Nahitaji Maombi na Ushauri

Questions and clear strategy and solutions for business leadership with a straight path to success choosing the right strategic path with yellow traffic signs cutting through a maze of tangled roads and highways.

Bwana Yesu asifiwe!

Haja ya moyo wangu kwa Wakristo wenzangu hapa Strictly Gospel ni kuomba ushauri pamoja na kuhitaji muungane nami katika kuliombea suala hili.

Mimi ni kijana nimeokoka  na ni mzaliwa wa kwanza kwenye familia yetu na mzaliwa wa kwanza kiroho kwa sababu Mungu alianza kuniokoa mimi ijapokuwa nina ndugu zangu wameokoka lakini bado hawajapokea neema yakuweza kusimama na Kristo.

Lililonileta ni suala hili kwamba nipo kwenye vita na sijajua nifanye nini kwenye jambo hili lililonipata mwaka huu. 

Nyumbani kwetu tuna mdogo wetu wa kike ambaye ni mtoto wa mwisho. Tatizo lililojitokeza nilianza kuota ndoto juu ya mama yangu mzazi. Nilikuwa naota nawaona watu wanamuita majina mabaya sana. Nikiota hivyo mimi nakuwa nabishana nao ndotoni, nikiwakemea kuhusu maneno yao, lakini wao walikuwa wananishangaa sana.

Hapo mwanzo sikuwa naelewa nini kinaendelea. Lakini wakati nakaribia kurudi likizo nyumbani, kwani nilikuwa nipo muhula wa kwanza mwaka wa tatu namalizia masomo yangu ya shahada ya kwanza katika moja ya vyuo vikuu Tanzania, nilikuwa nasikia kuna wimbo wa injili wenye maudhui ya kumsihi Mungu anipe nguvu nisikate tamaa. Hapo sikuelewa kwa nini wimbo huu ulikuwa unakuja hasa asubuhi tu pale ninapoamka, unakuja kichwani. 

Ndipo niliporudi nyumbani nikakuta habari mbaya sana ambazo sikuzitarajia maishani. Nilianza sikia kwa watu baki ya kuwa mama yangu anamkuwadia (anamtafutia wanaume) mdogo wangu ambaye alikuwa ana umri wa miaka 17 kwa wakati huo. Yeye ni wa kike na wa mwisho kwa wanaume. Sababu ya mama kumkuwadia ni eti ili apate pesa ya kulipa madeni!

Kwa kweli kama mtoto mkubwa niliposikia habari zile nikaamua kuongea na mdogo wangu, mimi kama kama kaka, na kutumia mbinu za kisaikolojia kumhoji. Baada ya kumhoji dipo akaniambia habari zote ambazo zilinifanya nikaunganisha ndoto ile niliyoiota siku za nyuma na ule wimbo uliokuwa unanielekeza nimuombe Mungu anipe nguvu nisikatee tamaa. Pamoja na hayo nilisikia na mengine mengi sana kiasi kwamba yalinihuzunisha na yaliniumiza na kunifanya niingiwe na uchovu wa kiroho ambao umenigharimu sana roho yangu.

Mdogo wangu huyo sasa kawa mjeuri sana. Ameshatoroka nyumbani kama mara nne; tunamtafuta; tunamrudisha.

Huku napo baba yangu maisha yake ndiyo siwezi elezea maana hayampi Mungu utukufu. Kwa kifupi ni kwamba roho za uzinzi na uasherati zimeivamia nyumba yetu. Wazazi wangu sasa wametengana na baba yangu anataka kuoa mwanamke, tuseme msichana, ambaye kwa kukadiria nimempita umri au tumelingana. Vita vimepamba moto kama asingekuwa Mungu, chuoni ningefeli kwasababu kuna wakati nilikuwa nashindwa kabisa hata kusoma!

Sasa nalileta kwenu, ndugu zangu katika Kristo, mnishauri hapa nifanya nini. Sambamba na ushauri huo ninaomba mniombee ili Mungu aiponye familia yangu.

By C.P

Furaha imetoweka nani ya Nyumba!

maombi2

Wapendwa katika Kristo!

Tumsifu Yesu Kristu! Nimefaidika na kufarijika sana kwa mafunzo mbalimbali kwenye blog hii! Mubarikiwe. Nipo katika shida kubwa kimaisha! Pamoja na bidii nyingi uchumi kwangu kwa miaka 4 sasa umezidi kudidimia kiasi kwamba Hata kula imekufa shida! Ada za shule, mavazi ni duni! Madeni yamezidi hayalipiki. Watoto wangu wamekua kama yatima furaha imetoweka ndani ya Nyumba. Mifugo yangu na rasilimali zangu ziko mashakani, tayari moja ya mashamba yangu lipo kwenye hati hati ya kupokonywa. Mipango yangu haiendi nimetoka uza baadhi ya ardhi yangu ipi kujikwamua kiuchumi kwa mipaka kadhaa sasa sifanikiwi na sasa hali ndio mbaya! Naomba Msaada wenu wa mombi. Mungu awabariki! Amen.

–Lourance M

—————————-
Wapendwa naomba utamke kitu juu ya mama huyu furaha iliyotoweka kwenye nyumba yake irudi  Mungu afanyaye njia pasipo njia akaonekane na kufungua njia kwake kwa jina la Yesu Kristo. Omba kwa kadiri Roho wa Mungu atakavyokuongoza!

Nimeokoka lakini nakandamizwa na majinamizi!

jinamiziNaombeni mnisaidie ni miaka zaidi ya 10 toka niokoke lakini ninatatizo moja la kukandamizwa pindi nilalapo, saa nyingine nahisi kabisa mtu amenikalia mgongoni, mara nyingine nkilala kifudifudi nahisi kitu kinaingizwa katikati ya makalio,pia kuna kipindi nilikuwa naamka usiku saa 9 kusali kila siku ndio mambo yakazidi yaani nkimaliza kusali sitolala ntafanyiwa hivyo vituko mpaka kunakucha, nisaidieni jamani nimechoka sana, hali hii ikinitokea nakuwa sina hata uwezo wakujitingisha hata kidole..mbarikiwe

— NS

Tafadhali popote ulipo tamka Neno juu ya ndugu yetu na hali hiyo ikamwache mara. Katika jina la Yesu!

Maombi juu ya Uponyaji wa mwanangu!

maombi

Ndugu Katika Damu ya Yesu,

Bwana Yesu asifiwe, wapendwa katika Jina la Yesu Kristo naomba kuwashirkisha katika maombi kwa ajili ya kijana wangu anaitwa SEBASTIAN S.KASENGA, huyu ni motto wangu wa kwanza, alihitimu mwaka jana Shahada ya Kwanza katika Chuo kikuu cha Dodoma – UDOM. Tatizo linalomsumbua ni Nervous System- miguu kukosa nguvu na mikono kutetemeka akishika kitu, kwa hali hii inamsumbua sana hawezi kutembea kwenda hata mita 10 mwili unachoka, bado naendelea na matibabu hospital. Imani yangu kubwa ni kwenye Maombi katika jina la Yesu Kristo naamini uponyaji utapatikana, ndiyo maana nawashirikisha wapendwa.

Bwana Yesu Asifiwe;

Naitwa: Samwel Kasenga – mkazi wa Kimara,