Reinhard Bonnke na Huduma ya Africa

Nigeria hivi karibuni!

Mwinjilisti wa kimataifa Reinhard Bonnke amejulikana kwa mikutano mikubwa anayoifanya Afrika. Ni mtoto wa mchungaji, alimpa Yesu maisha yake akiwa na miaka tisa (9) na Mungu alimuita kufanya kazi katika bara la Afrika tangu akiwa kijana mdogo na kuanza na mikutano yake maarufu kama “Fire Conference”

Katika mikutano yake ya Injili watu wengi wamekuwa wakimpa Yesu maisha yao,  Imekuwa ni furaha ndani ya moyo wake kuona watu waliopotea wakija kwa Kristo!

Katika miaka 35 tangu ameanza huduma yake ya kimataifa ijulikanayo kama Christ for all Nations (CfaN) ambayo ina ofisi Marekani, Kanada, Ujerumani, Uingereza, Nigeria, Afrika kusini, Singapore, Austraria na Hong Kong. Pamoja na kuhubiri Injili amekuwa akionesha filamu zenye changamoto kwa kanisa na Uinjilisti wa Roho Mtakatifu.

Bonnke ameweka historia kwenye kazi ya Mungu, Afrika haitamsahau na dunia haitamsahau kwa kazi amefanya, Mungu ambariki baba huyu kwa kukubali wito unaobadilisha maisha ya watu wengi, ni mume wa Anni, watoto wake ni Kai-Uwe, Gabrielle na Susie, pia ni babu wa wajukuu nane.

10 thoughts on “Reinhard Bonnke na Huduma ya Africa

  1. Nimekisoma hiki kitabu kiko vizuri. na mimi nasema uinjilisti ni moto sio mabishano ya akili za kibinadamu. Injili ni nguvu ya Kristo. BABANGU KRISTO AWATIE NGUVU.AMEN

  2. Hicho kitabu kinapatikana wapi wateule wa MUNGU au naweza kukipata wapi?

  3. Kweli,kitabu cha uinjikisti kwa moto ni moto ,mi ninacho na sihoki kukisoma,Mungu wabariki watumishi wako,Mungu nibariki Mimi,Amin!!

  4. even to me i like so much his preaching he is a good teacher.GODBLESS HIM SO MUCH.

  5. mkimpa m2 asome kitabu cha bonnke cha mwinjirist kuwa moto kama wew n mwijirist haswaaaaaaaa hakika utawaka moto ndaan ya roho yako utasukumwa na nguvu ya ajabu ktk huduma nakpenda hcho ktabu hebu wainjirst tafuten hcho kitabu mpate kujifunza mengi

  6. Pls pray 4 me 2 God,so that i may be strong in prayers. God bless u people.

Andika maoni yako