6 thoughts on “Vijana mitaani!

  1. Wachapwe fimbo kabisa. Hawana adabu. Mnatulalamikia sana wasichana kwanini na wao wasiachwe? maana hakuna jipya

  2. Wapendwa,

    Kwani hapo la ajabu ni lipi? Mimi nakumbuka wakati nikiwa kijana wa miaka 14-17 miaka ya 1980 mitindo hiyo ya mlegezo tulikuwa tunaivaa sana. Mimi nakumbuka nikiwa darasa la 6 hadi 7 na nilipokwenda sekondari miaka ya 90 kuvaa milegezo ilikuwepo. Sasa hapa la jabu lipi. Hakuna jipya hapa duniani.

  3. Wala mimi sioni sababu ya serikali kuingilia kati!!!!! sisi tuwahubiri injiri harafu tumuachiye Roho mtakatifu awatengeneze kweli kweli. tusije tukajikuta tumesafisha vikombi nyuma kumbe ndani huuuuuu!!!!!!!
    Kumbukeni katika Biblia Bwana hujiita mfinyanzi; na ni mfinyanzi wa kweli!!! Alinifinyanga bwana!! Yeye ni fundi stadi.
    Wapendwa; yule mtu aliye kuwa na mapepo ya kumtuma ku kaa makaburini Yesu hajawahi kumuambia avae; lakini alipo fukuza mapepo wale, mzee alivaa na kuka pamoja na Yesu kwa utulivu. Tuelewe kwamba mtu hutawaliwa katika ulimwengu wa roho! Lile ni pepo linawatuma kutembea uchi; Paulo hajatwambia kuita polisi tunapo vaamiwa na vikosi vya mapepo; anasema tuvae siraha zote za Mungu. Ebu tusome pamoja II korinto 10:4-7
    Wapendwa , shetani ni muongo sana na ni mjanja sana; sasa tuwe makini asitupotezee mda wetu. Ninawapenda sana tena sana.

  4. Watoto sio jukumu la serikali pekee. Mi ningeshauri hata wazazi na waalimu wahusike kuangalia maadili.Si kwa vijana wa kike peke yake.

  5. Iko lazima,Tena ni lazima sana. Sio kwa vijana tu but kwa wasanii, watu wa media etc, among others.

    Na hii (pamoja na nyingine nyingi) ni moja ya agenda za kuzipendekeza kwenye mchakato wa ukusanyaji wa maoni kwa ajili ya kupata katiba mpya ili ipitishwe iwe sheria ya mavazi na uvaaji wa staha maana sasa tuendako siko.

    So wapendwa ambao hamjachangia maoni yenu fanyeni hivyo, mimi nimei-raise issue hiyo jana ktk uchangiaji wa maoni nawee ambaye bado fanya hivyo now hao jamaa wakifika uliko.

    Be blessed.

  6. kwa kweli ni jambo la kushangaza sana. mimi mwenyewe binafsi inaniumiza kupita kiasi. si kwa vijana wa kiume tu sasa nina shangaa imeingia mpaka kwa wasichana. Tumwombe Mungu sana kwa ajili ya haya kwa kulia na kuomboleza na kuvaa magunia. tusimamie zamu yetu tusisubiri kutoa coments. Ibrahimu aliona kama watano wangelipona basi lakini hakuingia zamu yake. matokeo yake asubuhi aliambulia kuona moshi ukifuka. tayari sodoma na gomora ilikuwa imekwisha teketezwa. mwanzoni nilisoma kwenye magazeti kuwa huko marekani wanadai mtu akivaa hivi manake yupo tayari kwa kugeuzwa nyuma. sasa kwa uafrica wetu tusiruhusu hili. daniel aliomba mpaka malaika waka mjulisha ni kwa nini maombi yalikuwa hayajibiwi na sisi tufike hapo. tuombe na tuamini majibu yapo na hii tabia itakuja kutoweka tu. mambo yanakuja na kuondoka na hili pia litaondoka. Mungu na atupiganie.

    Hellen Lyimo

Andika maoni yako