Pastor asema mafuriko na matetemeko ya ardhi bado!

Mtume Brain Carn amesema kwenye moja ya kusanyiko lake kwamba, Matukio ya kutikisha dunia bado hayajaja yanakuja makubwa zaidi kama watu hawataziacha njia zao mbaya na kumrudia Mungu.

Ameongea hivyo baada ya kimbunga Isaac kilichofika New Orleans. Katika maongezi yake hayo, watu wengi wamejitokeza kupinga kwamba Mungu hawezi kuhukumu nchi na kuacha wanadamu wapate shida. Akauliza swali, kama Mungu aliweza kufanya kipindi cha Sodoma na Gomora atashindwaje kwa kipindi hiki kiovu?

Tukio hilo limetafsiriwa na watu tofauti wengine wakisema ni Baraka kwa sehemu zilizokuwa na ukame na wengine akiwepo Buster Wilson kusema ni adhabu kwa wakazi wa New Orleans kwa sherehe za mashoga na wasagaji zinazotarajiwa kufanyika mwezi huu.

 

3 thoughts on “Pastor asema mafuriko na matetemeko ya ardhi bado!

  1. Watu wa Mungu tuwe macho hata kipindi cha Nabii Nuhu watu walimcheka mafunuo hayaji kwa kila mtu kama matangazo ya mpira.Biblia inasema wanitafutao kwa bidii wataniona inamaana kwa wale wasio mtafuta Bwana mambo yatafanyika bila kuambiwa kitu.Lakini kwa wale wanao mcha Mungu hawatafichwa kitu.Ona mfanokwa wale malaika waliotumwa kwenda kuangamiza Sodoma na Gomola hawakuweza kumpita mtu wa Mungu Ibrahimu walimwambia wanakwenda kufanya kitu gani Sodoma. Mbarikiwe watu wa Mungu!!!!!!!

  2. Amen, Mungu awabariki wenye macho ya kuona kwa ajili ya wengine, masikio ya kusikia, na ufahamu wa kufahamu kwa ajili ya wengine. Amen

Andika maoni yako