Tuukomboe Wakati

Nini maana ya Ndoto hii?

wp-1449637914393.jpeg

Shalom wana Blog!

Naombeni kuambiwa maana ya ndoto hii kwani sio mara moja nimeota.

Kuota unapanda sehemu yenye mteremko sana(kilima) tukiwa na wenzetu lakini mimi hufanikiwa kupita, kisha kufanyiwa uchawi na watu nisowajua, na kuzungukwa na mapepo lakini huwa nayakemea sana kisha kutoweka.

Maana yake ni nini?

Mimi Sia

Shalom!

Adui King’ang’anizi

 

wpid-index.jpeg

 

Mhhh!

Maadui wengine kwenye maisha wako kama
Farao!

Unakutana na mtu kazini, kwenye biashara au
katika uwanja mwingine wowote wa maisha.
Inatokea tuu anakuwa adui yako pengine kwa
kusikiliza maneno ya uongo ya kuwachonganisha,
anayakazia kamba, anakuwa adui na kujiapia
kwamba atakula na wewe sahani moja! Au tuu
inatokea ulitaka kumshauri jambo, anageuza post,
inakuwa wewe ndiyo unajifanya unajua kila kitu,
anaanza kupambana na wewe ili udhaifu wako
auweke hadharani!

Kwa yule inayewezekana kujitenga naye
unajitenga, unahakikisha huingii katika “18” zake,
ukijua yatakwisha! Lakini wapi. Utashangaa
anaanza kupeleleza shughuli unayoifanya na
kutaka kukusanya data kwa kila mtu
anayekufahamu ili tuu apate pa kukutafutia
sababu akufuate huko huko uliko, pamoja na
kuwa ulishampisha kabisa katika uelekeo wake
wa maisha!

Anaanza kutafuta ulipopita ili na yeye akufuate!
Hapati raha kama hajapata nafasi
yakukukarahisha na anaweza akazua jambo
kubwa la kukusingizia ili tuu uadui uendelee
kuimarika na watu wakuone kumbe hufai!
Sasa unaanza kuwaza: Mbona huyu
nilishamuachia mambo ya maisha yake? Mbona
kama ni ofisi tulitengana kila mtu akabakia na ya
kwake?? Mbona nilishahama kabisa toka kwenye
kampuni anayofanyia yeye kazii?? Sasa kwa nini
bado ananifuatilia??

Ndipo linakuja jibu hiviiii: Kuna watu wana “roho”
ya Farao!
Wana wa Israel wameshakwenda zao lakini bado
jamaa aliwafuatilia hadi ndani ya baharii!!
Huyo mtu anayelazimisha vita na mtu asiye na
hatia mwisho wake ni lazima uwe kama jeshi la
Farao: Kumezwa na bahari!!

Solution: Ukiona mtu wa namna hii yuko nyuma
yako, kila ukibadilisha gia, na yeye anabadilisha.
Ukiingia garini na yeye anaingia; ukisema ngoja
nimuachie ntasafiri kwa trekta na yeye anashuka
anapanda trekta: Ukibadili namba ya simu
unashangaa kishaipata na anaendelea
kukuandikia sms za maudhi na vitisho-bubu….

Ukimuona mtu wa Hivyo Kaza Kumtazama
Mungu! Tafuta uso wa Mungu aliye Mtetezi wa
wenye haki! Kwa Hakika Mungu atakuelekeza
kwenye Bahari…siyo lazima iwe ya Shamu!
Itafika tuu mahali Mungu atamshughulikiaa na
atapotelea humo na ndiyo unakuwa mwisho wa
kumuona tena akisumbua sumbua maisha yako!

(Na ole wako wewe ambaye itamlazimu Mungu
akushughulikie ili mtu wake, mcha Mungu wake,
apate Amani maishani mwake!!!)

Wanadamu tupendaneni!

John Paul

KAZI na FAMILIA

family

Haina maana yoyote kusifiwa kuwa wewe ni kiongozi mzuri, manager mzuri, Mchungaji mzuri, halafu wakati huo huo familia yako ikawa katika mapungufu makali kwa sababu baba au mama hana muda na familia yake kwa kisingizio cha majukumu mengi!! Kwa kisingizio cha kutafuta pesa, shame!

Eti kwa sababu baba ni mbunge, ni waziri, ni CEO wa kampuni, ni mfanyabiashara au vyovyote eti hana muda na familia yake! Hii ni uzembe wa hali ya juu tena juu sana! Kuwa na kazi nyingi haikuhalalishii wewe, baba au mama kuisahau familia yako!

Ni kweli umefanya vizuri sana, biashara yako imeendelea sana ni sawa, ni kweli unaongoza kampuni vizuri sana ni sawa, ni kweli ni Mchungaji mzuri sana Kanisa limesimama imara kwa sababu yako. Lakini familia yako umeisahau, sisi wanafamilia tunahitaji muda na wewe, tunahitaji malezi yako, tunahitaji upendo wako, tunahitaji uwepo wako nyumbani katika wakati sahihi, tunahitaji connection na wewe, tunahitaji uongozi wako!

Eti unawadanganya watoto kwa kuwapa kila kitu wanachohitaji na wasivyohitaji (physical things). Simu kali, usafiri kwenda shule wanapelekwa, I-pads, Computer games, vyakula vya kila aina, vingi vikiwa processed viwandani matokeo yake unawaharibu afya. Ni kweli umefanya vizuri, lakini hii ndo inaitwa being SUCCESSFUL IN A WRONG THING! Unadhani maisha ni vitu? Jamii inabaki kukushangaa tu, mbona yuko vizuri sana lakini watoto wake mmoja tu ndo amesoma, wengine wamekataa shule, wanavuta bangi, ni wezi, ni wakorofi, wamezalishwa zalishwa tu! Wakati mwingine unaiga mambo ya wazungu, sasa wewe ni mzungu? Acha kuigaiga, unapotea!

Nelson Mandela ni kiongozi aliyepita ambaye kwa Afrika nzima na hata dunia yote wengi au wote walimkubali kuwa HE WAS A GREAT MAN in leadership and humility. Lakini tunaweza kusema, he was SUCCESSFUL IN A WRONG THING! Maana Hakupata muda na familia yake, matokeo yake watoto wake 4 wamekufa na HIV/AIDS. Jambo la kusikitisha sana!

Wako wachungaji wanakuwa committed kweli kweli kwenye kulea Kanisa, familia inamkosa baba. Yupo nyumbani kila siku kumbe hayupo, kwa macho yupo na sisi kumbe hayupo! Matokeo yake watoto mpaka wanaichukia kazi ya uchungaji!

Ukweli ni kwamba, kama huna muda juu ya jambo fulani, fahamu kuwa jambo hilo si MUHIMU KWAKO, halina MAANA KWAKO. Je, familia yako (mke au mume, watoto) ni wa muhimu kwako?? Au ATM CARD yako ni muhimu kuliko mtoto wako wala mke au mume wako! Tatizo umeweka fedha mbele sana kuliko utu, tena uliingia kwenye ndoa kwa kufuata MAZOEA, hujui kulea familia, hujafundishwa wala hutaki kujifunza. Ndo maana unaacha familia Arusha wewe unaishi Dar, familia Mwanza wewe Morogoro! Hayo siyo maisha bali ni utumwa wa maisha. Jifunze nini maana ya familia, malezi yake, nini wanahitaji toka kwako ili uwe BABA au MAMA mzuri. Familia kwanza ndiyo utakuwa kiongozi mzuri, anayejitambua. Huwezi angalia kutafuta fedha tu halafu familia inaharibika, fedha hizo hazina maana kama familia yako imeparanganyika.

Jamii yetu ina watu wasiojitambua, wezi, hawajiamini, waongo, wachakachuaji, wasiojituma, wavivu, wazembe, wala rushwa na mafisadi wengi maana wazazi wao hawajafundishwa namna ya kulea familia, hakuna malezi kwa watoto maana wanazaliwa na kuachwa watafute wenyewe nini maana ya maisha, nini maana ya kuwa mtu katika jamii, matokeo wanajifunza kwa wezi, mafisadi, wavivu nk. Ee Mungu tusaidie kuifahamu kweli!

Connect na watoto tangu uchanga wao hadi unapowaozesha, ili uwaonyeshe nini maana ya maisha, nini maana ya kuwa mtu katika jamii. Wafundishe ili wajitambue, endelea kuwa-mentor katika ubaba au umama wao pia. Ukiwaacha wawe wakubwa ndiyo uwe karibu nao tayari watakuwa wamejitengenezea mifumo ya maisha yao, na wewe wanakuona STRANGER kwenye mifumo waliyotengeneza. Kuwa baba au mama acha kujifanya uko busy, kwa nini ulianzisha familia kama uko busy???

Mungu utusaidie kuiona kweli, tukafanye kama inavyopaswa kuwa ili kukuza familia zenye michango katika jamii. Amina.

NOTHING CHANGES UNTIL YOUR MIND CHANGES!

Theophil

Sala ya Bwana

 beautiful-theme-with-the-lords-pray
Bwana Yesu asifiwe!
Napenda niwashirikishe kuhusu SALA YA BWANA ambayo watu wengi tunaijua. Tutakwenda  kuona ufafanuzi ambao unaweza kutusaidia ili kuweza kujua namna sahihi ya kutumia.

Sala hii ya Bwana inapatikana katika kile kitabu cha Mathayo 6:9-13:

9: Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,
10:Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.
11:Utupe leo riziki yetu.
12:Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
13:Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]Sala ya Bwana ni fupi sana lakini ina mapana yake kwa kuzingatia vipengere mbalimbali.
Katika sala ya Bwana kuna  vingere SABA (7) vya muhimu;
1. BABA YETU ULIYE MBINGUNI JINA LAKO LITUKUZWE.
Katika kipengele hiki mwombaji anapaswa kuwa na kipindi cha kumsifu na kumuabudu Mungu kwa majina yake, kabla ya kupeleka mahitaji yake, tambua kuwa Mungu anakaa Katika sifa
Jizoeze kumsifu na kumwabudu Mungu kwa majina Yake maana kila Jina Linabeba sifa za Mungu2. UFALME WAKO UJE HAPA DUNIANI
Katika kipengere hiki Yesu anatufundisha kufanya vita vya kiroho, kuvunja kazi za shetani na kuharibu nguvu za giza na kuzipinga hila za shetani ili kuruhusu ufalme wa Mungu uchukue nafasi.
Kumbuka kuwa shetani alitupwa dunia na amejenga ufalme wake, hivyo kuomba ufalme wa Mungu uje duniani ni kutangaza vita na mapambano dhidi ya ibilisi shetani. YAKOBO 4:7; 1PETRO 5:8-93. MAPENZI YAKO YATIMIZWE DUNIANI KAMA MBINGUNI
Katika kuomba kwetu ni muhimu sana kutafuta kuyajua mapenzi ya Mungu kwa watu wake duniani ambayo anataka yatimizwe.
Ukiisha yajua mapenzi hayo ya Mungu ni muhimu kukaa Katika kuyaombea ili yatimizwe Katika maisha yako.
Mapenzi ya Mungu hujulikana kwa kusoma na kusikiliza Neno la Mungu.
Mfano ni mapenzi ya Mungu watu wote waishi kwa Amani na utulivu (1TIMOTHEO 2:1-2),  ni mapenzi  ya Mungu watu waponywe magonjwa yao na kudumu Katika afya njema (3YOHANA 1:2)
NB: kuwa msomaji na msikilizaji mzuri wa Neno la Mungu kutakuwezesha kuyajua na kuyatambua mapenzi ya Mungu kwa watu wake walioko duniani.

4. UTUPE LEO RIZIKI YETU
Hiki ndiyo kipengere ambacho, mara nyingi, lengo la mwombaji yeyote hulenga.
Hiki ni kipengere ambacho mwombaji anatakiwa kupeleka mahitaji yake mbalimbali mbele za Mungu sawa sawa na haja za moyo zilivyo. Yawezekana ni mahitaji yanayotuhusu moja kwa moja sisi, lakini yaweza kuwa ni ndugu,  marafiki, majirani, nchi au taifa.
Na hapa Yesu alisema tunaweza kuomba lolote Katika Jina lake na Baba wa mbinguni atatenda
Soma YOHANA 14:13; MATHAYO  7:7-14, ISAYA 43:26.

5.UTUSAMEHE MAKOSA YETU
Katika muda wako wote wa maombi unatakiwa kupata muda wa kwenda mbele za Mungu kwa Toba ili kuungama na kutubu juu ya makosa mbalimbali ambayo huwa tumetenda kwa uovu mbele za Mungu.
Kumbuka neno linasema tukisema hatuna dhambi twajidanganya wenyewe na kweli haimo ndani mwetu, lakini tukiziungama dhambi zetu Mungu ni Mungu mwenye haki na rehema atatusamehe maovu yetu na kutusafisha dhambi zetu…1YOHANA 1:7-9
Pia hapa tunapata wakati mzuri wa kuomba Toba kwa ajili ya wengine, jamii yetu, kanisa lako, ukoo wako, kabila lako na taifa lako. Kama alivyofanya Daniel (DANIEL 9:1-19).

6.USITUTIE MAJARIBUNI BALI UTUOKOE NA YULE MWOVU (Shetani na hila zake na kazi zake)
Katika muda wako wote wa kuomba ni muhimu kupata nafasi ya kukiri na kuombea maeneo yako ya udhaifu ambayo yanaweza kukutia katika majaribu (YAKOBO 1:13-14).
Kukiri udhaifu mbele za Mungu na kumkabidhi Mungu udhaifu huo; husaidia sana ili shetani asije tumia udhaifu huo na mtu wa Mungu ukaingia Katika kumkosea Mungu na kuishi kinyume cha mapenzi ya Mungu.
Kila mmoja ana udhaifu wake kwa mfano:-hasira za haraka, masuala ya pesa, tamaa za mwili (zinaa na uasherati), matumizi ya ulimi (uongo,usengenyaji) na udhaifu wowote unaoujua mwenyewe.
Ni vema tena ni muhimu kupata muda na nafasi yakukiri  na kuombea maeneo yako ya udhaifu ambayo yanaweza kukutia Katika majaribu  mbele za Mungu.
7.KWA KUWA UFALME NI WAKO NA NGUVU NI ZAKO NA UTUKUFU NI WAKO TANGU SASA NA HATA MILELE
Kama mwanzo unapotaka kuanza maombi lazima kuanza kwa kumsifu na kumwabudu Mungu, vivyo hivyo mwombaji unatakiwa kumaliza maombi yako kwa kumsifu na kumtukuza Mungu. Mungu wetu hupenda sana kusifiwa na anatakiwa kusifiwa na kutukuzwa kila wakati (ZABURI 113)

Katika kipengere hiki cha saba tunaona Bwana Yesu anatufundisha sisi kama watu wake kufungua maombi yetu kwa kumsifu Mungu na kumtukuza pia anatufundisha kumaliza maombi yetu kwa kumsifu na kumwabudu Mungu. Jizoeze kila wakati uwapo Katika maombi Kumsifu na Kumwabudu Mungu pindi uanzapo na umalizapo (ZABURI150:6; ZABURI 33:1-5)

Kwa kuzingatia ufafanuzi huu tunaweza kuona kuwa kumbe  SALA YA BWANA siyo kitu cha kukiimba kwa kukariri kama tulivyozoea kufanya bali Sala ya Bwana ni muhutasari tu wa mambo muhimu yaliyopo katika kipindi cha maombi . Sala ya Bwana ni vipengele muhimu vya kuombea, pale tupatapo muda wa sala na maombi.

Asante na Mungu awabariki!!

Samwel Mmasa

Utasimama Wapi?

that_cry_behind_you

Hezekia alipougua ugonjwa ambao aliambiwa utamsababishia Kifo alilia mbele za Mungu, akamkumbusha jinsi alivyokwenda mbele zake kwa UKAMILIFU na Unyoofu wa Moyo na Mungu akamponya. (2Wafalme 20:1-7).

Mtu huyu wa Mungu alikuwa amejitengenezea Hazina na Ushahidi wa kumfanya akumbukwe na Mungu. Mungu alikubaliana kabisa na maisha ya Hezekia kwamba yalikuwa ni Mema!

Katika Kitabu cha Hosea 6:1 kuna maneno haya:

Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu.

Hapo tunaona jinsi watu wa Mungu walivyojikuta katika matatizo kwa kuwa Mungu mwenyewe ndiye aliyekuwa Amewararua. Hawa wakawa wanahimizana Kumrudia Mungu kwa kuwa ni mwenye Rehema. Hawakuwa na ujasiri wa kusema wamwambie Mungu angalau jema fulani walilofanya kwake.

Maandiko hayo mawili yanaonyesha namna mbili za kwenda mbele za Mungu. Aliyotumia Hezekia na hii inayoelekezwa katika Hosea.

Ni changamoto kwetu leo kwamba Ikitokea umepatwa na tatizo, utatumia njia gani wakati wa kumuomba Mungu akutoe katika shida hiyo?

Utamkumbusha mema uliyotenda au Utaomba rehema zake tuu ndiyo zikubebe? Je, tuna ujasiri wa kumwambia Mungu kwamba kuna mema kadhaa ambayo basi hata Mungu ayaangalie hayo ili aiondoe shida iliyopo mbele?

Ni jambo la kutafakari kwetu sote!

JP