jesus.
Have a blessing for good teachings i learnt a lot,feeling well opened and not lionliness in christ lord keep on preparing sermons like this so then we new teacher we would use to teach new entry in christ to know the good foundations in christian faith likely this particularly in this end days of age.GOD WILL PAY YOU 4 SURE KEEP ON, WELL DONE!! Michael Japhari IRINGA
mafundisho mazuri mno Mungu aendlee kukutumia mwalimu akupe na mafunuo mengine .Ubarikiwe
NAITWA CATHERINE .A.KUYONGA
NAPATA FARAJA SANA NA NINABARIKIWA SANA NINAPOSOMA MAFUNDISHO YAKO
KWA KUPITIA WEB SITE HII NAAMINI MUNGU ATANIWEZESHA KATIKA MALENGO NA NITAENDELEA KUFUATA MAFUNDISHO HAYA NA KUKUA KUIMARIKA KATIKA KRISTO.
Kwakuwa umelishika neno langu na subira yangu , mimi nami nitakulinda utoke katika saa kujaribiwa iliyotayari kuujilia ulimwengu wote kuwajaribu wakaao juu ya nchi .
Naja upesi shika sana ulicho nacho , asije mtu ayitwaa taji yako
Pastor Selestino
Ukiamini toka moyoni, na ukamkiri Bwana kwa kinywa, utaokoka!
nimefarijika sana na somo lako mwalimu kuhusu wokovu. kwa kweli Mungu akutie nguvu na akubariki sana. nitaendelea kufuatilia ulivotufundisha ili niweze kufika mbinguni.
Very good article, Blog inaweka mambo mazuri. Cheers.
Kwa kweli Mungu wetu ni mkuu sana na ni mwenye upendo wa ajabu mno kwetu. Sikufahamu kabisa kwamba ndani ya simu yangu hii kuna habari nzuri za uzima wa milele kama hizi, “May God bless you all for what a wonderful work you have done for us”. Naamini kabisa nikizingatia mafundisho haya muhimu nami nitakuwa si mwelewa tu wa la Neno la Mungu, bali nitakuwa mwalimu wa kuwafundisha wengine Neno hilo la Mungu.Ninawashukuru sana kwa kazi hii yenye neema kubwa na ninaomba Mungu awabariki sana. Amen!
God Almighty bless you so much