Bwana wa Majeshi ya Mbinguni ndiye Bwana wetu leo, Bwana wa Majeshi ya Israeli ndiye Bwana wetu leo, ni yeye yule jana leo na hata milele “Yehovah Sabaoth”! Kamanda na Komandoo…Amiri Jeshi mkuu na Bwana wa Vita …anasimama kwa ajili yetu, upande wetu, katikati yetu Shujaa aokoae kishujaa…Tunasonga mbele! tunakaza buti, Tunapasua mawimbi, tunamtazama aliyeianzisha kazi njema mioyoni mwetu yuko pamoja nasi hadi tumalize kazi.. tunatiwa nguvu mpya, kama Tai tunapaa, ujana wetu unarejeshwa, tu majasiri kama Simba. Pamoja kwa umoja katika Roho mtakatifu tuna kazi Kubwa mbele, kuhakikisha wanyonge wanainuliwa, dhaifu wanapata nguvu, maskini wanafanikiwa, walio mbali wanafikiwa, wenye dhambi wanatubu, wagonjwa wanapona, mapepo yanatoka, hofu ya Mungu inatawala, na Bwana wetu – Nyota ya alfajiri, Simba wa kabila la Yuda, Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana, Alfa na Omega ANATUKUZWA kuanzia mioyoni, makazini, kwenye biashara, makanisani, mashambani, angani na ardhini …Ulimwengu ujue nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, na kwamba hakuna jina lingine juu ya JINA LA YESU. Kila goti lijiandae kwenda chini, kila ulimi ujiandae kukiri ya kuwa YESU NI BWANA! utukufu heshima na adhama vina MUNGU wetu BABA YETU! katika JINA LA YESU.
–Pastor Abel Orgenes